Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 1,906
- 5,000
Wakuu,
Wameona wamtengee kabisa Tulia jimbo asipate tabu ya kusumbuana na Sugu, maana wanajua ataibika!
====
Halmashauri ya Jiji la Mbeya imependekeza kuanza mchakato wa kuchunguza na kuligawa Jimbo la Mbeya Mjini kupata jimbo jipya la Uyole, katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 25, 2025.
Jimbo hilo kwa sasa linaongozwa na Dk Tulia Ackson ambaye pia ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Muungano wa Mabunge Duniani (IPU).
Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Mchakato huo ukikamilika na kukidhi vigezo, Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) italitangaza jimbo jipya, jambo ambalo litakuwa jawabu la matakwa ya wakazi wa Mbeya Mjini.
Akizungumza niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa jiji hilo, John Nchimbi leo Machi 11, 2025 katika kikao maalumu cha Baraza la Madiwani, Mkuu wa Idara ya Utumishi na Utawala jijini humo, Nicodemus Tindwa amesema hatua hiyo ni baada ya kupokea barua kutoka Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.
Mwananchi
Wameona wamtengee kabisa Tulia jimbo asipate tabu ya kusumbuana na Sugu, maana wanajua ataibika!
====
Halmashauri ya Jiji la Mbeya imependekeza kuanza mchakato wa kuchunguza na kuligawa Jimbo la Mbeya Mjini kupata jimbo jipya la Uyole, katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 25, 2025.
Jimbo hilo kwa sasa linaongozwa na Dk Tulia Ackson ambaye pia ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Muungano wa Mabunge Duniani (IPU).
Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Mchakato huo ukikamilika na kukidhi vigezo, Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) italitangaza jimbo jipya, jambo ambalo litakuwa jawabu la matakwa ya wakazi wa Mbeya Mjini.
Akizungumza niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa jiji hilo, John Nchimbi leo Machi 11, 2025 katika kikao maalumu cha Baraza la Madiwani, Mkuu wa Idara ya Utumishi na Utawala jijini humo, Nicodemus Tindwa amesema hatua hiyo ni baada ya kupokea barua kutoka Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.
Mwananchi