Mbunge CCM atoa nguo ya ndani mkutanoni

Mbunge CCM atoa nguo ya ndani mkutanoni

Shadow

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2008
Posts
2,897
Reaction score
675
Hivi tunakwenda wapi sasa? What a dumbest way of protest!

12/20/2008 4:11:56 AM
KATIKA hali inayoashiria kukua kwa uhasama miongoni mwa viongozi wa chama cha Mapinduzi Mkoani Mbeya, Mbunge mmoja wa viti maalumu anadaiwa kumdhalilisha kiongozi mwenzake kwa kutaka kumvisha nguo yake ya ndani wakati wa kikao cha kamati ya siasa
Taarifa za ndani za kikao zinadai kuwa mbunge huyo alifanya kituko hicho katika kikao cha Desemba 17,mwaka huu, kwa kutoa nguo za ndani kutoka kwenye mkoba wake wa mkononi na kuwanyooshea wajumbe wa kikao hicho.

Vyanzo vya habari kutoka ndani ya kikao hicho vinadai kuwa mbunge huyo alikuwa akimtuhumu mwenyekiti wa moja ya jumuiya za CCM kwamba anapiga vita harakati zake za kuwania uongozi katika chama hicho.

"Wakati akimtuhumu mwenyekiti wa huyo wa moja ya jumuiya za chama hicho ndipo kwa mshangao alitoa nguo hiyo ya ndani kutoka katika pochi yake na kutaka kumvisha mwenyekiti mwenzake huyo ambaye ni mwanaume"

Habari zaidi zinadai mwenyekiti huyo ya jumuiya ambaye ni mgeni katika kikao hicho alichukizwa na kitendo hicho hivyo kuja juu baada ya kuona anadhalilishwa.

Hata hivyo kabla hajachukua hatua zaidi mwenyekiti wa CCM mkoani humo, Nawab Mulla aliingilia kati na kwa kutumia busara alimuonya mbunge huyo kwa kitendo chake kisicho cha maadaili kwa chama hicho.

Mulla alimtaka mbunge huyo kumuomba radhi mwenyekiti aliyemdhalilisha hali iliyomshawishi aliyedhaliliwa kutuliza jazba.

Baadhi ya wajumbe waliokuwa katika kikao hicho ambaye hawakupenda kutajwa majina yao walisema mbunge huyo alikuwa anaheshimiwa sana mkoani humo, alijivunjia heshima mbele ya wajumbe wa kikao hicho ambao baadhi ni sawa na wajukuu zake" alisema
Source: Nifahamishe
 
Tabia mbaya sana hii. Mbunge huyu lazima alikuwa ni mwanamke; kitendo cha kukimbilia kutoa chupi yake kinaonyesha jinsi alivyo mwepesi kutoa chupi zake na huenda aliukwaa ubunge kwa kutoa chupi yake vivyo hivyo.
 
Yote hiyo ni hasira ya kuona ama kuhisi anataka kuzuiliwa kwa analopanga kulipatan kupitia uongozi. Mtavua Pupi mpaka mlizovaa kuonesha hasira. Na hiyo ni ndani ya chama, subirini hasira zetu wananchi.
 
Hii ya kutoa chupi mbele ya kadamnasi ya watu imenikumbusha enzi za mtunzi marehemu John Rutayasingwa kwenye moja ya Riwaya zake, zile simulizi za mheshimiwa Bayeke aliyependa sana 'Blanketi chapa mtu', kwenye moja ya mikutano ya hadhara
Alitoa chupi ya kike na kuikung'uta kung'uta huku akifikiria ni anjifu.Umati wa mkutano walimcheka kwa mshangao.

Tofauti ya Mhe. Bayeke na hiki kituko cha CCM ni kuwa Bayeke alitoa chupi kwa bahati mbaya bila kukusudia wakati Mhe wa CCM alidhamiria.
 
Nionavyo mimi mama huyo alikusudia kutoa hiyo chupi kwenye huo mkutano,mara nyingi wanawake hutembea na kanga kwenye mkoba.mama huyo siyo mstaarabu kabisa . Hekima ya mtu hupimwa kwa jinsi anavyofanya maamuzi.hivyo sidhani kama huyo 'viti maalumu' ni mama mwenye maadili.Hivi ninyi mnaowachagua mnaangalia vigezo gani?Angekuwa ameitoa Dodoma ingekuwa aibu kubwa.Ushauri wangu apigwe chini kila mahali,kwani amedhalilisha waheshimiwa wetu
 
Madaraka ni matamu mno huko ccm, kila mmoja anakazana kuwa kiongozi wakidhani kuna pesa zingine za kificho ziko ple bot ili 2010 wakagawane
 
Kama viongozi ni hao halafu tunashangaa kwanini mkoa hauendelei?
 
