Mbona miaka ya hivi karibuni klabu zinazoshuka daraja epl ni rahisi tena kurudi epl ndani ya muda mfupi?

man dunga

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2013
Posts
3,358
Reaction score
5,783
Fulham ameshapanda wakati kashuka msimu wa karibuni. Norwich , Watford nao wanashuka na kupanda ndani ya muda mfupi. Burnemouth nae anaelekea kupanda wakati kashuka msimu uliopita.

Zamani ilikuwa ngumu, au viwango vya wachezaji wa kiingereza ambao ndio wengi vimeshuka? Akina fei toto , Manula n.k wakatafute fursa huko championship.
 
Bournemouth sio kwamba anaelekea...
Tayari ameshapanda..
Bado timu moja TU..

Sababu ni kuwa wanaongeza uwekezaji kutokana na malipo ambayo tayari wameshapata huko EPL,
Na wakati mwingine timu inakuwa haijabadili sana wachezaji..

Mpira siku hizi ni pesa na sio vipaji peke yake,
So mtu akitoka EPL tayari huwez kumlinganisha na mtu wa Ligue 1 au championship
 
Kama timu iliyoshuka itaweza kuwa na wachezaji iliokua nao ligi kuu angalau saba tu basi tayari ana kikosi cha kufunga timu nyingi za huko chini.

Plus anakua na financial muscle kuzidi aliowakuta so atahitaji kusajili viraka wa hapa na pale kisha mengine yatafuata.
 
Timu ikishuka daraja endapo haitauza wachezaji wake uwezekano wa kuludi ni mkubwa sana.

Mfano Sunderland ilishuka ikauza wachezaji wengi mpaka ikashuka tena daraja saizi ipo daraja la kwanza huko.
 
Ushindani ligi kuu ni mkubwa, hivyo timu zinazoshuka zinashuka zikiwa bora, tizama nafasi ya everton mfano sasa hivi, ikitokea akishuka kuoanda eazy tu, unakumbuka sakata la juve kushushwa daraja kule italia, alirudi kwa kishindo sababu ya ubora wa timu.
 
Mshiko wanaoshuka nao ni mkubwa sana, pia hizi timu mishahara yao ni paund 10000 kwa wiki
Hadi 2000
 
timu zinapo panda EPL zinapata pesa nyingi sna kama zawadi na pia timu zinapo shuka zina lipwa parachute money na FA ya england.. pesa inayo fanya ziweze kubakisha wachezaji wake weng bora na ivyo kupanda tena kurud ligi kuu inakuwa ni rahisi.
 
timu zinapo panda EPL zinapata pesa nyingi sna kama zawadi na pia timu zinapo shuka zina lipwa parachute money na FA ya england.. pesa inayo fanya ziweze kubakisha wachezaji wake weng bora na ivyo kupanda tena kurud ligi kuu inakuwa ni rahisi.
Kwa hiyo mkuu zamani walikuwa wanapewa kiasi kidogo na hivyo kushindwa kubakisha wachezaji? Akina Portsmouth, bolton, reading, birmingham n.k tangu washuke hawajarudi tena
 
Na hapa kwetu ndio hivyo hivyo. Zipo ambazo zikishuka hazidimi sana, mfano Costal Union, Ruvu Shooting, Ruvu JKT, na Ihefu (inakaribia kurudi).

Zipo ambazo zikishuka zinadima sana halafu zinarudi. Mfano Maji Maji, Lipuli, Mwadui.

Kuna timu kama Pan Africa, Pamba, African Sports, Cosmo Politan tangu zishuke zimeganda huko huko.
Na zipo ambazo hazijawahi kushuka.
So nikawaida tu hiyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…