Mbona Tanzania haishiriki katika Winter Olympics?

Gogle

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2013
Posts
1,495
Reaction score
867
Kwani ni lazima nchi zinazoshiriki ziwe na snow?
 
Ni mashindano ya kuteleza kwenye barafu. Ni mashindano yanayohusu mambo ya baridi kali Tanzania wapi na wapi
 
Yetu tunashiriki pale Kilimanjaro kilelen
 
Winter Olympic ni kwa ajili ya nchi za barafu tu!.
Nigeria wanashiriki na ile timu ya wanawake wanne....wanateleza kwenye barafu na vigari ....
Kumbe Nigeria kuna barafu....haha
 
Nigeria wanashiriki na ile timu ya wanawake wanne....wanateleza kwenye barafu na vigari ....
Kumbe Nigeria kuna barafu....haha
Usiwe mshamba hao ni nchi waalikwa hata wewe ukifikia vigezo unaweza alikwa!.. Ajabu yawezekana hata hujui maana ya Summer olympics, Winter Olympics na paralympic!.
 
Usiwe mshamba hao ni nchi waalikwa hata wewe ukifikia vigezo unaweza alikwa!.. Ajabu yawezekana hata hujui maana ya Summer olympics, Winter Olympics na paralympic!.
Ndio tueleweshe sasa
 
Ndio tueleweshe sasa
kifupi hizi olympics games zote huandaliwa na kamati ya michezo ya olympics au International Olympic Committee (IOC}
  1. Summer olympics Games.
    Hapa ndio michezo yote huchezwa hadi na ndio nchi zote bila ubaguzi zinazofuzu hupata nafasi kwenda shiriki. Mashindano haya hufanyika kila baada ya miaka minne (4) na mara ya mwisho yalikuwa Rio de Janeiro, Brazil mwaka 2016. Yanatarajia kufanyika 2020 Tokyo, Japan.
  2. Winter olympics Games.
    Mafanikio ya namba 1 (SO) yakapelekea kuzalisha WO ambayo inafanyika PyeongChang, SK na ni maeneo ya sehemu za barafu sababu michezo yake inahusu barafu zaidi ila kuna nchi zinaenda lakini zinakua nchi alikwa. Russia alizuiwa kwenda sababu ilionekana wachezaji wake wanatumia madawa, lakini baadae wameruhusiwa kwenda lakini kama wachezaji huru ina maana hawataiwakilisha nchi ya urusi.
  3. Paralympics Games.
    Haya ni mashindano kwa ajiri ya walemavu!. Nayo yatafanyika mwaka huu pia huko huko SK.
Ntolonyonyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…