PistolGang
JF-Expert Member
- Jan 16, 2013
- 392
- 44
Habarini ndugu, rafiki na jamaa zangu wa humu?
Nina swali la kupewa ufumbuzi kimsaada zaidi. Hii itawahusu wazazi wote na wataalamu wa maswala la watoto wachanga.
Stori inaanza hivi; Ni takribani miezi miwili na siku kadhaa tangu mke wangu ajifungue mwenetu kipenzi (Alhamdulillah) amejaliwa afya njema na kilo zinaenda vizuri.
Ila swala ni kwamba mimi na mke wangu sote ni wafanyakazi, hivyo mke wangu anakaribia kurudi kazini baada ya kumaliza zile siku za kupumzika.
Hofu kwa mwenetu ambae haipiti nusu saa bila kunyonya pale anapokua macho (hajalala) na mama yake wiki ijayo anaanza kwenda kazini (Atakua anaenda saa2 asbh na kurudi saa6 na nusu mchana) na kuna umbali kidogo mahali tunapoishi na kazini kwake, ni takribani masaa 4 na nusu atakua mbali na mtoto kwa siku zote za kazi ( I hope ndivyo ilivyo kwa wazazi wote ) kwa muda huo mtoto atakua yupo na dada wa kazi nyumbani.
Hivyo, tatizo la njaa litakua kubwa sana na tumeambiwa/inafahamika mtoto atakiwi kula chochote mpaka afikishe miezi sita.
Juzi katika pita pita zangu kwenye BabyShop/KidsCorner nimeona kijidude cha kukamulia maziwa ya mama na contena lake la kuhifadhia kwaajili ya kumnyonyeshea mtoto pale mama atapokua mbali.
Swali linakuja hapa; Je, maziwa ya mama yanapokamuliwa na kutuzwa kwa muda ni salama kwa mtoto? Kama ni salama yakae kwa muda gani kabla ya kuharibika? kama si salama, ni njia ipi ya kum_feed mtoto kwa situation hiyo (hapo juu)?
Nahitaji Msaada:
Nina swali la kupewa ufumbuzi kimsaada zaidi. Hii itawahusu wazazi wote na wataalamu wa maswala la watoto wachanga.
Stori inaanza hivi; Ni takribani miezi miwili na siku kadhaa tangu mke wangu ajifungue mwenetu kipenzi (Alhamdulillah) amejaliwa afya njema na kilo zinaenda vizuri.
Ila swala ni kwamba mimi na mke wangu sote ni wafanyakazi, hivyo mke wangu anakaribia kurudi kazini baada ya kumaliza zile siku za kupumzika.
Hofu kwa mwenetu ambae haipiti nusu saa bila kunyonya pale anapokua macho (hajalala) na mama yake wiki ijayo anaanza kwenda kazini (Atakua anaenda saa2 asbh na kurudi saa6 na nusu mchana) na kuna umbali kidogo mahali tunapoishi na kazini kwake, ni takribani masaa 4 na nusu atakua mbali na mtoto kwa siku zote za kazi ( I hope ndivyo ilivyo kwa wazazi wote ) kwa muda huo mtoto atakua yupo na dada wa kazi nyumbani.
Hivyo, tatizo la njaa litakua kubwa sana na tumeambiwa/inafahamika mtoto atakiwi kula chochote mpaka afikishe miezi sita.
Juzi katika pita pita zangu kwenye BabyShop/KidsCorner nimeona kijidude cha kukamulia maziwa ya mama na contena lake la kuhifadhia kwaajili ya kumnyonyeshea mtoto pale mama atapokua mbali.
Swali linakuja hapa; Je, maziwa ya mama yanapokamuliwa na kutuzwa kwa muda ni salama kwa mtoto? Kama ni salama yakae kwa muda gani kabla ya kuharibika? kama si salama, ni njia ipi ya kum_feed mtoto kwa situation hiyo (hapo juu)?
Nahitaji Msaada: