Mbinu za Kuepuka Utapeli Wakati wa Manunuzi Mtandaoni

Mbinu za Kuepuka Utapeli Wakati wa Manunuzi Mtandaoni

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
- Nunua kwenye tovuti zinazojulikana na kuwa mwangalifu wa herufi za kiunganishi cha tovuti hiyo. Mfano; Amazon.com inaweza kuwa Arnazon.com

- Hakikisha tovuti ina alama ya kufuli kwenye sehemu ya kuonesha kiunganishi. Hii inaonesha tovuti ina tumia HTTPS ambayo ni salama

- Fanya utafiti kuhusu Muuzaji ili kujua historia yake, hii itakusaidia kupata taarifa iwapo ni tapeli

- Epuka kutoa taarifa zako binafsi ambazo hazihusiani na Ununuzi huo kwa Muuzaji. Taarifa zinaweka kutumika vibaya

- Kuwa makini na 'ofa' za ununuzi zinazotolewa mtandaoni hususani kwa Muuzaji/tovuti usizozijua, inaweza kuwa ni mtego wa utapeli
 
mimi yalinikuta kwa kweli niliagiza simu kupitia Alibaba feki, nilichoambulia cha matumaini ni Tracking number feki ya DHL ya kuulizia mzigo ambao hadi leo ni kitendawili. Nilipoteza 175 $.
Ingawa bado naendelea kuagizia bidhaa mara kwa mara lakini kwa sasa natumia mfumo wao wa ndani wa malipo (ALIPAY).
KOSA LANGU kwa kwa wakati ule ilikuwa ni kutuma fedha kwa kutumia WESTERN UNION sitasahau.
 
Back
Top Bottom