Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
"MAZOEA" YAKO HUJENGA MWAMBA MGUMU KATIKA MOYO WAKO
Anaandika Robert HERIEL
Yule Shahidi
Ingawaje maisha yanatufundisha tusiwe na MAZOEA kila siku, hayataki tuzoee lakini Sisi ndio tunalazimisha kuwa na MAZOEA, ndio maana leo ni tofauti na Jana, na kesho itakuwa mbali na siku ya leo. Wala hatujui nini kitajiri kesho, na hata hiki cha leo hatukujua Kama kingekuwa hivi. Ndivyo nilisema, maisha ni mzunguko wa mambo mapya yaliyozaliwa na mambo ya zamani, tena kesho ilitoka katika siku ya leo. Ijapokuwa kila siku yajitegemea na inajitosheleza, lakini kusudi ni moja katika muunganiko wa maisha.
Mazoea ni kufanya Jambo moja, lilelile kila mara, huitwa mazoea, desturi, kawaida na Amali. Kufanya kitu kila mara huzaa mazoea, kisha kikishakomaa na kinatengeneza TABIA, Tena tabia hukua na kukomaa na kurithishwa kutoka kizazi kimoja mpaka kizazi kingine, wakati mmoja mpaka wakati mwingine, Zama moja mpaka nyingine, na hapo huzaliwa mwamba mgumu uitwao ASILI.
Hii ni kusema, Mazoea hujenga tabia, kisha tabia huleta ASILI. Hivyo ndivyo ilivyo. Hata hivyo hakuna kinachodumu, hata asili huzeeka na kupotea baada ya kukamilisha mzunguko wake.
Basi Siku zaenda wala hazirudu tena, tena zaja na kutuchukua na kutupeleka tusikokujua, tena hatutajua Kama tulikuwepo Kama sasa tusivyojua kuwa tulikuwapo.
Mazoea huumiza pale yanapotaka kuondolewa,tena. Tena yapo maumivu makali katika kuitoa tabia, mwisho ni kifo katika kuondoa asili ya kiumbe.
Mazoea ni mahusiano baina ya mtu mwenyewe, au mtu na mtu mwingine, au mtu na vitu, au mtu na Mazingira yanayomzunguka.
Yapo mazoea ya Mke na mume
Mazoea ya Mzazi na mtoto
Mazoea ya Mtu na Gari au Nyumba au vitu vyake
Mazoea ya Mtu na mahali anapoishi
Kutenganisha Mtu mwenye mazoea ni Jambo gumu linaloumiza Sana.
Hata hivyo Maumivu yatatokana na umri na ukomavu wa mazoea yenyewe.
Kadiri watu wanavyozoeana ndivyo ugumu wa kuwatenganisha unavyozidi kuimarika.
Ikiwa ilichukua siku kuzoea kitu basi itachukua Siku kukitenganisha na mtu huyo kukisahahu.
Ikiwa ilichukua Mwaka au miaka kuzoea kitu ndivyo itakavyo chukua mwaka au miaka kukitenganisha kitu na mtu huyo kukisahau.
Mazoea huishi moyoni na akilini.
Hujenga hisia za upendeleo na Kumbukumbu zilizojichimbia kulingana na urefu wa mzizi wa mazoea yenyewe.
Kumhamisha mtu mahali alipopazoea sio kwamba hataki au hapendi Bali kitakachomfanya apinge ni mazoea.
Sio kwamba wana ndoa au wapenzi hawataki kuachana, bali mazoea ndio huwaletea mushkeli.
Kimsingi, linapokuja suala la mahusiano ya ndoa, Taikon huwaga nashauri kuwa usiruhusu mwenza wako akawa na mazoea na watu wengine kiasi cha kupitiliza.
Pia ni ngumu kumchukua mke/mume WA mtu na kumfanya mwenza wako ikiwa alishazoeana Mume/mke wake. Hapo utawatenganisha kimwili tuu lakini mioyo Yao itakuwa pamoja, sio ajabu wakawa wanakutana bila ya wewe kujua.
Kizazi cha sasa kuna mambo madogo ambayo ni makubwa katika matokeo ambayo kinayapuuzia ndio maana kinalialia.
Hata mtu akifa, watu watalia Kwa sababu sio kwamba aliyekufa ni ndugu Yao au mzazi wake Bali kinacholiza mtu siku ya Msiba ni MAZOEA.
Ndio maana akifa mtu usiye na mazoea Naye, ukaribu Naye huwezi kusikia uchungu.
Au hata akifa Mama au Baba ambaye hajakulea wala haukuwa karibu Naye Huwezi kuhisi uchungu mkali ukilinganisha na Wale waliokuwa na mazoea Naye
Hakuna kitu kinauma Kama Kifo cha mtu wa karibu kabisa yaani mtu uliyemzoea.
Mazoea ni mwamba mgumu unaoujenga moyoni mwako, hivyo ni muhimu kujitahidi kutozoea mtu kupita kiasi Kupunguza makali na maumivu ya kutisha siku mtakapoachana.
Kwa maana Kuachana ni HAKIKA, Iwe Kwa Mauti au kufarakana.
Nipumzike sasa!
Nawatakia maandalizi Mema ya SABATO!
