Yupo wapi sasa huyo GK? Halafu uwe unapunguza masikhara, maana katika wale vijana kila mtu alikua na style yaks na kila mtu alikua anajitungoa mashairi ya sehemu yake.
Gwamaka Kalihura a.k.a GK alikua na style yake iliyokua ina ficha na kubalance hali yake ya kigugumizi, pia iliyokua ina akisi mitazamo yake ya kupenda ugomvi na ubabe na matusi mengi. Hata majina aliyojiita yalionyesha ni mtu wa aina gani au aliyependa hali gani au aliyrpenda kuinekanaje. Ndiyo maa akawa anajiita King Crazy GK, Amiri jeshi mkuu, Bokasa etc
Wakati Ambwene Yessaya (AY) yeye alikua hana muda wa kuonya au kuelimisha au kutisha mtu keenye mashairi yake, yeye aliamua kuja na mashairi yanayolenga ku burudisha zaidi. Yeye alipokua akitunga mashairi anafikiria zaidi jinsi watu watakavyo kuwa wana swing na party huko club na ndiyo maana aliamua kuniita Mzee wa Commercial.
Khamis Mwinjuma,a.k.a Mwanafalsa baadaye Mwana Fa, yeye alikuja na style ya mashairi ya kufikirisha zaidi, yenye nasaha, elimu, ya halinya juu ambayo yamengwa fungwa katika mfumo wa lygha unaohitaji kutuliza akili ili kumuelewa. Mashairi hasa ambayo yanahitaji uelewa katika usanifu wa kiswahili. Na mfumo wa utunzi wa kiswahili uliathiriwa na kuwa shaped na tabia yake ya tangu anakua ya kupenda kusoma na kuandika mashairi (Malenga).
Hawa vijana kila mmoja alikua na wapenzi wake ingawa Mwana Fa ndiye alikua na maneno yaliyokaa vichwani mwa watu wa Marika yote ingawa siku zote ilikua ngumu kuumba au kuyakarili mashairi yake zaidi ya kuyafurahia aimbapo alikua na misamiati iliyoishi kwa muda mrefu.
Unaposema GK ndiye alikua na uwezo mkubwa kuliko wengine wote katika lile kundi lao, unakia umenionyesha wewe ni mtu wa aina gani, yaani ni mtu wa kubutua butua, piga mitama, ngado kwa ng'ado, mtaa kwa mtaa, utawachinja kama bokasa, amiri jeshi mkuu umesha lianzisha....yaani mtu wa hivyo