Mbunge atamka Waadilifu lakini JK Rais wetu hayumo

mmmh simba akilowana hawi paka jamani, kama kundi la marafiki zako ni simba sizani kama we utakuwa ni ng'ombe...minachoamini anatulia timing ili atupige kisha arudi zake wawi akachokoe chaza.
 
Huyu Dr Shein ni mfano mwingine wa matumizi mabaya ya rasilimali za taifa letu. Ana elimu kubwa sana huyu jamaa, PhD katika molecular biology. Nchi zilizoendelea vichwa kama hivi ndio viliwekwa maabara vikazalisha haya maajabu mnayosikia ya GMO's, cloned organisms, genetic engineering nk. Kuna masikhara makubwa ya aina mbili nimesikia kuhusu Dr Shein, la kwanza nilisikia alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es salaam (Muhimbili pale) kusomea udaktari wa binadamu, lakini "wanoko" wa enzi hizo ambao nasikia bado wapo wakam-"disco" mwaka wa kwanza tu! Mwaka uliofuata ndio akapata scholarship akaenda nje ambako aliunga nondo juu ya nondo hadi aliporudi na hiyo PhD ya molecular biology. Masikhara ya aina ya pili ni kazi aliyopewa aliporudi, akaajiriwa kwenye Wizara ya Afya Zanzibar kama pathologist (ninavyojua pathologists ni watu kama Prof Shaba ambao huwa wanafanya uchunguzi wa maiti, postmortems na mambo kama hayo)! Baadaye akaingia kwenye tume ya kudhibiti UKIMWI Zanzibar. Yaani hakufanya kazi aliyosomea hata siku moja! Sasa najiuliza madude magumu namna hiyo aliyasoma ya nini, bora angejiunga tu huku kwenye "ungwini"! Baadae akaingia kwenye siasa na sasa ni makamu wa rais, na kina GT hapa wanamkejeli na mkasi, ati ndio kifaa chake cha kazi! Jamani, alikuwa "genius" huyu msimuone hivi na utulivu wake, ni "maakili" yamejazana kichwani humo yamekosa matumizi!
 
ccm sasa wameanza kuamka, muungwana wameshindwa kumuweka kwenye kundi la waadilifu ee....sawa sawa.
hata huyo pinda tuna wasi wasi nae kuwa hali iwapo itatulia kidogo tu atachota vijisenti vyake na yeye.
shein is a totale bore, kuiba ki hivyo hawezi, shy amemsema kuwa kawaachia wanawe wawe na uraia wa uingereza.....hao wanawe waloachiwa are they under 18?
 
Wewe Shy una uhakika gani kwamba huyu mbunge hana wanao muunga mkono?Ok sawa vyovyote vile lakini ujumbe umefika na sasa hivi huyo mjomba yako Ben anakosa usingizi,sasa nimegundua kuwa wewe ni mtu unae toka ktk jamii ya mafisadi
 
Wewe Shy una uhakika gani kwamba huyu mbunge hana wanao muunga mkono?Ok sawa vyovyote vile lakini ujumbe umefika na sasa hivi huyo mjomba yako Ben anakosa usingizi,sasa nimegundua kuwa wewe ni mtu unaetoka ktk jamii ya mafisadi
 


Na ndiyo maana kuna "kufaulu" na "kushindwa"
 
Hayo ni mawazo ya Mheshmiwa Mbunge na havimfanyi Muungwana kuwa fisadi.

Mimi naamini Muungwana ni safi!
 
huyu muungwana ni as msafi as they come.Tukumbuke tu kuwa JK alibambikiwa huyu na kina Mkapa ndio kabakishwa kupiga mikasi tu.Huyu akienda mikoani hufikia kwenye state lodges,hata Arusha yeye hufikia Ikulu ndogo wakati JK huwa Ngurdoto au kule mbugani kwa matajiri
 
Hayo ni mawazo ya Mheshmiwa Mbunge na havimfanyi Muungwana kuwa fisadi.

Mimi naamini Muungwana ni safi!

Muungwana ni msafi???? Msafi hawezi kukaa na waliochafuka muda wote na yeye asipakae matope.

