Mbowe chukua somo muhimu kwa Trump, MAGA na Republicans uiponye CHADEMA

Mbowe chukua somo muhimu kwa Trump, MAGA na Republicans uiponye CHADEMA

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Wakati Trump anaibuka kugombea urais mwaka 2016 alipingwa karibia na establishment yote ya chama cha Republicans, alikuwa anaonekana mropokaji na kituko tu mbele ya "wenye chama", hakuna aliyedhani angefika mbali ila leo hii ni Rais wa Marekani kwa awamu ya pili.

Kama wajumbe tu wa chama cha Republicans ndio wangekuwa wanapiga kura kwa uhakika Trump asingetoboa, angeshindwa vibaya sana, bahati yake nzuri wanachama wote ndio waliokuwa wapiga kura kumchagua mgombea Urais.

Sasa hivi Trump ile Republican ya zamani yote kaifagilia mbali, kama wewe sio movement yake ya MAGA huwezi tuna kufurukuta au kusikika ndani ya chama cha Republicans. Miamba ya Republicans wakina Familia ya Bush, Dick Cheney, John Bolton, John Boehner, Paul Ryan na wengine wengi waliomkataa Trump wamepotea kabisa katika siasa za Republicans na nchi ya Marekani.

Kwa upepo uliopo ninaamini kama kura zingekuwa zinapigwa na wanachama wote wa CHADEMA Mbowe hawezi kushinda ila kwa wajumbe wa CHADEMA anaweza kushinda kwa sababu zozote zile(sio jambo la ajabu wajumbe wengi kuwa disconnected na uhalisia uliopo kwa wanachama wao na raia kwa ujumla)

Mbowe itakusaidia nini ukishinda kwa wajumbe halafu wanachama na raia hawako pamoja na wewe? Utakuwa umeisaidiaje CHADEMA katika hali hiyo?
 
Wakati Trump anaibuka kugombea urais mwaka 2016 alipingwa karibia na establishment yote ya chama cha Republicans, alikuwa anaonekana mropokaji na kituko tu mbele ya "wenye chama", hakuna aliyedhani angefika mbali ila leo hii ni Rais wa Marekani kwa awamu ya pili.

Kama wajumbe tu wa chama cha Republicans ndio wangekuwa wanapiga kura kwa uhakika Trump asingetoboa, angeshindwa vibaya sana, bahati yake nzuri wanachama wote ndio waliokuwa wapiga kura kumchagua mgombea Urais.

Sasa hivi Trump ile Republican ya zamani yote kaifagilia mbali, kama wewe sio movement yake ya MAGA huwezi tuna kufurukuta au kusikika ndani ya chama cha Republicans. Miamba ya Republicans wakina Familia ya Bush, Dick Cheney, John Bolton, John Boehner, Paul Ryan na wengine wengi waliomkataa Trump wamepotea kabisa katika siasa za Republicans na nchi ya Marekani.

Kwa upepo uliopo ninaamini kama kura zingekuwa zinapigwa na wanachama wote wa CHADEMA Mbowe hawezi kushinda ila kwa wajumbe wa CHADEMA anaweza kushinda kwa sababu zozote zile(sio jambo la ajabu wajumbe wengu kuwa disconnected na uhalisia uliopo kwa wanachama wao na raia kwa ujumla)

Mbowe itakusaidia nini ukishinda kwa wajumbe halafu wanachama na raia hawako pamoja na wewe? Utakuwa umeisaidiaje CHADEMA katika hali hiyo?
Umenena vema mkuu.
 
Mara ya mwisho ulikuwa pamoja na Wenje.

Vipi bado unaendelea na msimamo huo?
Mpaka sasa hivi sioni uthibitisho wa maana wa Wenje au Mbowe kuhongwa na CCM, Abdul au dola ila natambua wana CHADEMA wengi wanaamini hivyo na chama ni wanachama walio wengi. Haijalishi Mbowe, Wenje na kundi lake ni wasafi kiasi gani, wanachama walio wengi wakikukataa wamekukataa tu na katika demokrasia ni muhimu kuheshimu machaguo au maoni ya walio wengi.
 
Mpaka sasa hivi sioni uthibitisho wa maana wa Wenje au Mbowe kuhongwa na CCM, Abdul au dola ila natambua wana CHADEMA wengi wanaamini hivyo na chama ni wanachama walio wengi. Haijalishi Mbowe, Wenje na kundi lake ni wasafi kiasi gani, wanachama walio wengi wakikukataa wamekukataa tu na katika demokrasia ni muhimu kuheshimu machaguo au maoni ya walio wengi.
Leo hii unasema huoni uthibitisho lakini ni wewe huyo huyo ambaye ulikuwa tayari kuyakubali maneno ya Wenje kuhusu swala la kumsaidia Lissu apate stahiki zake kupitia Abdul bila uthibitisho.

