beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,880
- 6,368
Mbunge wa Jimbo la Lupembe, Edwin Swale amesema Bajeti wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi imeanza vibaya na haina matumaini kwa Watanzania wengi, Wabunge wote wanalalamika na Waziri naye amekata tamaa.
Amesema Wananchi wa Lupembe wamekuwa wakifurika kwenye Kampeni na kushangilia ujio wa barabara ya Kibena mpaka Madeke na mwaka 2020 Wizara iliitengea Bilioni 5.9, lakini leo Wizara hiyo hiyo imepunguza fedha hadi Bilioni 2.
Ameongeza, "Waziri nisaidie kujua nini kimekusibu kuipunguza kutoka Bilioni 5 mpaka 2? Wananchi wa Lupembe tumekosa nini? Fedha hii umeiondoa umepeleka wapi na kwanini?"
Amesema Wananchi wa Lupembe wamekuwa wakifurika kwenye Kampeni na kushangilia ujio wa barabara ya Kibena mpaka Madeke na mwaka 2020 Wizara iliitengea Bilioni 5.9, lakini leo Wizara hiyo hiyo imepunguza fedha hadi Bilioni 2.
Ameongeza, "Waziri nisaidie kujua nini kimekusibu kuipunguza kutoka Bilioni 5 mpaka 2? Wananchi wa Lupembe tumekosa nini? Fedha hii umeiondoa umepeleka wapi na kwanini?"