Fundi Mchundo
Platinum Member
- Nov 9, 2007
- 10,448
- 8,705
Tangu CHADEMA wameanza kampeni zao za Chadema digitali hadi ya Katiba Mpya huyu Mheshimiwa sijamsikia. Viongozi na wanachama wenzake wanawekwa ndani lakini yuko kimya.
Mwenyekiti wake anafunguliwa mashtaka ya ugaidi bado yuko kimya. Lakini wakati haya yanaendelea anafungua mashindano ya Aida Cup akiwa pamoja na Mkuu wa Wilaya Mheshimiwa Lijualikali.
Kwa mawazo yangu ni bora angetangaza kujitoa kwenye chama chake ili aweze kuwatumikia vizuri wananchi wa Nkasi ambao alisema walimchagua yeye na sio chama chake.
Baada ya kujitoa ajiunge na chama tawala ambacho bila shaka kitampa nafasi ya kugombea kiti hicho katika uchaguzi maalum utakaofuta.
Kwa vile chama cha awali hakitagombea (hata kingegombea) bila shaka atashinda na ataweza kuwawakilisha watu wa jimbo lake bila nafsi yake kumsuta. Kama ataona aibu kufanya hivyo, chama chake, kwa heshima na taadhima kichukue kadi yao ili awe huru.
Hivyo hivyo kwa madiwani wanaokiwakilisha chama hicho katika maeneo yao.
Amandla..
Mwenyekiti wake anafunguliwa mashtaka ya ugaidi bado yuko kimya. Lakini wakati haya yanaendelea anafungua mashindano ya Aida Cup akiwa pamoja na Mkuu wa Wilaya Mheshimiwa Lijualikali.
Kwa mawazo yangu ni bora angetangaza kujitoa kwenye chama chake ili aweze kuwatumikia vizuri wananchi wa Nkasi ambao alisema walimchagua yeye na sio chama chake.
Baada ya kujitoa ajiunge na chama tawala ambacho bila shaka kitampa nafasi ya kugombea kiti hicho katika uchaguzi maalum utakaofuta.
Kwa vile chama cha awali hakitagombea (hata kingegombea) bila shaka atashinda na ataweza kuwawakilisha watu wa jimbo lake bila nafsi yake kumsuta. Kama ataona aibu kufanya hivyo, chama chake, kwa heshima na taadhima kichukue kadi yao ili awe huru.
Hivyo hivyo kwa madiwani wanaokiwakilisha chama hicho katika maeneo yao.
Amandla..