Mbaroni kwa kuwafanyia wanafunzi mitihani

Mbaroni kwa kuwafanyia wanafunzi mitihani

Msongoru

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2008
Posts
306
Reaction score
24
na Shangwe Thani, Shinyanga



JESHI la Polisi mkoani Shinyanga, linawashikilia walimu wawili wa shule za msingi kwa tuhuma za kuwafanyia mtihani wa taifa wa kumaliza elimu ya msingi wanafunzi watano kinyume cha sheria na taratibu za mitihani.

Kamanda wa Polisi mkoani Shinyanga, Shaibu Ibrahim, alisema ofisini kwake jana kuwa tukio hilo lilitokea Septemba 11 wakati wanafunzi wa shule za msingi nchini wakifanya mtihani wa taifa wa darasa la saba.

Aliwataja walimu wanaoshikiliwa na polisi kuwa Bengwe Hiellele (44), mwalimu wa Shule ya Msingi ya Ibango, iliyopo katika Kijiji cha Salawe Wilaya ya Shinyanga Vijijini na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi ya Itobanilo, John Madirisha.

Mwalimu Hielele, aliyekuwa msimamizi wa mtihani katika shule hiyo kwa kushirikiana na mwalimu Madirisha ambaye ni mwalimu mkuu wa Shule ya Itobanilo, wanadaiwa kuwafanyia mtihani wanafunzi watano, kinyume cha sheria na taratibu za mitihani.

Kamanda Ibrahim, aliwataja wanafunzi waliofanyiwa mitihani kuwa ni Shangaluka Msala, Frank Jumanne, Maganga Magadya, John Jumanne na Saidi Cosmas na kwamba uchunguzi wa awali wa polisi umebaini kuwa wanafunzi hao walitoa shilingi 20,000 kila mmoja ili wasaidiwe kufanyiwa mtihani na walimu hao.

Alibainisha kuwa kabla ya kukamatwa kwao walimu hao walikuwa wamewafanyia mitihani ya hisabati, Kiswahili, Sayansi na Kiingereza na mwalimu Hielele, alipopekuliwa mfukoni alikutwa akiwa na karatasi ya maswali ya somo la hisabati ambao ulifanyika Septemba 10 mwaka huu.
 
na Shangwe Thani, Shinyanga



JESHI la Polisi mkoani Shinyanga, linawashikilia walimu wawili wa shule za msingi kwa tuhuma za kuwafanyia mtihani wa taifa wa kumaliza elimu ya msingi wanafunzi watano kinyume cha sheria na taratibu za mitihani.

Kamanda wa Polisi mkoani Shinyanga, Shaibu Ibrahim, alisema ofisini kwake jana kuwa tukio hilo lilitokea Septemba 11 wakati wanafunzi wa shule za msingi nchini wakifanya mtihani wa taifa wa darasa la saba.

Aliwataja walimu wanaoshikiliwa na polisi kuwa Bengwe Hiellele (44), mwalimu wa Shule ya Msingi ya Ibango, iliyopo katika Kijiji cha Salawe Wilaya ya Shinyanga Vijijini na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi ya Itobanilo, John Madirisha.

Mwalimu Hielele, aliyekuwa msimamizi wa mtihani katika shule hiyo kwa kushirikiana na mwalimu Madirisha ambaye ni mwalimu mkuu wa Shule ya Itobanilo, wanadaiwa kuwafanyia mtihani wanafunzi watano, kinyume cha sheria na taratibu za mitihani.

Kamanda Ibrahim, aliwataja wanafunzi waliofanyiwa mitihani kuwa ni Shangaluka Msala, Frank Jumanne, Maganga Magadya, John Jumanne na Saidi Cosmas na kwamba uchunguzi wa awali wa polisi umebaini kuwa wanafunzi hao walitoa shilingi 20,000 kila mmoja ili wasaidiwe kufanyiwa mtihani na walimu hao.

Alibainisha kuwa kabla ya kukamatwa kwao walimu hao walikuwa wamewafanyia mitihani ya hisabati, Kiswahili, Sayansi na Kiingereza na mwalimu Hielele, alipopekuliwa mfukoni alikutwa akiwa na karatasi ya maswali ya somo la hisabati ambao ulifanyika Septemba 10 mwaka huu.


Hayo ndo ya Shinyanga!!!! Chuo cha Ustawi wa jammi jamaa la Mzumbe University lilikuja kumfanyia girlfriend wake mtihani!!!! Hii ni habari nyepesinyepesi ya wiki iliyopita. Jamani maksi za kwenye vyeti somteimes si lolote, ndiyo maana mtu anaomba kazi cheti flying colours. Then mpe practical duties. deliverables ni zero au tuseme hasi kabisa then unashangaa mbona cheti kapasua sana??? Hizi ni sawa na maksi za chupi.

Yale yale ya BOT wafanyakazi watano vyeti ni fake??? Sasa je wao walifanyiwa mtihani au ni vyeti vilichongwa mitaani?? Usanii mwingi Tanzania.
 
Hiyo habari hapo juu ni kielelezo kidogo cha hali halisi (Rushwa, Ufukara uliokubuhu, Udhalimu/oppression.... the list goes on). Natabiri kwamba JK atakuwa raisi wa kwanza wa TZ kushitakiwa.


Ujumbe mzito kwenye katuni.





.
 
Ni njaa tu za walimu wetu....20,000 umfanyie mwanafunzi mtihani. Nadhani sirikali ya JK iwe makini katika kupanga viwango vya mishahara vya watumishi wake.

Yawezekana na ufisadi unaondelea unawapa machungu walimu kuona viongozi wanafisadi kila siku na wao wameona bora wafisadi katika maeneo yao...Nchi haina mwenyewe sasa....
 
Ni njaa tu za walimu wetu....20,000 umfanyie mwanafunzi mtihani. Nadhani sirikali ya JK iwe makini katika kupanga viwango vya mishahara vya watumishi wake.

Yawezekana na ufisadi unaondelea unawapa machungu walimu kuona viongozi wanafisadi kila siku na wao wameona bora wafisadi katika maeneo yao...Nchi haina mwenyewe sasa....

Lakini pia sisi wengine kusoma hatutaki!! Ni wavivu mno.
 
Back
Top Bottom