MTANZANIA620
Member
- Jun 20, 2023
- 65
- 81
Katika kuhakikisha hilo jana tarehe 30 Agosti, 2024 ametekeleza ahadi yake ya shilingi milioni tano yenye lengo la kuwaunga mkono waumini wa imani ya Kiislamu Msikiti mkuu wa Taqwa BAKWATA kata ya Kahe walioamua kujenga vyumba viwili vya elimu ya awali pamoja Madrasa kwa kujitolea wao wenyewe kwa hali na mali pamoja na kushirikisha wadau mbalimbali.
Soma Pia: Kimei aendelea kuweka rekodi Vunjo
Uongozi wa msikiti huo pamoja na BAKWATA kata ya Kahe wamemshukuru Dkt Kimei kwa mchango wake na kumpongeza kwa kutowabagua wananchi anaowawakilisha kwa imani zao.
Dkt Kimei amewaomba viongozi wote wa dini kuendelea kuiombea Tanzania na kumuombea Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ili aendelee kuiongoza Nchi yetu katika usawa na haki.