Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 2,833
- 1,301
Mbunge Dkt. Christina Mnzava Atembelea Kituo cha Afya cha Ushetu, Kahama
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Dkt. Christina Mnzava ametembelea Kituo cha Afya cha Ushetu, Kahama-Shinyanga na kukagua utekelezaji wa Ilani katika Kituo cha Afya Ushetu.
Vilevile, Mhe. Dkt. Christina Mnzava akiwa Kituo cha Afya Ushetu Ametoa msaada wa Mashuka katika wodi ya wanawake na watoto. Pia, Ametoa vifaa vya michezo Shule ya Sekondari MWELI na ameahidi kuwapatia magodoro watoto wa kike wanaoishi katika mazingira magumu ambao wanasoma katika Shule ya Sekondari Mweli.
Aidha, Mhe. Dkt. Christina Mnzava alihutubia mkutano mkubwa wa hadhara kwa kusikiliza kero za wananchi na kuzipatia majibu kwani Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alitoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa wodi mbili na jango la upasuaji katika kituo hiki hivyo wananchi walimpongeza sana kwa juhudi anazozifanya hali iliyopelekea kuvuna wanachama wapya wa ccm 300 (mia tatu)!