Ulikubali maneno ya Wenje aliyoyatoa bila uthibitisho na kuwa upande wake huku ukidai kuwa maneno hayo yamejitosheleza sana ikiwemo na pale aliposema aliwahi kumkopa Lissu na ndio maana ana maslahi kwenye hizo hela mpaka kumleta Abdul nyumbani kwa Lissu.

Hayo yote uliyakubali bila uthibitisho. Leo vipi ufanye u-turn ya 360 kuanza kama ambavyo role model wako amekuwa accused kufanya?
 
Hii ni organic movement upepo hauvumi kwa Mbowe wakati huu sijui kwanini hashtuki .

Issue sio kujitoa au kugombea issue kubwa ni watu [wanachama na mashabiki wa chadema] kupoteza imani pakubwa juu yake.

Mtu anaweza kulibeza hili ila ukweli wanamabadiliko wengi hata wasio na chama waliamini Chadema kwa muda mrefu na hawa ndio walichangia pakubwa ile 2020 milioni 70 Mbowe asifungwe.

Hawa ndio wamepoteza imani nae ila yeye akaona awaite wabangaizaji, binafsi naamini uchaguzi hautokuwa huru maana tayari kuna influence ya pesa za Abdul kuhonga wajumbe na wengi wapo kwa matumbo yao na kumtegemea Mbowe kupata mkate wao huku wakijifaragua ni wanaharakati na wanamageuzi.

Mbowe atakaposhinda ndio mgawanyiko na wananageuzi halisi watajitenga na Chadema mpya itakayoongozwa na rimoti za Abdul na mama yake.
 
Mbowe itakusaidia nini ukishinda kwa wajumbe halafu wanachama na raia hawako pamoja na wewe? Utakuwa umeisaidiaje CHADEMA katika hali hiyo?
Maswali mazuri sana haya..

Mbowe angetanguliza mbele maslahi ya Chadema huenda hata asingegombea tena uenyekiti wa Chadema kama vile alivyoahidi alivyochaguliwa mara ya mwisho.
 
Leo hii unasema huoni uthibitisho lakini ni wewe huyo huyo ambaye ulikuwa tayari kuyakubali maneno ya Wenje kuhusu swala la kumsaidia Lissu apate stahiki zake kupitia Abdul bila uthibitisho.

Ulikubali maneno ya Wenje aliyoyatoa bila uthibitisho na kuwa upande wake huku ukidai kuwa maneno hayo yamejitosheleza sana ikiwemo na pale aliposema aliwahi kumkopa Lissu na ndio maana ana maslahi kwenye hizo hela mpaka kumleta Abdul nyumbani kwa Lissu.

Hayo yote uliyakubali bila uthibitisho. Leo vipi ufanye u-turn ya 360 kuanza kama ambavyo role model wako amekuwa accused kufanya?
Lissu amethibitisha mwenyewe kutaka kusaidiwa na Abdul kupata stahiki zake, na alimuambia kabisa Abdul akimsaidia kupata pesa zake atakuwa rafiki yake.
 
Lissu amethibitisha mwenyewe kutaka kusaidiwa na Abdul kupata stahiki zake, na alimuambia kabisa Abdul akimsaidia kupata pesa zake atakuwa rafiki yake.
Alithibitisha kwa ushahidi upi?

Kwasababu kama unataka kuita maneno yale yale aliyoyasema Lissu kuwa ni ushahidi bila kitu kingine cha ziada cha ku sapoti basi ulitakiwa ukubali na zile shutuma za rushwa kumhusu Wenje na Abdul kwasababu ni huyo huyo Lissu ndio aliyesema.

Lissu hakuanza tu kwa kusema "Abdul akimsaidia atakuwa rafiki yake" hii ndio quote inayoonesha udhaifu wa followers wengi wa Wenje pamoja na Wenje mwenyewe.

Hamuelezei mlolongo ulipoanzia mpaka kufikia kwenye kauli hiyo nyie mnahitimisha tu kwa jumping to conclusions.

Lissu kabla hajafika kwenye hilo neno ambalo wewe na Wenje mnalitumia kama utetezi alisema Abdul alikuja na approach ya rushwa na aka declare kuwa tayari viongozi wenzake wamepewa.

