Mazungumzo mafupi na kitukuu cha Abushiri bin Salim

Mazungumzo mafupi na kitukuu cha Abushiri bin Salim

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
MAZUNGUMZO MAFUPI NA KITUKUU CHA ABUSHIRI BIN SALIM AL HARITH

Leo jioni nimeingia katika duka moja.

Baada ya salaam kijana aliyekuwa pale dukani nyuma ya counter akanishukuru kwa kumwandika babu yake.

Mimi nikamuulia, ''Babu yako gani niliyemwandika?''

Kijana akanijibu, "Abushiri bin Salim.''

Nikashtuka nikamuuliza, ''Abushiri ni babu yako?''

"Naam ni babu yangu kwa upande wa kikeni kwangu bibi yangu Abushuri ni babu yake.''

Nikamuuliza kama hakuwa hafanyi maskhara.

Hapo huyu kijana akinitajia jina la mama yake na likaenda na kuishia kwa Abushiri.

Hapo nikatulia na yeye akawa katulia nikaanza kuuliza maswali ikiwa anajua historia ya huyu babu yake mkuu.

Alinijibu kuwa Abushiri katokea Zanzibar na alikuwa na wake wengi ambao wote walizaa watoto.

Tukaendelea na mazungumzo mimi nikitaka kujua kama kuna kumbukumbu yoyote katika familia yao kuhusu Abushiri.

Kijana akaniambia kuwa bibi yake kamfahamisha kuwa ardhi ambayo wanayo hivi sasa Zanzibar ni ya Abushiri.

Akaendelea kunifahamisha kuwa Abushiri babu yake mkuu alikuwa mtu tajiri sana Zanzibar na aliacha mashamba makubwa ambayo baada ya kuuliwa yalitaifishwa na Wajerumani ila ardhi kidogo iliyoachiwa familia.

Kijana akaniongezea akanambia kuwa kuna uvumi kuwa Abushiri alizika hazina kubwa katika ardhi yake na huko nyuma baada ya kifo chake kulikuwa na majaribio ya kutaka kuitafuta hazina hii lakini familia ilisimama kidete kupinga kuingiliwa faragha yao.

Ardhi hii imebaki katika familia hadi hivi sasa.

Screenshot_20210915-065125_WhatsApp.jpg
 
Huyo wa kwanza kushoto ni Makanda Bin Mwinyimkuu na wa kwanza kulia ni Jumbe Jahazi waliokua marafiki wakubwa wa Abushir Bin Salim

Makanda Bin Mwinyimkuu alikua ni miongoni mwa Waungwana wa mji wa Bagamoyo enzi za ustawi wake kibiashara na kiuchumi

Wajukuu wa Makanda wachache wangalipo katika miji ya Mbarara na Kasese nchini Uganda ambapo inasadikiwa ndipo mauti yalipomkuta. Aidha vitukuu, vilembwe na vinying'inya vya Makanda wapo wengi Tanzania, Congo ya DRC na Uganda

Jahazi alikua ni Jumbe Bagamoyo na miongoni mwa wajukuu zake ni pamoja na marehemu Dr Buyuni Jahazi aliyefariki miaka michache iliyopita

Mabwana wakubwa hawa walishirikiana na Abushiri katika vita na hujuma dhidi ya Wajerumani.

Makanda alikamatwa sambamba na Abushiri alikua anyongwe kama Abushiri lakini aliweza kuwatoroka askari waliokuwa wakimlinda na akatoweka asionekane mpaka alipoibukia Uganda ambapo alifanya makazi na kuacha familia na athari nzuri za kila aina

Watoto wa Makanda ni pamoja na Mwinyikondo, Mwinyiwengi(huyu alikua baba wa Abdurahman Wengi mchezaji wa Cosmo na refarii miaka ya 1980s) na Mwinyilau kuwataja wachache. Mwinyikondo alikua na mtoto akiitwa Rajab wakikaa Magomeni Mapipa mtaa wa Dosi namba 65 na alifariki mwaka 1980 aliwa na miaka 80

Historia ya Makanda Bin Mwinyimkuu ni ndefu na inahitaji uzi unaojitegemea kuilezea
 
Huyo wa kwanza kushoto ni Makanda Bin Mwinyimkuu na wa kwanza kulia ni Jumbe Jahazi waliokua marafiki wakubwa wa Abushir Bin Salim

