Mbowe: Ilikuwa miaka saba ya maumivu

Mbowe: Ilikuwa miaka saba ya maumivu

Oldmantz

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2023
Posts
704
Reaction score
1,457
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema miaka saba iliyopita ilikuwa ya bonde la maumivu makali kwa wananchi wote. Alitaja maumivu hayo akihusisha wale waliofungwa magerezani na watumishi waliofukuzwa kwa kigezo cha vyeti feki.

Mbowe aliyasema hayo jana mkoani Njombe alipokuwa akiwahutubia wananchi mkoani humo, ikiwa ni mwendelezo wa mikutano ya hadhara baada ya kuruhusiwa hivi karibuni.

“Wako walionyang’anywa mali, Tanzania ikageuzwa kuwa Taifa la mateso, wananchi wakaishi kwenye hofu, lakini kwa wiki moja tuliyofanya mikutano ya hadhara, nikiliangalia Jeshi la Polisi silielewi mbona limekuwa na ubinadamu hivyo,”alisema Mbowe.

Alisema miaka saba iliyopita jeshi hilo halikuwa hivyo, lakini wanashukuru kwa sasa hali hiyo imebadilika na wanaamini kiongozi wa nchi anatengeneza vyombo vya dola kwa kuzingatia misingi ya kujali haki kwa wote.
“Tunachokiona leo ni Tanzania tunayoipenda Chadema tukizungumza, polisi wapo wanalinda amani na wanasikiliza sera.Tulifika hatua polisi wetu walionekana maadui kwa wananchi na raia, walikuwa wanawaombea mambo mabaya,”alisema.

Kiongozi huyo alisema vyombo vya ulinzi na usalama siku zote vinapaswa kusimamia amani, huku akieleza siku chama hicho kikishika dola hawataagiza polisi kutoka mataifa mengine, bali vijana hao wataendelea na wajibu huo katika mazingira bora.

“Msipendelee Chadema, simamieni haki kwa vyama vyote, thawabu yenu mtaipata duniani na mbinguni lakini mkipewa amri za kuhatarisha amani, msizisikilize,”alisema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kanda ya Nyasa, Mchungaji Peter Msigwa alisema sera ya chama hicho imekuwa ikizungumzia sera ya majimbo, inayosisitiza watu katika maeneo yao wawachague watu wenye uwezo wa kuwawajibisha wale waliowachagua pale wanapobaini uwezo wao ni mdogo.

Kilimo
Akizungumza suala la kilimo, Msigwa alisema katika maeneo mbalimbali waliyozunguka kipindi hiki cha mikutano, wakulima wa mazao mbalimbali yakiwamo ndizi, parachichi, kahawa, cocoa, pareto, mpunga, mahindi, bado wanatekeleza kilimo chao kwa gharama kubwa.

“Na mazao mengi yanalimwa kanda ya Nyasa, halafu anakuja mtu mmoja ambaye hajulikani anakuja kuwapangia namna ya kutumia rasilimali zenu hili haliwezekani,”alisema Msigwa.

Alinukuu maneno ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kuwa aliwaambia wananchi wa Njombe, ili waweze kuendelea wanahitaji vitu vitatu ambavyo ni watu, ardhi na siasa safi.

Credit: MWANANCHI NEWSPAPER

 
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema miaka saba iliyopita ilikuwa ya bonde la maumivu makali kwa wananchi wote. Alitaja maumivu hayo akihusisha wale waliofungwa magerezani na watumishi waliofukuzwa kwa kigezo cha vyeti feki.

Mbowe aliyasema hayo jana mkoani Njombe alipokuwa akiwahutubia wananchi mkoani humo, ikiwa ni mwendelezo wa mikutano ya hadhara baada ya kuruhusiwa hivi karibuni.

“Wako walionyang’anywa mali, Tanzania ikageuzwa kuwa Taifa la mateso, wananchi wakaishi kwenye hofu, lakini kwa wiki moja tuliyofanya mikutano ya hadhara, nikiliangalia Jeshi la Polisi silielewi mbona limekuwa na ubinadamu hivyo,”alisema Mbowe.

Alisema miaka saba iliyopita jeshi hilo halikuwa hivyo, lakini wanashukuru kwa sasa hali hiyo imebadilika na wanaamini kiongozi wa nchi anatengeneza vyombo vya dola kwa kuzingatia misingi ya kujali haki kwa wote.
“Tunachokiona leo ni Tanzania tunayoipenda Chadema tukizungumza, polisi wapo wanalinda amani na wanasikiliza sera.Tulifika hatua polisi wetu walionekana maadui kwa wananchi na raia, walikuwa wanawaombea mambo mabaya,”alisema.

