Mbeya: Mkandarasi atimuliwa, "anajinasibu ana cheo kikubwa kamati ya CCM mkoa"

Mbeya: Mkandarasi atimuliwa, "anajinasibu ana cheo kikubwa kamati ya CCM mkoa"

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera ameelekeza uongozi wa jiji la Mbeya, kusitisha mkataba wa mkandarasi anayejenga vyumba vitatu vya madarasa na vyoo, katika shule ya msingi mafanikio kata ya Itezi jijini Mbeya kwa kushindwa kukamilisha madarasa hayo kwa wakati.

Madarasa hayo yanayojengwa kwa fedha kutoka serikali kuu kiasi cha shilingi millioni 88, fedha zilizo tolewa mwezi wa sita mwaka 2024, lakini ujenzi wake umekua ukisuasua hadi sasa ukiwa bado haujakamilika, huku mkandarasi akiwatishia wananchi wa eneo hilo kua ni mjumbe wa kamati ya nidhamu wa chama cha mapinduzi CCM, ili kuwazuia kumfuatilia kwa ukaribu.

Nao baadhi ya mafundi waliotumiwa na mkandarasi kutekeleza mradi huo wameeleza namna mkandarasi huyo alivyofanya dhuluma kwao kwa kuwapa kazi bila malipo ambayo wanadai hadi sasa, huku mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya Mhe. DorMohamed Issa akieleza maamuzi yaliyofikiwa na uongozi wa jiji hilo.

 
Tatizo ni ngumu kuamini kama kweli RC yupo pamoja na wananchi,kwani nilikua mratibu wa mradi huko nyuma katika Mkoa wa Simiyu na RC alikua bwana yule wa barabara za kulipia,nilipitia kigumu sana,kwani alinisumbua sana kuhusu mradi huo na mpaka nikafikia hatua ya kuacha kazi,ila PM akanitia moyo na kuniambia kua,Mr ndibuka piga kazi huu mradi,masharti ni kutowapa mamlaka serikalini,hivyo piga kazi... Hebu RC atuambie kama masrahi na hii kampuni?
 
Wazee bado tunasafari ndefu sana, yaani vyumba vitatu vya madarasa tunakusanyana kiasi hiki mpaka mkuu wa mkoa?..

Hiyo si ni amri tu kutoka kwa mkurugenzi wa halmashauri anayedeal na huyo mkandarasi, 2xmonth tunakupa umalize, Ukishindwa tunakunyang'anya kazi na kufidia gharama zetu na kazi anapewa mwingine na wewe tunafuta leseni ya ukandarasi na tin number kule TRA usifanye kabisa biashara kwa kipengele cha kukosa uaminifu.
 
Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera ameelekeza uongozi wa jiji la Mbeya, kusitisha mkataba wa mkandarasi anayejenga vyumba vitatu vya madarasa na vyoo, katika shule ya msingi mafanikio kata ya Itezi jijini Mbeya kwa kushindwa kukamilisha madarasa hayo kwa wakati.

Madarasa hayo yanayojengwa kwa fedha kutoka serikali kuu kiasi cha shilingi millioni 88, fedha zilizo tolewa mwezi wa sita mwaka 2024, lakini ujenzi wake umekua ukisuasua hadi sasa ukiwa bado haujakamilika, huku mkandarasi akiwatishia wananchi wa eneo hilo kua ni mjumbe wa kamati ya nidhamu wa chama cha mapinduzi CCM, ili kuwazuia kumfuatilia kwa ukaribu.

Nao baadhi ya mafundi waliotumiwa na mkandarasi kutekeleza mradi huo wameeleza namna mkandarasi huyo alivyofanya dhuluma kwao kwa kuwapa kazi bila malipo ambayo wanadai hadi sasa, huku mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya Mhe. DorMohamed Issa akieleza maamuzi yaliyofikiwa na uongozi wa jiji hilo.

Ccm wote wako hivi hivi
 
Wazee bado tunasafari ndefu sana, yaani vyumba vitatu vya madarasa tunakusanyana kiasi hiki mpaka mkuu wa mkoa?..

Hiyo si ni amri tu kutoka kwa mkurugenzi wa halmashauri anayedeal na huyo mkandarasi, 2xmonth tunakupa umalize, Ukishindwa tunakunyang'anya kazi na kufidia gharama zetu na kazi anapewa mwingine na wewe tunafuta leseni ya ukandarasi na tin number kule TRA usifanye kabisa biashara kwa kipengele cha kukosa uaminifu.
Kazi ya kufanywa na Mwenyekiti wa kijiji anayejielewa lakini hapo utashangaa mpaka Waziri Mkuu anaenda
 
Vyumba vitatu vya madarasa navyo vinajengwa na mkandarasi

Hivyo si unatafuta fundi Michael tu anakujengea fresh kabisa
Huyu ameshinda kwenye Mfumo wa NEST ambapo unajisajili. Kila fundi mwenye sifa ana haki ya kujisajili. Na baada ya hapo, sifa kubwa ya kupata kandarasi ni kuwa na bei ndogo ya gharama za ujenzi.
 
Huyu ameshinda kwenye Mfumo wa NEST ambapo unajisajili. Kila fundi mwenye sifa ana haki ya kujisajili. Na baada ya hapo, sifa kubwa ya kupata kandarasi ni kuwa na bei ndogo ya gharama za ujenzi.
Wanaangalia Bei Ndogo Na Si Ubora Wa Kazi,,mazafaka....!!!
 
Wanaangalia Bei Ndogo Na Si Ubora Wa Kazi,,mazafaka....!!!
Sio kweli. Ukiishachaguliwa na mfumo wa NEST unatakiwa uzingatie Bili of Quantity (BoQ) na ramani. Kujenga chini ya kiwango ni uzembe wa Mwandishi Msimamizi.
 
Sio kweli. Ukiishachaguliwa na mfumo wa NEST unatakiwa uzingatie Bili of Quantity (BoQ) na ramani. Kujenga chini ya kiwango ni uzembe wa Mwandishi Msimamizi.
Sio Kweli Wakati Umeandika Wewe Kwenye Hoja Yako Namba 9,,,"Nukuu"Sifa Kubwa Ni Kuwa Na Bei Ndogo Ya Ujenzi Ili Uweze Pata Kandarasi"
 
Back
Top Bottom