Mbunge huyu Msukuma!

Mbunge huyu Msukuma!

Sijali

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2010
Posts
2,672
Reaction score
1,814
Ni dhahiri kabisa, kutokana na michango yake bungeni, mbunge Msukuma anawashinda wengi kwa maono na ubunifu.

Amekuwa consistent kutoa maoni yenye mashiko, yaliyofanyiwa utafiti na hata kuthubutu kuonesha tija ya maoni yake endapo yatatumika. Hizi kwa kawaida ni sifa za mtu aliyebobea katika 'usomi'.

Ila kitu ninachohitalifiana naye ni ile ada yake ya mara kwa mara ya kuwabehua wasomi; kiasi kwamba ameanza kuwaaminisha vijana wavivu kuwa kusoma 'si lazima' na kwamba mtu anaweza kufika mbali kwa ujanja ujanja tu, bila ya kusoma!

Rai hii imeanza kushika mizizi sana baina ya makundi ya vijana Tanzania. Vijana wengi ninaozungumza nao wanaamini kuwa elimu si muhimu kwa mafanikio.

Sisemi kuwa Msukuma pekee ndiye anayehusika na hili, lakini nahofia kiasi anavyoendelea kulishabikia hilo, tena kutoka kilele cha taasisi ya uongozi, kitazidisha hisia hiyo.

Ukweli ni kuwa elimu ni muhimu sana kwa maendeleo ya mtu binafsi na taifa, na bila ya elimu si mtu wala taifa litafika popote.

Hii si kusema hakutakuwepo watu wachache, kama bwana Msukuma, ambao watakuwa na talanta au kipawa cha maarifa nje ya mfumo wa elimu. Lakini hii ni 'phenomenon' si sheria. Kosa ni kuifanya hii ni sheria na si 'phenomenon'.

Aidha, hao 'wasomi' ambao bwana Msukuma anawabehua, kwa kweli wengi wao hawakuelimika. Kuna tofauti kubwa baina ya 'kwenda Shule' na kuelimika. 'Usomi' au kuelimika kunaweza kutokea bila ya kwenda shule.

Wengi wanaoitwa 'wasomi' hapa Tanzania, kwa kweli wamekwenda shule tu, hawakuelimika!
 
Ni dhahiri kabisa, kutokana na michango yake bungeni, mbunge Msukuma anawashinda wengi kwa maono na ubunifu.

Amekuwa consistent kutoa maoni yenye mashiko, yaliyofanyiwa utafiti na hata kuthubutu kuonesha tija ya maoni yake endapo yatatumika. Hizi kwa kawaida ni sifa za mtu aliyebobea katika 'usomi'.

Ila kitu ninachohitalifiana naye ni ile ada yake ya mara kwa mara ya kuwabehua wasomi; kiasi kwamba ameanza kuwaaminisha vijana wavivu kuwa kusoma 'si lazima' na kwamba mtu anaweza kufika mbali kwa ujanja ujanja tu, bila ya kusoma!

Rai hii imeanza kushika mizizi sana baina ya makundi ya vijana Tanzania. Vijana wengi ninaozungumza nao wanaamini kuwa elimu si muhimu kwa mafanikio.

Sisemi kuwa Msukuma pekee ndiye anayehusika na hili, lakini nahofia kiasi anavyoendelea kulishabikia hilo, tena kutoka kilele cha taasisi ya uongozi, kitazidisha hisia hiyo.

Ukweli ni kuwa elimu ni muhimu sana kwa maendeleo ya mtu binafsi na taifa, na bila ya elimu si mtu wala taifa litafika popote.

Hii si kusema hakutakuwepo watu wachache, kama bwana Msukuma, ambao watakuwa na talanta au kipawa cha maarifa nje ya mfumo wa elimu. Lakini hii ni 'phenomenon' si sheria. Kosa ni kuifanya hii ni sheria na si 'phenomenon'.

Aidha, hao 'wasomi' ambao bwana Msukuma anawabehua, kwa kweli wengi wao hawakuelimika. Kuna tofauti kubwa baina ya 'kwenda Shule' na kuelimika. 'Usomi' au kuelimika kunaweza kutokea bila ya kwenda shule.

Wengi wanaoitwa 'wasomi' hapa Tanzania, kwa kweli wamekwenda shule tu, hawakuelimika!
Kazi ya elimu Tanzania ni kukusaidia kupata nafasi ya kazi yenye fursa y a wizi mkubwa ili kupata maendeleo kwa urahisi.

Asilimia kubwa ya wasomi Tanzania sio kwamba wametumia akili zao kupata pesa kihalali bali fursa walizopewa kwenye mamlaka kufanikisha wizi mkubwa serikalini na utapeli kama Rifaro Africa na Kalynda.
Ukiniambia hivi nitakubaliana nawe,kuwa vijana wasome ili watafute fursa za kuiba serikalini.
Kinyume na hapo wasomi wetu hawana jipya lolote.
Elimu ni mfumo wa kifree mason kutengenezeana connection za kuumiza wasio na nguvu
 
Back
Top Bottom