Kiongozi huyo alisema vyombo vya ulinzi na usalama siku zote vinapaswa kusimamia amani, huku akieleza siku chama hicho kikishika dola hawataagiza polisi kutoka mataifa mengine, bali vijana hao wataendelea na wajibu huo katika mazingira bora.

“Msipendelee Chadema, simamieni haki kwa vyama vyote, thawabu yenu mtaipata duniani na mbinguni lakini mkipewa amri za kuhatarisha amani, msizisikilize,”alisema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kanda ya Nyasa, Mchungaji Peter Msigwa alisema sera ya chama hicho imekuwa ikizungumzia sera ya majimbo, inayosisitiza watu katika maeneo yao wawachague watu wenye uwezo wa kuwawajibisha wale waliowachagua pale wanapobaini uwezo wao ni mdogo.

Kilimo
Akizungumza suala la kilimo, Msigwa alisema katika maeneo mbalimbali waliyozunguka kipindi hiki cha mikutano, wakulima wa mazao mbalimbali yakiwamo ndizi, parachichi, kahawa, cocoa, pareto, mpunga, mahindi, bado wanatekeleza kilimo chao kwa gharama kubwa.

“Na mazao mengi yanalimwa kanda ya Nyasa, halafu anakuja mtu mmoja ambaye hajulikani anakuja kuwapangia namna ya kutumia rasilimali zenu hili haliwezekani,”alisema Msigwa.

Alinukuu maneno ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kuwa aliwaambia wananchi wa Njombe, ili waweze kuendelea wanahitaji vitu vitatu ambavyo ni watu, ardhi na siasa safi.

Credit: MWANANCHI NEWSPAPER

Ukiona kiongozi anatetea veti feki ujue amna kitu kichwani au na yeye anacheti feki
 
Angejua Wachaga wanavyompenda JPM hangesema vile. Hata waliokuwa hawampendi baada ya kifo (JPM)wanajuta na kusema alikuwa "mwamba".
 
Mbowe na chadema ni matapeli kama matapeli wengine.
Mbowe na chadema watatumia miaka 7 ijayo kuelezea wanayoita mateso waliyopitia chini ya Magufuli.

Hakuna hoja ya msingi, ni Magufuli asubuhi hadi jioni.
 
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema miaka saba iliyopita ilikuwa ya bonde la maumivu makali kwa wananchi wote. Alitaja maumivu hayo akihusisha wale waliofungwa magerezani na watumishi waliofukuzwa kwa kigezo cha vyeti feki.

Mbowe aliyasema hayo jana mkoani Njombe alipokuwa akiwahutubia wananchi mkoani humo, ikiwa ni mwendelezo wa mikutano ya hadhara baada ya kuruhusiwa hivi karibuni.

“Wako walionyang’anywa mali, Tanzania ikageuzwa kuwa Taifa la mateso, wananchi wakaishi kwenye hofu, lakini kwa wiki moja tuliyofanya mikutano ya hadhara, nikiliangalia Jeshi la Polisi silielewi mbona limekuwa na ubinadamu hivyo,”alisema Mbowe.

Alisema miaka saba iliyopita jeshi hilo halikuwa hivyo, lakini wanashukuru kwa sasa hali hiyo imebadilika na wanaamini kiongozi wa nchi anatengeneza vyombo vya dola kwa kuzingatia misingi ya kujali haki kwa wote.
“Tunachokiona leo ni Tanzania tunayoipenda Chadema tukizungumza, polisi wapo wanalinda amani na wanasikiliza sera.Tulifika hatua polisi wetu walionekana maadui kwa wananchi na raia, walikuwa wanawaombea mambo mabaya,”alisema.

Kiongozi huyo alisema vyombo vya ulinzi na usalama siku zote vinapaswa kusimamia amani, huku akieleza siku chama hicho kikishika dola hawataagiza polisi kutoka mataifa mengine, bali vijana hao wataendelea na wajibu huo katika mazingira bora.

“Msipendelee Chadema, simamieni haki kwa vyama vyote, thawabu yenu mtaipata duniani na mbinguni lakini mkipewa amri za kuhatarisha amani, msizisikilize,”alisema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kanda ya Nyasa, Mchungaji Peter Msigwa alisema sera ya chama hicho imekuwa ikizungumzia sera ya majimbo, inayosisitiza watu katika maeneo yao wawachague watu wenye uwezo wa kuwawajibisha wale waliowachagua pale wanapobaini uwezo wao ni mdogo.

