Mbeya: NHIF Yabaini ubadhirifu, wahusika watoweka kusikojulikana

Mbeya: NHIF Yabaini ubadhirifu, wahusika watoweka kusikojulikana

Lady Whistledown

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2021
Posts
1,147
Reaction score
2,008
Naibu Waziri wa Afya, Dkt, Godwin Mollel amesema wamebaini kuwa Polyclinic moja imetoweka na Tsh. Millioni 137 za NHIF ambayo waliibaini kutoa huduma kwenye nyumba ya wageni na walipoifuatilia ili kuwakamata wahusika walitoweka kusikojulikana hadi hii leo.

Pia akiwa katika kikao cha Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii hivi karibuni jijini Dar es Salaam, Dk Mollel alisema, wataalamu walioagizwa kufanya uchunguzi wamebaini ubadhilifu wa Tsh. Bilioni 1.6 za NHIF Mbeya mjini pekee.

Hii ni baada ya Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu kuipa NHIF siku 14 za kumpelekea mikakati ya kudhibiti udanganyifu unaofanywa kwa kutumia mifumo ya TEHAMA na wateja wake.

Chanzo: Mwananchi
 
Ilo ni shamba la bibi ni zote zinanuka yaan ni ofisi zote zinanuka wizi
 
Duh hapo wanufaika wakisikia hivi wanatamani kutoendelea changia michango
 
Shamba la bibi unavuna kutokana na ukubwa wa sandarusi lako
Na hasa Sasa hivi ni kama vile mafisi yenye njaa yametoboa shimo upande wa pili baada ya mlango wa shimo kuziba kwa cement kali. Wamekalia cheap politics za kupanda boat toka znz hadi Dar. Eti ni uzalendo huku mabilion yakipigwa kila kona Sasa hivi Tz.
 
Huwezi kulipa bila kujua unamlipa nani, wamepiga kolabo...
 
Wangelifumua shirika upya, na kufanya verification ya vendors wote upya. Ila pia kuwe na utaritibu wa kuconfirm na mnufaika kudhibitisha huduma alizopata.
 
Waziri ummy juzi akawa analalamika ooh mfuko unataka kufa kumbe wameshindwa kuudhibiti tu ni kwamba wameshindwa kuziba mianya kwa sababu haiwezekani mfuko unachangiwa na watu labda 1000 kila mwezi na wanaougua na kutumia hela hawafiki hata nusu ya hao labda wataugua 200 tu hao wengine 800 hela zao huwa zinaenda wapi? management tu mbovu period na ulafi uliopitiliza
 
Ila tuache utani aisee NHIF wanapigwa sana hasa kwenye hizi hospital kubwa na polyclinic, yaani watu wanakaa wanatengeneza claims fake na wanalipwa vizuri tu.
 
Mbona hiyo kliniki inajulikana na inafanya kazi sema mkitaka connection mnipe nusu ya hiyo hela kwanza.
 
Upumbavu mtupu!!

1. Yaani NW Dr. Mollel anashindwa kututajia Jina na hiyo Polyclinic?
2. Ofisi yake ina register ya health facility zote nchi hii na wamiliki wake... Kwanini hawa'disclose details zao tuwajue?
3. Tangu lini NHIF ikalipa reimbursement kwa facility inayotolea huduma kwenye nyumba za wageni?

Endeleeni na ujinga wenu.
 
Back
Top Bottom