Pre GE2025 Mbunge Atupele Mwakibete Achangia Tsh. Milioni 15 Ujenzi Nyumba ya Mwalimu Busokelo Boys

Pre GE2025 Mbunge Atupele Mwakibete Achangia Tsh. Milioni 15 Ujenzi Nyumba ya Mwalimu Busokelo Boys

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

WhatsApp Image 2024-10-10 at 16.38.14.jpeg

Mbunge wa Jimbo la Busokelo, Mhe. Atupele Fredy Mwakibete leo Tarehe 10/10/2024 ameunga mkono jitihada za Wazazi na Wananchi katika Ujenzi wa Nyumba ya Mwalimu shule ya Sekondari ya Wavulana Busokelo inayopatikana kata ya Isange kwa Kuchangia pesa Shilingi Milioni 15.

Akiwa katika Mahafali ya pili ya kidato cha Nne kama Mgeni Rasmi, Mhe. Atupele Fredy Mwakibete ameongoza zoezi la changizo kwa wazazi kupitia keki ambapo zaidi ya shilingi Laki Tano zimepatikana.

WhatsApp Image 2024-10-10 at 16.38.20(2).jpeg

Aidha, Mhe. Atupele Fredy Mwakibete amesema changamoto zilizotolewa kwenye Taarifa ya Shule ikiwemo ya ukosefu wa Nyumba za walimu jitihada zimeanza kupitia wazazi na yeye kuunga mkono,pia barabara ya kuingia shuleni itarekebishwa na mitambo ya ofisi ya mbunge, suala la maji Mamlaka husika inafanyia kazi pamoja na bwalo la chakula watashauriana na madiwani ili waanze kwa mapato ya ndani lakini kuhusu jengo la Utawala atawasiliana na Waziri wa TAMISEMI ili kupeleka maombi rasmi.

Pia, Mhe. Atupele Fredy Mwakibete ametoa changamoto kwa Mwanafunzi atakayefaulu kwa Daraja la Kwanza (Div 1.7) basi atampatia zawadi ya pesa Shilingi Milioni Moja na Kwa waalimu watakaofaulisha masomo kwa Daraja A watapata zawadi ya Shilingi Laki Moja kwa Kila Somo.

WhatsApp Image 2024-10-10 at 16.38.20(1).jpeg
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2024-10-10 at 16.38.19.jpeg
    WhatsApp Image 2024-10-10 at 16.38.19.jpeg
    294.2 KB · Views: 3
  • WhatsApp Image 2024-10-10 at 16.38.20.jpeg
    WhatsApp Image 2024-10-10 at 16.38.20.jpeg
    429.5 KB · Views: 2
Kumbe wabunge wanapesa.... connection jamani I swear sitowaangusha😊
 
Back
Top Bottom