Huenda sio mwizi kama akina Mkapa, lakini pia sio msafi.
 
Mimi naamini Muungwana ni safi!

Mkuu FD,

Heshima mbele, muungwana bado ni safi, lakini pia huwezi kufumbia macho the political fact hapa kwamba Lowassa, Msabaha, Karamagi, Mkapa, Yona, Chenge, marafiki zake wa karibu tena sana, ni proven mafisadi tena big time, unajua kuanzia Mwalimu mpaka Yesu hakuwa na marafiki kama hawa!
 
Hayo ni mawazo ya Mheshmiwa Mbunge na havimfanyi Muungwana kuwa fisadi.

Mimi naamini Muungwana ni safi!

We kizazi cha mafisadi, usafi wake uko wapi? acha upambe
 
Mi naomba mungu hiki kizazi cha wana-CCM wa sasa afanye replacement hakuna mwenye afadhari hao mnaoona wako kimya na kuwasifia nao wanatafunia ndani ya shuka wote wezi na ndio maana hakuna wa kumnyooshea kidole mwenzake...Sijui ni balaa gani limeikumba Tz???
 
Hata mimi binafsi namuona JK kama mtu safi. Ila wajibu wetu ni kuendelea kusimamia harakati zake zisipungue speed maana naye anabanwa sana na mafisadi hao.

Tusimkatishe sana tamaa, kwani katika awamu zote tatu zilizo mtangulia mimba za Mafisadi zilitungwa awamu ya kwanza wakati Azimio la Arusha linatungwa.

Awamu ya pili Mafisadi yakazaliwa kila limoja likawa na mchezo wa kwake, yakaanza chekechekea na kumaliza chuo kikuu.

Awamu ya tatu Mafisadi yameanza kazi katika Wizara na Idara mbalimbali. Hapo ndipo tulipoona ujanja wa panya kuuma na kupuliza. Tunachokiona sasa ni harakati za mafisadi yale yale toka awamu ya tatu.

Awamu ya nne mafisadi yanagombana baada ya kuzidiana mali ambapo sasa siri zinafichuka ni kama vile "cannibalism" ambayo huwakumba kuku na kuanza kuuwana wenyewe kwa kudonoana. Ila tushukuru kwamba mambo haya yametokea kwani kama si hali hii ya kuumbuana kwa viongozi hawa wala tusingejua kuna hali kama hiyo ya UFISADI. Mh Rais kuzitembelea wizara kuliibua baadhi ya mambo hadi yakaweza kuanza kuibuka kama tunavyoyaona.
 
Rais awe safi alafu achague au arithi viongozi wachafu?

Mwenyekiti wa chama cha kijani aliyeshindwa kuwafuta uanachama mafisadi wa richmond na EPA leo yeye ni safi?

Hainingii akilini
 
GT,

..muache Mzee wetu Sheikh Idiris Abdul Wakil Nombe.

..Yule Mzee alikuwa poa sana ila Wazanzibari watu wagumu mno.
 
Kadiri mkuu wa kaya anavyoendelea kuwakumbatia mafisadi tunafika sehemu tunaquestion uadirifu wake maana haiwezekani mawaziri wake, makatibu wakuu wake, gavana wote mafisadi wa hali ya juu halafu yeye hasiwachukulie hatua, hata kama anafuata sheria bado watu kama EL, RA Karamavi na wengine alitakiwa kukaa nao mbali maana ni majambazi wa nchi yetu.
 
Kwa hiyo hata speaker wa bunge letu ni mchafu?
 

Khe!! Shy shy wee!!!. Kuna kitu kinaitwa HAKI ZA BINAADAMU. Hivyo wewe unataraji huyo Mzee awazuwie Haki zao za Kibinaadamu watoto wake ambao wameshapindukia umri wa miaka 21. Uko sayari gani wewe-Shy shy (au ndio unaona haya)?
 
Haya mtasema yote.Viongozi wote ni waadilifu.Waacha wale.Mungu awape nini.
 

Hapa Shy nakuomba utoe vigezo utetee hoja yako hii.

Useme ana watoto wangapi na wepi wana uraia wa UK.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…