DOKEZO Mbeya: Mwalimu Mkuu Shule ya Sekondari Mabatini analazimisha wanafunzi wenye ufaulu mdogo kurudia darasa, wakigoma anawafukuza

DOKEZO Mbeya: Mwalimu Mkuu Shule ya Sekondari Mabatini analazimisha wanafunzi wenye ufaulu mdogo kurudia darasa, wakigoma anawafukuza

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

CHUMA78

New Member
Joined
Feb 11, 2025
Posts
3
Reaction score
0
Habari wanajukwaa!

Je, kuna utaratibu wowote kwa shule ya Sekondari kuamuru kumfukuza shule mtoto mwenye ufaulu hafifu?

Nimekutana na hii scenario katika shule moja ya Sekondari iliyopo mtaa wa Mabatini, Kata ya Mabatini, Wilaya ya Mbeya Jiji, Mkoa wa Mbeya. Hii shule inaitwa Mabatini Secondary School, wiki hii mwalimu mkuu wa shule ameita wazazi shuleni kwa ajili ya kutoa taarifa.

Taarifa iliyotolewa ni kwamba kwa baadhi ya wanafunzi ambao wana ufaulu hafifu hasa hawa wa kidato cha pili ambao mwaka jana walikuwa kidato cha kwanza wanatakiwa kurudia darasa na kama ikitokea wamegoma waachane na shule na kujiunga na mafunzo ya Ufundi ambayo yametolewa na Serikali hivi karibuni.

Naulizia kupata muongozo, je, hii inakubalika?

=========================
Mkurugenzi wa Jiji: Wazazi wenye malalamiko wafike ofisini kwangu

Akielezea kuhusu suala hilo, Mkurugenzi wa Mbeya Jiji, John John Nchimbi amezungumza na JamiiForums na kusema:

“Suala hilo halijafika kwangu lakini nimekuwa mara zote nikiwashauri Wazazi au Walezi wenye malalamika au wanahisi wameonewa wasiishie kuandika Mtandaoni, waje ofisini kwangu tuzungumze.

“Mtoto hawezi na haitakiwi kurudishwa darasa bila mzazi kujua au kwa lazima, ikitokea kuwa hakuwepo darasani muda mrefu hapo anaweza kurudishwa lakini kwa Mzazi kupewa taarifa ya maandishi.

“Nawakaribisha wote wenye changamoto, wiki hii nipo ofisini, waje kuanzia saa mbili asubuhi watanikuta, nipo kwa ajili yao."

=========================​

Afisa Elimu Mkoa wa Mbeya, Mwalimu Kiduma Mageni alipozungumza na JamiiForums amesema:

"Kama Mwalimu anafanya hivyo anakosea na nikinyume cha utaratibu, Mwanafunzi kurudia inatakiwa ridhaa ya Mzazi na baada ya mazungumzo inatakiwa athibitishe kwa maandishi, pia mimi ndio ninayepitisha huo uamuzi wa Mwanafunzi kurudia darasa, hivyo suala hilo nitalifuatilia kwa ukaribu."
 
Shule zinaruhusiwa kuwa na pass mark zake, mfano mimi shule niliyosoma O level ukipata wastani C unarudi nyumbani kutafuta shule nyingine.
 
Habari wanajukwaa!

Je, kuna utaratibu wowote kwa shule ya Sekondari kuamuru kumfukuza shule mtoto mwenye ufaulu hafifu?

Nimekutana na hii scenario katika shule moja ya Sekondari iliyopo mtaa wa Mabatini, kata ya Mabatini, Wilaya ya Mbeya Jiji, Mkoa wa Mbeya. Hii shule inaitwa Mabasimi Secondary School, wiki hii mwalimu mkuu wa shule ameita wazazi shuleni kwa ajili ya kutoa taarifa.

Taarifa iliyotolewa ni kwamba kwa baadhi ya wanafunzi ambao wana ufaulu hafifu hasa hawa wa kidato cha pili ambao mwaka jana walikuwa kidato cha kwanza wanatakiwa kurudia darasa na kama ikitokea wamegoma waachane na shule na kujiunga na mafunzo ya Ufundi ambayo yametolewa na Serikali hivi karibuni.

Naulizia kupata muongozo, je, hii inakubalika?
Tena MSHUKURU MUNGU huyo mwalimu anaona mbali we unawezaje kwenda mbele topic za nyuma hujacover au na ww zwa zwa
 
Kama mtoto ana uwezo mdogo darasani, ni vizuri akatafutiwa shughuli nyingine ya kufanya! Badala ya kumlazimisha kukariri masomo ambayo hayana faida yoyote ile kwenye maisha yake.

Au unafikiri mtu kama Mbwana Samatta angelazimishwa kusoma, mpaka leo angekuwepo huko aliko?

Mkuu wa shule, wewe timua tu hao watoto ili wakitoka hapo shule wakavumbue vipaji vyao halisi vya biashara, ufundi, usanii, uanamichezo, nk. Badala ya kukusumbua tu na kukuongezea masifuri kwenye matokeo ya kidato cha pili na nne kwenye hiyo shule yako.
 
shule ya serikali?
Tena zipo nyingi tu mdau. Kwenye hizi shule za serikali kuna matabaka mengi, yenye nguvu
Kwa mfano, shule cream za serikali zinachuana vigezo na masharti na akina St . Francis.
Huyo HM anecheza vyema kadiri ya matakwa ya mtaala mpya
 
Habari wanajukwaa!

Je, kuna utaratibu wowote kwa shule ya Sekondari kuamuru kumfukuza shule mtoto mwenye ufaulu hafifu?

Nimekutana na hii scenario katika shule moja ya Sekondari iliyopo mtaa wa Mabatini, kata ya Mabatini, Wilaya ya Mbeya Jiji, Mkoa wa Mbeya. Hii shule inaitwa Mabasimi Secondary School, wiki hii mwalimu mkuu wa shule ameita wazazi shuleni kwa ajili ya kutoa taarifa.

Taarifa iliyotolewa ni kwamba kwa baadhi ya wanafunzi ambao wana ufaulu hafifu hasa hawa wa kidato cha pili ambao mwaka jana walikuwa kidato cha kwanza wanatakiwa kurudia darasa na kama ikitokea wamegoma waachane na shule na kujiunga na mafunzo ya Ufundi ambayo yametolewa na Serikali hivi karibuni.

Naulizia kupata muongozo, je, hii inakubalika?
Acha kutetea ujinga.

Huyo mwalimu yupo sahihi sana .

Mwanafunzi mzembe ,dawa yake kumkaririsha darasa .
 
Back
Top Bottom