Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,267
Muda huu wa saa 6.20 mchana, watu wanazidi kumiminika uwanjani huku foleni za kukata tiketi zikiongezeka kama inavyoonekana hapa.
Kumbuka mechi hii itakuwa mubashara kupitia Azam Sports 2 na kwa upande wa radio TBC Taifa inakutangazia kuanzia saa 10. 00 jioni.
Vikosi vyote viwili tukianza na wenyeji wa mchezo huu, Mbeya City:
Upande wa wageni wa mchezo huu, Simba Sports Club:
=======
Timu ndo zinaingia uwanjani kuashiria kuanza kwa mpambano
==> 0' Mpira umeanza: Mbeya City 0-0 Simba Sports Club
==> Goooooaaal dakika ya 8' Shiza Kichuya anaipatia Simba SC goli la kwanza, Mbeya City 0-1 Simba SC
==> 15' Mbeya City 0-1 Simba SC
==> 30' Mbeya City 0-1 Simba SC
45 ' za kipindi cha kwanza za mchezo wa mpira zimekwisha ambapo matokeo ni Mbeya City 0-1 Simba Sports Club.
Half time;
45' za kwanza kipindi cha pili za mtanange huu zinaanza
==> 65' matokeo bado Mbeya City 0-1 Simba Sports Club
==> 80' Mbeya City 0-1 Simba Sports Club
90+3' Mpira umekwisha kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya City ikiwa nyumbani imefungwa goli moja bila majibu, goli likifungwa na winga Shiza Kichuya akipokea pasi safi kutoka Jonas Mkude.
Kwa matokeo hayo Simba SC imerejea kileleni mwa msimamo wa ligi kuu Tanzania bara (VPL), kwa alama 19 huku Ruvu Shooting ikisalia mkiani na alama zake 5.