Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,468
- 911,184
Mdada kuwa mbalamwezini ni kutii amri ya asilia.
Mie sina kinyongo naelewa ni matakwa ya Muumba.
Walakini anapozua mazogo mie huwa nataabika.
Natamani apite mwezini kwa shwari bila kunitaabisha.
Mbona akiwa mbalamwezini huanzisha mazogo?
Naelewa kero za mbalamwezini pengine kumbughudhi.
Khali yake kubadilika na kujiona pengine hapendeki.
Tumbo kumdodosa na hulazimishwa kujichunga na khali.
Akikhofu zege lisim'minike basi hujisitiri kwa nepi.
Mbona akiwa mbalamwezini huanzisha mazogo!
Kabla na baada ya siku zake vicheko humtawala!
Hiyo khali kunisuuza roho yangu na kulifaidi penzi letu.
Lakini akikamatwa na mbalamwezi huwa mkali mithili ya mbogo!
Sijui huhofu nini kwani mie sina mpango wa pembeni.......
Mbona akiwa mbalamwezini huanzisha mazogo?
La ajabu akimaliza siku zake hunitaka yote yaishe!
Mkakati wake ni kunitongoza hatimaye kunikagua!
Bahati njema huwa sijaguswa na huduma safi kumpatia!
Vifijo na nderemo kunishushia lakini msamaha huwa sipewi!
Mbona akiwa mbalamwezini huanzisha mazogo?
Mie sina kinyongo naelewa ni matakwa ya Muumba.
Walakini anapozua mazogo mie huwa nataabika.
Natamani apite mwezini kwa shwari bila kunitaabisha.
Mbona akiwa mbalamwezini huanzisha mazogo?
Naelewa kero za mbalamwezini pengine kumbughudhi.
Khali yake kubadilika na kujiona pengine hapendeki.
Tumbo kumdodosa na hulazimishwa kujichunga na khali.
Akikhofu zege lisim'minike basi hujisitiri kwa nepi.
Mbona akiwa mbalamwezini huanzisha mazogo!
Kabla na baada ya siku zake vicheko humtawala!
Hiyo khali kunisuuza roho yangu na kulifaidi penzi letu.
Lakini akikamatwa na mbalamwezi huwa mkali mithili ya mbogo!
Sijui huhofu nini kwani mie sina mpango wa pembeni.......
Mbona akiwa mbalamwezini huanzisha mazogo?
La ajabu akimaliza siku zake hunitaka yote yaishe!
Mkakati wake ni kunitongoza hatimaye kunikagua!
Bahati njema huwa sijaguswa na huduma safi kumpatia!
Vifijo na nderemo kunishushia lakini msamaha huwa sipewi!
Mbona akiwa mbalamwezini huanzisha mazogo?