Mbulu kunani? Kwanini barabara ya Kilomita 75 kutoka Karatu- Mbulu ujenzi hauanzi?

Mbulu kunani? Kwanini barabara ya Kilomita 75 kutoka Karatu- Mbulu ujenzi hauanzi?

saigilomagema

JF-Expert Member
Joined
Jun 5, 2015
Posts
4,683
Reaction score
7,222
Wilaya ya Mbulu ilianzishwa mwaka 1905 wakati huo mfumo wa utawala ukiwa wa majimbo na wilaya. Mbulu ilikuwa mojawapo ya wilaya 2 ktk iliyokuwa jimbo la kaskazini iliyokuwa na wilaya za Arusha na Mbulu yenyewe.

Wilaya ya Mbulu ni mojawapo ya wilaya zilizo ktk maeneo yenye rutuba kubwa. Wilaya ya Mbulu ya wakati ule leo imegawanyika ktk wilaya za Hanang, Babati, Karatu na Mbulu yenyewe. Ingekuwa uzazi Mbulu leo ni babu lakini je ni kwa bahati mbaya makao makuu ya wilaya ya Mbulu mpaka leo hayajafikiwa na barabara ya lami?

Wilaya zilizozaliwa kutoka wilaya ya Mbulu makao makuu yao yameshafikiwa na barabara za lami muda mrefu. Mi nauliza Mbulu kuna nini mbona imepuuzwa hivi? Mh. Rais mwogopeni Mungu mnashindwa kweli kuwajengea hao wananchi Km 75 tu wakati mnajenga miradi ya mamia ya kilometa?

Ujenzi wa barabara ya Mnivata-Tandahimba-Newala-Masasi wa zaidi ya Km 160 umeshaanza. Mkataba wa ujenzi wa barabara tajwa ulisainiwa baada ya ule wa Karatu-Mbulu uliosainiwa tarehe 16.06.2023 lakini hakuna dalili ya kuanza ujenzi.

Jamani Mbulu kuna nini?
 
Mtindo uliopo sasa hivi ni kuwaambia raia bejeti imeshatengwa, kuzindua tu na kutangaza miradi ya barabara halafu wanaanza ujenzi miaka mingi mbeleni na wanajenga miaka mingi
 
Pesa hazipo,Kwa mujibu wa Bunge Bajeti iliyopangwa 90% inaishia kulipa madeni ya TanRoads.

Hata hivyo wataanza Kwa zuga ya Kisiasa ila kukamilika itakuwa majaaliwa.

TanRoads Kwa Sasa wame focus kwenye miradi inayoendelea kuliko kuanza mipya wakati pesa za kulipa hazipo.

Hadi uchaguzi ukipita ndipo Wizara zitapata pesa ila Kwa Sasa Nguvu yote Iko kwenye uchaguzi
 
Pesa hazipo,Kwa mujibu wa Bunge Bajeti iliyopangwa 90% inaishia kulipa madeni ya TanRoads.

Hata hivyo wataanza Kwa zuga ya Kisiasa ila kukamilika itakuwa majaaliwa.

TanRoads Kwa Sasa wame focus kwenye miradi inayoendelea kuliko kuanza mipya wakati pesa za kulipa hazipo.

Hadi uchaguzi ukipita ndipo Wizara zitapata pesa ila Kwa Sasa Nguvu yote Iko kwenye uchaguzi
Uchaguzi una bajeti kiasi gani ya kukwamisha barabara kujengwa??
 
Uchaguzi una bajeti kiasi gani ya kukwamisha barabara kujengwa??
Zaidi ya Bilioni 600.Sio kwamba zimekwamia Bali Barabara Mpya hapana focus Iko kwenye Barabara ambazo tayari zinaendelea na ujenzi na kulipa madeni ya zamani
 
Wambulu waendelee kutukirimu tu yale mambo yetu lakini mambo ya lami wasahau nakumbuka yule mbunge wao alipiga summer sort bungeni kisa anadai lami imagine toka enzi ya magufuli mpaka leo hakuna kitu
 

Attachments

  • 20240701_183456.jpg
    20240701_183456.jpg
    50.5 KB · Views: 7
Kuna transect kutoka Babati via Kiru valley Murray Mbulu ni bonge la shortcut hiyo ingekuwa lami longtime....shida ya wa Iraqw ni imani za Kishirikina kuogopa vifo Baliseh Wazee hawataki kitu kinaitwa lami....kuna ujenzi ulianza lami ndandi kwa ndani Mbulu Dongombesh daah ni nyasi tu na Mkandarasi kasepa....yaani wao ni bora wapite Magara kule kwenye makona makali ya kutumbukia huko makorongoni kuliko shortcut itengenezwe .bulu Babati via Murray and Kiru

Hawa waacheni waacheni wanasiri yao kutoka huko Ethiopia kwa kina Yuda Masay Akonay Nadee

Lami ipite Dareda Bashineti Dongobesh mpaka Haydom ila sio Gera Gwang Imboru
 
Kuna transect kutoka Babati via Kiru valley Murray Mbulu ni bonge la shortcut hiyo ingekuwa lami longtime....shida ya wa Iraqw ni imani za Kishirikina kuogopa vifo Baliseh Wazee hawataki kitu kinaitwa lami....kuna ujenzi ulianza lami ndandi kwa ndani Mbulu Dongombesh daah ni nyasi tu na Mkandarasi kasepa....yaani wao ni bora wapite Magara kule kwenye makona makali ya kutumbukia huko makorongoni kuliko shortcut itengenezwe .bulu Babati via Murray and Kiru

Hawa waacheni waacheni wanasiri yao kutoka huko Ethiopia kwa kina Yuda Masay Akonay Nadee

Lami ipite Dareda Bashineti Dongobesh mpaka Haydom ila sio Gera Gwang Imboru
Ile ya Haydom mpaka katesh inajengwa maana ni binge la short cut la simiyu
 
Barabara kuu ya kutoka Arusha kwenda Moshi,ni mashimo na viraka mwanzo mwisho.

Mitano Tena Kwa bibi
 
Labda wabunge wenu,Mbulu rural na wa Mbulu mjini wavue nguo sasa bungeni labda Serikali itawasikiliza..maana inaonekana Sarakasi hazijaleta tija
 
Waweke lami kutokea Mbuyu wa mjerumani mpk Mbulu mjini,zile kona pale Magara pia ni utalii tosha na pia ni karibu zaidi kutokea barabara kuu...
 
Bilioni 600 za nini wakati uchaguzi wa serikali za mitaa wanatumia ream paper tu kama wanafunzi??
Ona taifa la hovyo wanatumia pesa kibao kwa ajili ya uchaguzi ...Ttizo kubwa kuendesha domakrasio ndio kunaleta umaskini ...Bora kufuta uchaguzi na vyama vyote .
 
Back
Top Bottom