DOKEZO Mbeya Vijijini kata ya Iwiji umeme unakatika mara kwa mara, mafundi wakija kutengeneza wanadai malipo kutoka kwa wananchi

DOKEZO Mbeya Vijijini kata ya Iwiji umeme unakatika mara kwa mara, mafundi wakija kutengeneza wanadai malipo kutoka kwa wananchi

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Mkoa wa Mbeya, wilaya ya Mbeya Vijijini, kata ya Iwiji baadhi ya vitongoji tuna tuna umeme wa REA, ambao umekuwa kero kubwa kwetu kwani hukatika mara kwa mara.

Muda mwingine hata ndani ya dakika 5 unaweza kata na kurudi mara mbili, bila kuambiwa chanzo ni nini.

Pia inapotokea kuna shida, vituo vya msaada ni mbali sana mpaka mjini kupata huduma ya TANESCO, na mara nyingine huwa wakipigiwa makao makuu wanawapa maelekezo mafundi watengeneze, baada ya hapo hao mafundi huanza kudai hela ya mafuta ya pikipiki, kutoka kata jirani ya Ilembo , hata kama tatizo linahusu kwenye trasnformer. Mfano ni baada ya transfomer kuharibika kitongoji cha Magole ilikaa siku 5 bila kutengenezwa ili hali wameambiwa.

Kero kubwa ni raia kuogopa kuwapigia kwani wanaogopa kutoa nauli ya mafundi.
 
Back
Top Bottom