Mbunge Ezra Chiwelesa Achaguliwa Kuwa Rais wa Moja ya Kamati Bunge la Maziwa Makuu

Mbunge Ezra Chiwelesa Achaguliwa Kuwa Rais wa Moja ya Kamati Bunge la Maziwa Makuu

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

MBUNGE MHE. EZRA CHIWELESA ACHAGULIWA KUWA RAIS WA MOJA YA KAMATI BUNGE LA MAZIWA MAKUU.

Tarehe 27 Machi, 2023 umefanyika uchaguzi wa viongozi mbalimbali wa Kamati za Kudumu za Bunge la Nchi za Maziwa Makuu Jijini Juba Sudani Kusini.

Katika uchaguzi huo Mbunge wa Jimbo la Biharamulo Magharibi na kiongozi wa msafara wa Wabunge kutoka Tanzania Mhe. Eng. Ezra Chiwelesa amechaguliwa kuwa Rais wa kamati ya kudumu ya masuala ya kibinadamu na kijamii (Humanitarian and Social Issues).

Aidha, Jamhuri ya Afrika ya Kati wamechaguliwa kuwa Makamu wa Rais na Burundi wakichaguliwa kwenye nafasi ya katibu wa kamati.

Kuchaguliwa kwa Mhe. Ezra Chiwelesa kutoka Bunge la Tanzania kunadhihirisha kuaminika kwa Tanzania kimataifa hali iliyosababishwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ameimarisha masuala ya kidiplomasia.

WhatsApp Image 2023-03-28 at 13.40.07.jpeg
WhatsApp Image 2023-03-28 at 13.40.07(1).jpeg
WhatsApp Image 2023-03-28 at 13.40.08.jpeg
WhatsApp Image 2023-03-28 at 13.40.08(1).jpeg
 
Back
Top Bottom