Kilimo
Akizungumza suala la kilimo, Msigwa alisema katika maeneo mbalimbali waliyozunguka kipindi hiki cha mikutano, wakulima wa mazao mbalimbali yakiwamo ndizi, parachichi, kahawa, cocoa, pareto, mpunga, mahindi, bado wanatekeleza kilimo chao kwa gharama kubwa.

“Na mazao mengi yanalimwa kanda ya Nyasa, halafu anakuja mtu mmoja ambaye hajulikani anakuja kuwapangia namna ya kutumia rasilimali zenu hili haliwezekani,”alisema Msigwa.

Alinukuu maneno ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kuwa aliwaambia wananchi wa Njombe, ili waweze kuendelea wanahitaji vitu vitatu ambavyo ni watu, ardhi na siasa safi.

Credit: MWANANCHI NEWSPAPER

Ngoja walinda legacy waje, haiwezekan Mbowe aseme ilikua miaka saba ya maumiv kwamba waliumizwa na nan? Hizo mali nan aliiba? Ina maan awamu ile ilikua na wezi? Hii haikubaliki!!!
 
Mbowe na chadema ni matapeli kama matapeli wengine.
Mbowe na chadema watatumia miaka 7 ijayo kuelezea wanayoita mateso waliyopitia chini ya Magufuli.

Hakuna hoja ya msingi, ni Magufuli asubuhi hadi jioni.
Shetani amesemwa tangu enzi za Adam.mpaka leo. Mwovu siku zote husemwa pamoja na uovu wake.

Utawala wa kidikteta wa awamu ya 5 chini ya dikteta Magufuli utasemwa kwa vizazi vingi vijavyo. Na lazima ataingizwa kwenye kumbukumbu za kitaifa kama mtu mwovu aliyewahi kuwa kiongozi mkuu wa nchi.

Na hakika, kwa karne nyingi zijazo, Taifa halitakubali kuwa na kiongpzi dikteta kama marehemu Magufuli. Watu watamtazama mgombea na kusema, huyu hapana, anaweza kuja kuwa Maguguli mwingine.
 
Shetani amesemwa tangu enzi za Adam.mpaka leo. Mwovu siku zote husemwa pamoja na uovu wake.

Utawala wa kidikteta wa awamu ya 5 chini ya dikteta Magufuli utasemwa kwa vizazi vingi vijavyo. Na lazima ataingizwa kwenye kumbukumbu za kitaifa kama mtu mwovu aliyewahi kuwa kiongozi mkuu wa nchi.

Na hakika, kwa karne nyingi zijazo, Taifa halitakubali kuwa na kiongpzi dikteta kama marehemu Magufuli. Watu watamtazama mgombea na kusema, huyu hapana, anaweza kuja kuwa Maguguli mwingine.
Magufuli hajawahi kua dikteta. Ni propaganda za watu wajinga tu ila waelevu tunajua Magufuli hajawahi kua dikteta.

Magufuli kwa mambo makubwa aliyoifanyia hii nchi kwa miaka 5 atakumbukwa milele.

Vizazi na vizazi vitakua vinajifunza kwamba Magufuli alijenga bwawa, alijenga sgr, alitandaza barabara nchi nzima, alinunua ndege, alihamishia serikali Dodoma, alienga maduka ya madawa ya serikali kila wilaya, lijenga hospitali za kanda nchi nzima, alifuta ada ya shule za sekondari completely, alisogeza karibu huduma za afya, alijenga shule na hospitali za kutosha halafu hayo yote aliyafanya bila kutoza watu tozo, chakula bei unga kilo shilingi 800, mchele kilo shilingi 800 tena super, nyama kilo elfu 5, bando la data gb moja elfu 1, hakukua na njaa wala ukame, umeme uliwaka miaka yote, maji yalipatikana miaka yote.

Magufuli aliwakoa watanzania wasife njaa wakati wa kipindi cha covid akazuia njia za kitaahira za lockdown kutumika Tanzania ambapo baadae ilikuja kuthibitika kwamba Lockdown haikua njia sahihi, ni njia za kibwege kwani hazikuzuia covid. Magufuli hakutaka watanzania wafe kwa njaa kwa kukaa ndani.

Mashoga yalitaka afungie watu ndani wafe kwa njaa kisha waseme amefungia watu wamekufa.

Stori nyingine kuhusu Magufuli ni stori za kutaahira tu zitapuuzwa kadri ya muda. Always ukweli huja baadae.
 
Inahitaji kujitoa ufahamu kumuamini mwanasiasa
 
Kwa wanasiasa na mafisadi.

Wanaoonja joto ya jiwe sasa ni wananchi wa kawaida.
 
Back
Top Bottom