Makanda Bin Mwinyimkuu alikua ni miongoni mwa Waungwana wa mji wa Bagamoyo enzi za ustawi wake kibiashara na kiuchumi

Wajukuu wa Makanda wachache wangalipo katika miji ya Mbarara na Kasese nchini Uganda ambapo inasadikiwa ndipo mauti yalipomkuta. Aidha vitukuu, vilembwe na vinying'inya vya Makanda wapo wengi Tanzania, Congo ya DRC na Uganda

Jahazi alikua ni Jumbe Bagamoyo na miongoni mwa wajukuu zake ni pamoja na marehemu Dr Buyuni Jahazi aliyefariki miaka michache iliyopita

Mabwana wakubwa hawa walishirikiana na Abushiri katika vita na hujuma dhidi ya Wajerumani.

Makanda alikamatwa sambamba na Abushiri alikua anyongwe kama Abushiri lakini aliweza kuwatoroka askari waliokuwa wakimlinda na akatoweka asionekane mpaka alipoibukia Uganda ambapo alifanya makazi na kuacha familia na athari nzuri za kila aina

Watoto wa Makanda ni pamoja na Mwinyikondo, Mwinyiwengi(huyu alikua baba wa Abdurahman Wengi mchezaji wa Cosmo na refarii miaka ya 1980s) na Mwinyilau kuwataja wachache. Mwinyikondo alikua na mtoto akiitwa Rajab wakikaa Magomeni Mapipa mtaa wa Dosi namba 65 na alifariki mwaka 1980 aliwa na miaka 80

Historia ya Makanda Bin Mwinyimkuu ni ndefu na inahitaji uzi unaojitegemea kuilezea
Sesten...
Sasa umenitia darasani.

Dr. Jahazi mimi alikuwa kaka yangu na ni mtu tukizungumza sana.

Nimepata pia kukutana na kaka yake yeye anaishi Mombasa.

Mwaka wa 1993 tena mwezi wa Ramadhani tulipanda ndege moja na tukakaa pamoja kwenda Harare.

Alinihadithia historia ya Prince Badru Kakunguru wa Uganda kwa urefu.

Sasa nimeelewa.
 
Sesten...
Sasa umenitia darasani.

Dr. Jahazi mimi alikuwa kaka yangu na ni mtu tukizungumza sana.

Nimepata pia kukutana na kaka yake yeye anaishi Mombasa.

Mwaka wa 1993 tena mwezi wa Ramadhani tulipanda ndege moja na tukakaa pamoja kwenda Harare.

Alinihadithia historia ya Prince Badru Kakunguru wa Uganda kwa urefu.

Sasa nimeelewa.
 
Taazia nzuri sana iliyoelezea baadhi ya sifa za al marhum Dr Jahazi. Hakika alikua ni mtu wa akhlak(tabia na mwenendo mwema sana). Na kwa hakika Uslamu ni akhlak

Muft Badru Kakunguru ni hadithi njema nyingine katika watu walioendeleza sana Uislamu Uganda. Allah Awaraham wazee wetu hawa
 
Sesten...
Sasa umenitia darasani.

Dr. Jahazi mimi alikuwa kaka yangu na ni mtu tukizungumza sana.

Nimepata pia kukutana na kaka yake yeye anaishi Mombasa.

Mwaka wa 1993 tena mwezi wa Ramadhani tulipanda ndege moja na tukakaa pamoja kwenda Harare.

Alinihadithia historia ya Prince Badru Kakunguru wa Uganda kwa urefu.

Sasa nimeelewa.

Naam, sheikh Badru Kakunguru
 
Taazia nzuri sana iliyoelezea baadhi ya sifa za al marhum Dr Jahazi. Hakika alikua ni mtu wa akhlak(tabia na mwenendo mwema sana). Na kwa hakika Uslamu ni akhlak

Muft Badru Kakunguru ni hadithi njema nyingine katika watu walioendeleza sana Uislamu Uganda. Allah Awaraham wazee wetu hawa
Sesten...
Amin.

Mwaka wa 2003 nilihudhuria mkutano Kampala na mmoja katika watu maarufu alikuwa Prof. Ali Mazrui.

Mjukuu wa Badru Kakungulu alikuwapo katika mkutano huu na alitualika chakula cha usiku nyumbani kwake.

