Mbunge Josephat Gwajima na genge lako, Tubuni dhambi ya uongo labda Mungu atawasamehe

Mbunge Josephat Gwajima na genge lako, Tubuni dhambi ya uongo labda Mungu atawasamehe

stonecutter

JF-Expert Member
Joined
Jun 12, 2022
Posts
1,724
Reaction score
2,584
Salam wakuu.

Niende kwenye mada. Katika kuzunguka huku na kule ndani ya nchi ktk kutimiza majukumu yangu, mwishoni mwa juma lililopita nilikuwa kusini mwa nchi. Mkoani Ruvuma, wilaya moja ya Nyasa ambayo makao yake makuu ni Mbamba Bay.

Sasa, kwa siku mbili mfululizo yaani Alhamisi na Ijumaa, kulikuwa na matangazo khs mkutano wa siku moja wa Gwajima siku ya Jumamosi. Matangazo ya mkutano yalieleza wazi kwamba, kutakuwa na kutoa misukule, yaani watu waliokufa kishirikina ndani ya ziwa Nyasa au penginepo.

Matangazo yalisema wazi kuwa, wale waliofiwa na wapendwa wao waje na picha zao na kuandika majina matatu ya aliyekufa. Wakuu, kule kusini dhana ya uchawi na watu kufa vifo vya utata wenyeji walisema imeshamiri sana.

Hivyo Gwajima alisubiriwa kwa shauku kubwa watu wakiwa na picha za wapendwa wao. Siku ikawadia, Gwajima akaanza kazi. Baada ya mahubiri machache akaanza kuita misukule, njoooo, njooo, hadi mwisho, hakuna hata msukule uliofika pale. Wenyeji wamelaumu udanganyifu uliofanyika. Gwajima hii dhambi tubuni.
 
Usipanic, wewe endelea kutunza picha za mpendwa wako. Hivi tangu umemfahamu na hizo harakati zake umeshawahi kuona ametoa misukue wangapi?
 
Usipanic, wewe endelea kutunza picha za mpendwa wako. Hivi tangu umemfahamu na hizo harakati zake umeshawahi kuona ametoa misukue wangapi?
Mkuu, asante kwa mchango wako. Jibu la swali lako pia SIJAWAHI KUONA MISUKULE ALIYOITOA. Nakumbuka wakati anaanza kuvuma hapa DAR miaka ile kama skosei 2006- alisema atamfufua AMINA CHIFUPA, hadi leo kimya.
 
Gwajima ni mpumbavu kama walivyo sukuma gang na UVCCM huwa anawahadaa wapumbavu wenzake, kama anaweza kufufua misukule kwanini alishindwa kumfufua dikiteta aliyekufa kichawi na sasa analimishwa jehanamu.
Duuuuh! mbwa mwitu aliyejivika ngozi ya kondoo.
 
Nilishangaa Sana wananchi wa Kawe kumpa kura kama mbunge wao.
Sera zenyewe eti atawapeleka Barmigiham marekani
 
Gwajima ni mpumbavu kama walivyo sukuma gang na UVCCM huwa anawahadaa wapumbavu wenzake, kama anaweza kufufua misukule kwanini alishindwa kumfufua dikiteta aliyekufa kichawi na sasa analimishwa jehanamu.
Kwanini unasema kichawi Mkuu
 
Nilishangaa Sana wananchi wa Kawe kumpa kura kama mbunge wao.
Sera zenyewe eti atawapeleka Barmigiham marekani
Kura za askofu hazikutoshea kwenye uchaguzi wa chama akabebwa na Jiwe. Kuja kwa wananchi pia akashindwa na Halima. Lakini kutokana na agano la askofu na jiwe basi, jiwe akambeba askofu. Na askofu akakubali kutenda dhambi. Na khs hizo ahadi za kuwapeleka huko, basi kumbe ni mzoefu wa kudanganya.
 
Back
Top Bottom