Labda lengo lake lilikuwa kumwaga radhi........................
Na bado sio chupi tuu,tutaona vingi next year na mwaka wa uchaguzi
 
Huyo mbunge aliyefanya kitendo hicho hana jina?

Kati ya wabunge wa viti maalum Mbeya kuna Hilda Ngoye na Florence Kyendesya.
 
Huyu mwanamke laana tuullah kabisa .Yaani chupi ? Huyu ameolewa ama ?
 
Kila mtu hapa ame assume huyu mama alitoa chupi. Huenda alitoa Sindiria. Kumvisha mwanaume chupi inaweza kuwa kazi kubwa.

Yote yote bado ni utovu wa nidhamu na maadili wa hali ya juu. TZ kungekuwa na kuwajibika, hata huo ubunge angepoteza.

Hivi Mbeya ina wabunge wangapi wanawake? Inabidi tupate jina lake huyu mama.
 
Kila mtu hapa ame assume huyu mama alitoa chupi. Huenda alitoa Sindiria. Kumvisha mwanaume chupi inaweza kuwa kazi kubwa.

Yote yote bado ni utovu wa nidhamu na maadili wa hali ya juu. TZ kungekuwa na kuwajibika, hata huo ubunge angepoteza.

Hivi Mbeya ina wabunge wangapi wanawake? Inabidi tupate jina lake huyu mama.

😱

...huenda pia ikawa ni shumizi 😀

kamdhalilisha sana mskini 🙁, kwetu pwani 'amemaanisha' huyo baba ana mambo ya ki 'shoga-shoga!'
 
Kwa mujibu wa taarifa alitoa sidiria, ila vyote sawa tu chupi sidiria, shimizi. Hawa ndio wanajiita empowered women! gggggggggggggggrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrhhhhhhh!
 
Kwa jinsi yeyote na sababu yeyote ile, mhusika hana sababu kujishushia heshima kiasi hiki.Inaonyesha pia jinsi tulivyo na viongozi mufilisi wa akili.Hoja hupingwa na hoja na siyo kutoleana nguo za ndani ili uwe ume make a point.Mwanamke huyu hawakilishi wanawake wenzie bali anajiwakilisha mwenyewe kwa mbinu zake chafu.Kama walivyosema wengine hapo juu, huyu hastahili heshima maana hana heshima na hastahili kumwongoza mtu yeyote maadam kashindwa kujiongoza mwenyewe!
 
Nionavyo mimi mama huyo alikusudia kutoa hiyo chupi kwenye huo mkutano,mara nyingi wanawake hutembea na kanga kwenye mkoba.mama huyo siyo mstaarabu kabisa . Hekima ya mtu hupimwa kwa jinsi anavyofanya maamuzi.hivyo sidhani kama huyo 'viti maalumu' ni mama mwenye maadili.Hivi ninyi mnaowachagua mnaangalia vigezo gani?Angekuwa ameitoa Dodoma ingekuwa aibu kubwa.Ushauri wangu apigwe chini kila mahali,kwani amedhalilisha waheshimiwa wetu

Je kuna haja ya kuvivuta hivi viti maalumu manake criteria ya kuchaguliwa kwake huwa ni ya ajabu ajabu
 
Kwa jinsi yeyote na sababu yeyote ile, mhusika hana sababu kujishushia heshima kiasi hiki.Inaonyesha pia jinsi tulivyo na viongozi mufilisi wa akili.Hoja hupingwa na hoja na siyo kutoleana nguo za ndani ili uwe ume make a point.Mwanamke huyu hawakilishi wanawake wenzie bali anajiwakilisha mwenyewe kwa mbinu zake chafu.Kama walivyosema wengine hapo juu, huyu hastahili heshima maana hana heshima na hastahili kumwongoza mtu yeyote maadam kashindwa kujiongoza mwenyewe!

WS, ni vigezo vipi utumika kuwapata hawa wawakilishi wa viti maalumu? kwa nini isiwe wananchi kuwapigia wakina mama kuingia kwenye buge kama tunavyowapigia wabunge wa kawaida? Wananchi wanawajua vizuri kuliko kuwekewa mtu aliyechaguliwa na kundi dogo kwenye closed door. Mtakuja kutuletea hata mapsycho huko bungeni!
 
Back
Top Bottom