Mazungumzo kati ya wajumbe wa Urusi na Ukraine kuendela tena leo, 03/03/2022

Mazungumzo kati ya wajumbe wa Urusi na Ukraine kuendela tena leo, 03/03/2022

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
1646314739465.png

Wajumbe wa Urusi na Wajumbe wa Ukraine wanatarajiwa kukutana leo kwa mazungumzo nchini Belarus ikiwa ni mara ya pili ya mazungumzo ya ana kwa ana tangu Urusi ilipoivamia Ukraine kijeshi siku nane zilizopita.

Ripoti zinasema kuwa Wawakilishi wa pande zote watakutana katika eneo la Brest nchini Belarus linalopakana na Poland.

Katika hotuba ya video kwa Taifa la Ukraine leo, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amewahimiza Waukraine kuendelea kupambana lakini hakutaja kama Warusi wamekamata miji yoyote.

Urusi leo imekiri kwa mara ya kwanza tangu kuanza kwa uvamizi huu kwamba karibu Wanajeshi 500 wa Urusi wameuawa katika mapigano na karibu 1,600 wamejeruhiwa huku Idara ya dharura ya Ukraine ikisema zaidi ya Raia 2,000 wameuawa.

Pia soma:Ukraine yakubali mazungumzo ya amani na Urusi, ni leo Jumatatu
 
Vita hii imetengenezwa tu!! tena maksudi ili kuwapima NATO nguvu zao sasa hao NATO Members hawana akili.. hawaioni israel ime kaa mbaliii! kimyaa! na hawa ndo Bankers hatare Dunianiii!.

Msisahau kitu kimoja vita ya Bankers, Financialer!! ndo hasa wanatafuta faida kwa Udi na uvumba......vita zote Ulaya zina faida kwa ma banker tangu miaka dahari!!..siyo kama sisi huku tunapigana tu kuonyesha umwamba!
 
Back
Top Bottom