MBEYA: Je, TANESCO na REA mmeishiwa nguzo mpaka mnafunga nyaya za kusambazia umeme kama kamba za kuanikia nguo?

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Hapa ni kitongoji cha Hasengo, kijiji cha Shibolya wilaya ya Mbeya vijijini mkoani Mbeya, Ni jambo jema na tunashukuru huduma ya umeme imetufikia kupitia wakala wa kusambaza umeme vijijini REA, baada ya kutokuwepo kwa huduma hiyo muhimu tangu kupata uhuru wa nchi hii.

Bila shaka usambazaji wa huduma hii kwa wananchi unapaswa pia kuzingatia usalama wa watu kutokana na hatari kubwa ya umeme. Kilichofanyika hapa kwetu ni kuhatarisha maisha ya watu hasa watoto wadogo. Ufungaji wa namna hii wa nyaya za umeme kama kamba za kuanikia nguo ni hatari sanaa,

Na bado hapo katikati waya unabembea karibu mtu yeyote anayepita hapo anaweza kuufikia na kushika na watoto pia hucheza karibu na hapo, hii ni hatari zaidi

Nyaya zinatepeta ni kwamba TANESCO & REA mmeishiwa nguzo mpaka mnafunga nyaya za umeme kama kamba za kuanikia nguo?


TANESCO pamoja na REA mfanyie kazi changamoto hii ili kuweka maisha ya watu salama kwa kuondoa hatari hii
 

Attachments

  • 20241226_165722.jpg
    1.2 MB · Views: 4
Hii Ni hatari ,huku Kuna special thread ya Tanesco mkuu,forward huko hii thread,sijui tuu ku forward ningefanya hivyo
 
Angalia vizuri, kuna nyaya nyingi tu mijini sio za Tanesco kuna cable tv na mitanado ya simu.
 
Hapana ni Mbeya Vijijini kuna mbunge mmoja asiyewaza wananchi wake anaitwa Orani Njenza
Wabunge wote wa mkoa wa mbeya ni hewa!
Kuna wacjimbo la Lupa na mwingine Jimbo la Chunya! Tumepanga 2025 ,ubunge watausikia radioni
 
Stuxnet Jimbo la Mbunge wako Njenza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…