Mbona Mzee wa Komesho(AY) hakumualika Crazy GK kwenye harusi yake?

Hatahivyo uwezo wa GK katika utungaji wa mashairi na uchanaji uko juu sana kwa kulinganisha na hao matoz 2 wanaishi kwa maigizo.
 
Hatahivyo uwezo wa GK katika utungaji wa mashairi na uchanaji uko juu sana kwa kulinganisha na hao matoz 2 wanaishi kwa maigizo.
Yupo wapi sasa huyo GK? Halafu uwe unapunguza masikhara, maana katika wale vijana kila mtu alikua na style yake na kila mtu alikua anajitungia mashairi ya sehemu yake.
Gwamaka Kalihura a.k.a GK alikua na style yake iliyokua ina ficha na kubalance hali yake ya kigugumizi, pia iliyokua ina akisi mitazamo yake ya kupenda ugomvi na ubabe na matusi mengi. Hata majina aliyojiita yalionyesha ni mtu wa aina gani au aliyependa hali gani au aliyependa kuonekanaje. Ndiyo maa akawa anajiita King Crazy GK, Amiri jeshi mkuu, Bokasa etc

Wakati Ambwene Yessaya (AY) yeye alikua hana muda wa kuonya au kuelimisha au kutisha mtu kwenye mashairi yake, yeye aliamua kuja na mashairi yanayolenga ku burudisha zaidi. Yeye alipokua akitunga mashairi anafikiria zaidi jinsi watu watakavyo kuwa wana swing na party huko club na ndiyo maana aliamua kujiita Mzee wa Commercial.

Khamis Mwinjuma,a.k.a Mwanafalsa baadaye Mwana Fa, yeye alikuja na style ya mashairi ya kufikirisha zaidi, yenye nasaha, elimu, ya hali ya juu ambayo yamefungwa fungwa katika mfumo wa lugha unaohitaji kutuliza akili ili kumuelewa. Mashairi hasa ambayo yanahitaji uelewa katika usanifu wa kiswahili. Na mfumo wa utunzi wa kiswahili uliathiriwa na kuwa shaped na tabia yake ya tangu anakua ya kupenda kusoma na kuandika mashairi (Malenga).
Hawa vijana kila mmoja alikua na wapenzi wake ingawa Mwana Fa ndiye alikua na maneno yaliyokaa vichwani mwa watu wa Marika yote ingawa siku zote ilikua ngumu kuimba au kuyakarili mashairi yake zaidi ya kuyafurahia aimbapo alikua na misamiati iliyoishi kwa muda mrefu vichwani mwa watu na ndani ya jamii.
Unaposema GK ndiye alikua na uwezo mkubwa kuliko wengine wote katika lile kundi lao, unakua umenionyesha wewe ni mtu wa aina gani, yaani ni mtu wa kubutua butua, piga mitama, ng"ado kwa ng'ado, mtaa kwa mtaa, utawachinja kama bokasa, amiri jeshi mkuu umesha lianzisha....yaani mtu wa hivyo.
 
Well said,Ni GK huyohuyo na ile staili yake ya kurap km DMX ndiye aliye pionia bifu la ECT na TMK though staili ya kurap ya GK ilikua simple sana na ilikua inawakosha wengi,wenye kaliba yake....but frankly speaking Kuondoka kwa FA na AY ilikua pigo kwa GK.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…