Prof. Mazrui ndiye aliyetoa neno la shukurani na alieleza historia ya ukoo huu na vipi umehusiana na Kabaka wa Uganda.
 
Huyo wa kwanza kushoto ni Makanda Bin Mwinyimkuu na wa kwanza kulia ni Jumbe Jahazi waliokua marafiki wakubwa wa Abushir Bin Salim

Makanda Bin Mwinyimkuu alikua ni miongoni mwa Waungwana wa mji wa Bagamoyo enzi za ustawi wake kibiashara na kiuchumi

Wajukuu wa Makanda wachache wangalipo katika miji ya Mbarara na Kasese nchini Uganda ambapo inasadikiwa ndipo mauti yalipomkuta. Aidha vitukuu, vilembwe na vinying'inya vya Makanda wapo wengi Tanzania, Congo ya DRC na Uganda

Jahazi alikua ni Jumbe Bagamoyo na miongoni mwa wajukuu zake ni pamoja na marehemu Dr Buyuni Jahazi aliyefariki miaka michache iliyopita

Mabwana wakubwa hawa walishirikiana na Abushiri katika vita na hujuma dhidi ya Wajerumani.

Makanda alikamatwa sambamba na Abushiri alikua anyongwe kama Abushiri lakini aliweza kuwatoroka askari waliokuwa wakimlinda na akatoweka asionekane mpaka alipoibukia Uganda ambapo alifanya makazi na kuacha familia na athari nzuri za kila aina

Watoto wa Makanda ni pamoja na Mwinyikondo, Mwinyiwengi(huyu alikua baba wa Abdurahman Wengi mchezaji wa Cosmo na refarii miaka ya 1980s) na Mwinyilau kuwataja wachache. Mwinyikondo alikua na mtoto akiitwa Rajab wakikaa Magomeni Mapipa mtaa wa Dosi namba 65 na alifariki mwaka 1980 aliwa na miaka 80

Historia ya Makanda Bin Mwinyimkuu ni ndefu na inahitaji uzi unaojitegemea kuilezea
Kwenye hili kabrasha hawa askari wamemsimulia vizuri sana Bwana Bushiri
 
MAZUNGUMZO MAFUPI NA KITUKUU CHA ABUSHIRI BIN SALIM AL HARITH

Leo jioni nimeingia katika duka moja.

Baada ya salaam kijana aliyekuwa pale dukani nyuma ya counter akanishukuru kwa kumwandika babu yake.

Mimi nikamuulia, ''Babu yako gani niliyemwandika?''

Kijana akanijibu, "Abushiri bin Salim.''

Nikashtuka nikamuuliza, ''Abushiri ni babu yako?''

"Naam ni babu yangu kwa upande wa kikeni kwangu bibi yangu Abushuri ni babu yake.''

Nikamuuliza kama hakuwa hafanyi maskhara.

Hapo huyu kijana akinitajia jina la mama yake na likaenda na kuishia kwa Abushiri.

Hapo nikatulia na yeye akawa katulia nikaanza kuuliza maswali ikiwa anajua historia ya huyu babu yake mkuu.

Alinijibu kuwa Abushiri katokea Zanzibar na alikuwa na wake wengi ambao wote walizaa watoto.

Tukaendelea na mazungumzo mimi nikitaka kujua kama kuna kumbukumbu yoyote katika familia yao kuhusu Abushiri.

Kijana akaniambia kuwa bibi yake kamfahamisha kuwa ardhi ambayo wanayo hivi sasa Zanzibar ni ya Abushiri.

Akaendelea kunifahamisha kuwa Abushiri babu yake mkuu alikuwa mtu tajiri sana Zanzibar na aliacha mashamba makubwa ambayo baada ya kuuliwa yalitaifishwa na Wajerumani ila ardhi kidogo iliyoachiwa familia.

Kijana akaniongezea akanambia kuwa kuna uvumi kuwa Abushiri alizika hazina kubwa katika ardhi yake na huko nyuma baada ya kifo chake kulikuwa na majaribio ya kutaka kuitafuta hazina hii lakini familia ilisimama kidete kupinga kuingiliwa faragha yao.

Ardhi hii imebaki katika familia hadi hivi sasa.

View attachment 1938162
Hapa twaweza jifunza ni nini kilichojiri Bagamoyo na Pangani
 

Attachments

Back
Top Bottom