Haya maneno hamyasemi mnarukia rukia tu kwenye "Lissu alisema Abdul akimsaidia atakuwa rafiki yake"

Halafu hoja nyingine nayotaka kuiweka ni kuwa kama wewe unakubali maneno ya Wenje kwasababu yamefanana na kauli alizotoa Lissu na kusema kwamba ni za kweli kwasababu wote walikuwa wahusika kwenye hilo tukio.

Kumbuka kwenye tukio kulikuwa na jumla ya watu wanne ambao ni Wenje, Abdul, Lissu na mfanyakazi wake Lissu.

Huyu mfanyakazi wake Lissu tayari amehojiwa na amekiri kwa kueleza kile kile alichozungumza Lissu. Video hii hapa chini.


View: https://youtu.be/rpoAjfR3a5g

Kama ulikubali kwasababu Lissu alisema basi unatakiwa ukubali kwasababu msaidizi wa Lissu amesema kwakua naye alikuwa part of the conference.

Otherwise ukubali tu kuwa ulikuwa unam quote nukta chache tu ambazo kwa upande wako zilikuwa zina feed ego yako.
 
Alithibitisha kwa ushahidi upi?

Kwasababu kama unataka kuita maneno yale yale aliyoyasema Lissu kuwa ni ushahidi bila kitu kingine cha ziada cha ku sapoti basi ulitakiwa ukubali na zile shutuma za rushwa kumhusu Wenje na Abdul kwasababu ni huyo huyo Lissu ndio aliyesema.

Lissu hakuanza tu kwa kusema "Abdul akimsaidia atakuwa rafiki yake" hii ndio quote inayoonesha udhaifu wa followers wengi wa Wenje pamoja na Wenje mwenyewe.

Hamuelezei mlolongo ulipoanzia mpaka kufikia kwenye kauli hiyo nyie mnahitimisha tu kwa jumping to conclusions.

Lissu kabla hajafika kwenye hilo neno ambalo wewe na Wenje mnalitumia kama utetezi alisema Abdul alikuja na approach ya rushwa na aka declare kuwa tayari viongozi wenzake wamepewa.

Haya maneno hamyasemi mnarukia rukia tu kwenye "Lissu alisema Abdul akimsaidia atakuwa rafiki yake"

Halafu hoja nyingine nayotaka kuiweka ni kuwa kama wewe unakubali maneno ya Wenje kwasababu yamefanana na kauli alizotoa Lissu na kusema kwamba ni za kweli kwasababu wote walikuwa wahusika kwenye hilo tukio.

Kumbuka kwenye tukio kulikuwa na jumla ya watu wanne ambao ni Wenje, Abdul, Lissu na mfanyakazi wake Lissu.

Huyu mfanyakazi wake Lissu tayari amehojiwa na amekiri kwa kueleza kile kile alichozungumza Lissu. Video hii hapa chini.


View: https://youtu.be/rpoAjfR3a5g

Kama ulikubali kwasababu Lissu alisema basi unatakiwa ukubali kwasababu msaidizi wa Lissu amesema kwakua naye alikuwa part of the conference.

Otherwise ukubali tu kuwa ulikuwa unam quote nukta chache tu ambazo kwa upande wako zilikuwa zina feed ego yako.

Lissu alikuwa anataka Abdul amsaidie kupata malipo yake kama nani?
 
Lissu alikuwa anataka Abdul amsaidie kupata malipo yake kama nani?
Hata hili nalo umeshindwa kulielewa?

The same damn question.

Ikiwa Wenje anasema ujio wa Abdul haukuwa na implications za rushwa, unaweza kuniambia Wenje alimleta Abdul ili aje amsaidie Lissu kama nani?

Inaonekana unakosa umakini kwenye speech za Lissu au unatatizo personal la uelewa.

Kwa hiyo hoja ya Abdul amsaidie Lissu ili kupata stahiki, ni tofauti na Abdul amsaidie Lissu kufikisha documents ili apate stahiki zake.

Lissu alimpatia documents Abdul ili amfikishie raisi sio kwasababu za kimadaraka (uongozi) bali ni kwasababu za ukaribu wake na raisi ukizingatia yule ni mama yake hivyo ana access hiyo.

Na ndio maana Lissu alikuwa mtu wa kwanza kum-question authority ya Abdul kuwa mwakilishi huko Uganda kwasababu ni jambo la kimadaraka (uongozi) ambao yeye hana.
 
Back
Top Bottom