Pre GE2025 Mbeya yaanza mchakato wa kuligawa jimbo la Mbeya Mjini alipo Tulia Ackson na kupata jimbo lingine la Uyole

Pre GE2025 Mbeya yaanza mchakato wa kuligawa jimbo la Mbeya Mjini alipo Tulia Ackson na kupata jimbo lingine la Uyole

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu,

Wameona wamtengee kabisa Tulia jimbo asipate tabu ya kusumbuana na Sugu, maana wanajua ataibika!

====

1741708044383.jpeg

Halmashauri ya Jiji la Mbeya imependekeza kuanza mchakato wa kuchunguza na kuligawa Jimbo la Mbeya Mjini kupata jimbo jipya la Uyole, katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 25, 2025.

Jimbo hilo kwa sasa linaongozwa na Dk Tulia Ackson ambaye pia ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Muungano wa Mabunge Duniani (IPU).

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Mchakato huo ukikamilika na kukidhi vigezo, Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) italitangaza jimbo jipya, jambo ambalo litakuwa jawabu la matakwa ya wakazi wa Mbeya Mjini.

Akizungumza niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa jiji hilo, John Nchimbi leo Machi 11, 2025 katika kikao maalumu cha Baraza la Madiwani, Mkuu wa Idara ya Utumishi na Utawala jijini humo, Nicodemus Tindwa amesema hatua hiyo ni baada ya kupokea barua kutoka Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.

Mwananchi
 
Sugu ½ Tulia½
Kazi na utu, tunasonga mbele
 
Niliona hilo suala mapema sana.

Kwa maoni yangu, Nguvu kubwa sana zimetumika kwa jambo hili kutokea.

Kumegwa kwa Mbeya.

Jimbo moja la kutetea masilahi ya wawekezaji na jimbo lingine la Wananchi wa kawaida. Hii ndiyo gerrymandering kama inavyoitwa huko Marekani. Ni hatari sana sehemu tuliyofikia.

Mmawia hakutabiri ila alikuwa anajuwa kinachojiri huko.
Hivi majuzi, au niseme toka bethideyi ya Sugu tumeona nini, nani na nani ni nani wakiingia na kutoka Mbeya. Tukiacha Iringa, "Uingereza" na Sasa Mbeya "Marekani" yapo maeneo mengi yanayowatoa mate mabeberu. Na Chama nambari moja itakayokuja kuuza our sovereign state if not states ni CHADEMA na sera yake ya Majimbo.

Narudia Bora CCM kuliko CHADEMA.CCM wanaweza kuwa na baadhi wanaoiba rasilimali kutoka katika ardhi yetu, ila tusiruhusu CHADEMA waje kutuuza mazima, Ardhi na Rasilimali zetu.
Chagua kwa Uangalifu 2025

Chagua kwa uangalifu 2025
 
Wakuu,

Wameona wamtengee kabisa Tulia jimbo asipate tabu ya kusumbuana na Sugu, maana wanajua ataibika!

====


Halmashauri ya Jiji la Mbeya imependekeza kuanza mchakato wa kuchunguza na kuligawa Jimbo la Mbeya Mjini kupata jimbo jipya la Uyole, katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 25, 2025.

Jimbo hilo kwa sasa linaongozwa na Dk Tulia Ackson ambaye pia ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Muungano wa Mabunge Duniani (IPU).

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Mchakato huo ukikamilika na kukidhi vigezo, Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) italitangaza jimbo jipya, jambo ambalo litakuwa jawabu la matakwa ya wakazi wa Mbeya Mjini.

Akizungumza niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa jiji hilo, John Nchimbi leo Machi 11, 2025 katika kikao maalumu cha Baraza la Madiwani, Mkuu wa Idara ya Utumishi na Utawala jijini humo, Nicodemus Tindwa amesema hatua hiyo ni baada ya kupokea barua kutoka Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.

Mwananchi
Bora Waongeze na jimbo lingine MBALIZI 🙂
 
Back
Top Bottom