Joseph_Mungure
Senior Member
- Mar 6, 2021
- 110
- 167
Picha zinazoonyesha viatu vilivyoongezwa kwato kwenye soli ili mtu anapotembea viache nyayo za mnyama ardhini zimesambazwa pia sana mtandaoni.
Miongoni mwa waliosambaza ni gavana wa zamani wa kaunti ya Nairobi Mike Sonko aliyeandika kwamba viatu kama hivyo hutumiwa na wahalifu kaskazini mwa Bonde la Ufa.
Alisema hilo huifanya vigumu kuwafuata wahalifu hao kwani utafikiria nyayo walizoacha ni za ng’ombe.
Waliosambaza picha hizo wamekusudia kuonyesha uvumbuzi wa wahalifu na wezi wa mifugo na jinsi wanavyotumia ubunifu wao kuwakwepa maafisa wa usalama.
Lakini picha hizo hazina uhusiano wowote na Kenya, na si mara ya kwanza kusambaa mitandaoni.
Mapema Julai 2021, zilisambaa mtandaoni Kenya na Nigeria.
Msemaji wa Mbuga ya Taifa ya Kruger nchini Afrika Kusini alisema kwamba ni kweli picha hizo zilipigwa katika mbuga hiyo iliyopo Afrika Kusini,
“Picha hizo zilipigwa baada ya kukamatwa kwa majangili waliodhani wanaweza kuwapotosha askari wetu wenye ujuzi ambao mwishowe walifanikiwa kuwakamata licha ya juhudi zao hizo,” msemaji huyo Isaac Phaahla alisema.
“Hatuwezi kudhibiti kusambaa kwa picha hizo katika mitandao ya kijamii lakini matumaini yetu ni kuwa wenzetu watajifunza kutoka kwa tuliyoyapitia na wasidanganyike na wahalifu hawa.”
Mamlaka ya hifadhi za wanyama nchini Afrika Kusini ilikuwa imeripoti kuhusu kisa cha kilichowahusisha wawindaji haramu mnamo 2 Julai katika hifadhi hiyo.
Mmoja aliuawa katika ufyatulianaji risasi na walinzi na wengine wawili wakatoroka ingawa walikuwa wakiandamwa. Haijabainika iwapo kisa kilichorejelewa ndicho kilichohusisha viatu vilivyo pichani.
Written by @el_mando_tzView attachment 2527025
Miongoni mwa waliosambaza ni gavana wa zamani wa kaunti ya Nairobi Mike Sonko aliyeandika kwamba viatu kama hivyo hutumiwa na wahalifu kaskazini mwa Bonde la Ufa.
Alisema hilo huifanya vigumu kuwafuata wahalifu hao kwani utafikiria nyayo walizoacha ni za ng’ombe.
Waliosambaza picha hizo wamekusudia kuonyesha uvumbuzi wa wahalifu na wezi wa mifugo na jinsi wanavyotumia ubunifu wao kuwakwepa maafisa wa usalama.
Lakini picha hizo hazina uhusiano wowote na Kenya, na si mara ya kwanza kusambaa mitandaoni.
Mapema Julai 2021, zilisambaa mtandaoni Kenya na Nigeria.
Msemaji wa Mbuga ya Taifa ya Kruger nchini Afrika Kusini alisema kwamba ni kweli picha hizo zilipigwa katika mbuga hiyo iliyopo Afrika Kusini,
“Picha hizo zilipigwa baada ya kukamatwa kwa majangili waliodhani wanaweza kuwapotosha askari wetu wenye ujuzi ambao mwishowe walifanikiwa kuwakamata licha ya juhudi zao hizo,” msemaji huyo Isaac Phaahla alisema.
“Hatuwezi kudhibiti kusambaa kwa picha hizo katika mitandao ya kijamii lakini matumaini yetu ni kuwa wenzetu watajifunza kutoka kwa tuliyoyapitia na wasidanganyike na wahalifu hawa.”
Mamlaka ya hifadhi za wanyama nchini Afrika Kusini ilikuwa imeripoti kuhusu kisa cha kilichowahusisha wawindaji haramu mnamo 2 Julai katika hifadhi hiyo.
Mmoja aliuawa katika ufyatulianaji risasi na walinzi na wengine wawili wakatoroka ingawa walikuwa wakiandamwa. Haijabainika iwapo kisa kilichorejelewa ndicho kilichohusisha viatu vilivyo pichani.
Written by @el_mando_tzView attachment 2527025