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa Sasa Dar es salaam
Anaandika Robert HERIEL
Yule Shahidi
Ingawaje maisha yanatufundisha tusiwe na MAZOEA kila siku, hayataki tuzoee lakini Sisi ndio tunalazimisha kuwa na MAZOEA, ndio maana leo ni tofauti na Jana, na kesho itakuwa mbali na siku ya leo. Wala hatujui nini kitajiri kesho, na hata hiki cha leo hatukujua Kama kingekuwa hivi. Ndivyo nilisema, maisha ni mzunguko wa mambo mapya yaliyozaliwa na mambo ya zamani, tena kesho ilitoka katika siku ya leo. Ijapokuwa kila siku yajitegemea na inajitosheleza, lakini kusudi ni moja katika muunganiko wa maisha.
Mazoea ni kufanya Jambo moja, lilelile kila mara, huitwa mazoea, desturi, kawaida na Amali. Kufanya kitu kila mara huzaa mazoea, kisha kikishakomaa na kinatengeneza TABIA, Tena tabia hukua na kukomaa na kurithishwa kutoka kizazi kimoja mpaka kizazi kingine, wakati mmoja mpaka wakati mwingine, Zama moja mpaka nyingine, na hapo huzaliwa mwamba mgumu uitwao ASILI.
Hii ni kusema, Mazoea hujenga tabia, kisha tabia huleta ASILI. Hivyo ndivyo ilivyo. Hata hivyo hakuna kinachodumu, hata asili huzeeka na kupotea baada ya kukamilisha mzunguko wake.
Basi Siku zaenda wala hazirudu tena, tena zaja na kutuchukua na kutupeleka tusikokujua, tena hatutajua Kama tulikuwepo Kama sasa tusivyojua kuwa tulikuwapo.
Mazoea huumiza pale yanapotaka kuondolewa,tena. Tena yapo maumivu makali katika kuitoa tabia, mwisho ni kifo katika kuondoa asili ya kiumbe.
Mazoea ni mahusiano baina ya mtu mwenyewe, au mtu na mtu mwingine, au mtu na vitu, au mtu na Mazingira yanayomzunguka.
Yapo mazoea ya Mke na mume
Mazoea ya Mzazi na mtoto
Mazoea ya Mtu na Gari au Nyumba au vitu vyake
Mazoea ya Mtu na mahali anapoishi
Kutenganisha Mtu mwenye mazoea ni Jambo gumu linaloumiza Sana.
Hata hivyo Maumivu yatatokana na umri na ukomavu wa mazoea yenyewe.
Kadiri watu wanavyozoeana ndivyo ugumu wa kuwatenganisha unavyozidi kuimarika.
Ikiwa ilichukua siku kuzoea kitu basi itachukua Siku kukitenganisha na mtu huyo kukisahahu.
Ikiwa ilichukua Mwaka au miaka kuzoea kitu ndivyo itakavyo chukua mwaka au miaka kukitenganisha kitu na mtu huyo kukisahau.
Mazoea huishi moyoni na akilini.
Hujenga hisia za upendeleo na Kumbukumbu zilizojichimbia kulingana na urefu wa mzizi wa mazoea yenyewe.
Kumhamisha mtu mahali alipopazoea sio kwamba hataki au hapendi Bali kitakachomfanya apinge ni mazoea.
Sio kwamba wana ndoa au wapenzi hawataki kuachana, bali mazoea ndio huwaletea mushkeli.
Kimsingi, linapokuja suala la mahusiano ya ndoa, Taikon huwaga nashauri kuwa usiruhusu mwenza wako akawa na mazoea na watu wengine kiasi cha kupitiliza.
Pia ni ngumu kumchukua mke/mume WA mtu na kumfanya mwenza wako ikiwa alishazoeana Mume/mke wake. Hapo utawatenganisha kimwili tuu lakini mioyo Yao itakuwa pamoja, sio ajabu wakawa wanakutana bila ya wewe kujua.
Kizazi cha sasa kuna mambo madogo ambayo ni makubwa katika matokeo ambayo kinayapuuzia ndio maana kinalialia.
Hata mtu akifa, watu watalia Kwa sababu sio kwamba aliyekufa ni ndugu Yao au mzazi wake Bali kinacholiza mtu siku ya Msiba ni MAZOEA.
Ndio maana akifa mtu usiye na mazoea Naye, ukaribu Naye huwezi kusikia uchungu.
Au hata akifa Mama au Baba ambaye hajakulea wala haukuwa karibu Naye Huwezi kuhisi uchungu mkali ukilinganisha na Wale waliokuwa na mazoea Naye
Hakuna kitu kinauma Kama Kifo cha mtu wa karibu kabisa yaani mtu uliyemzoea.
Mazoea ni mwamba mgumu unaoujenga moyoni mwako, hivyo ni muhimu kujitahidi kutozoea mtu kupita kiasi Kupunguza makali na maumivu ya kutisha siku mtakapoachana.
Kwa maana Kuachana ni HAKIKA, Iwe Kwa Mauti au kufarakana.
Nipumzike sasa!
Nawatakia maandalizi Mema ya SABATO!
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa Sasa Dar es salaam