Mbunge Kishimba atoa Onyo: Bodi ya Mikopo (HESLB) itafilisika ikiendelea kutoa fedha kwa Elimu Isiyoajirika, Bodi inazitupa hela kwa GPA isiyoajirika

Mbunge Kishimba atoa Onyo: Bodi ya Mikopo (HESLB) itafilisika ikiendelea kutoa fedha kwa Elimu Isiyoajirika, Bodi inazitupa hela kwa GPA isiyoajirika

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mbunge Jumanne Kishimba, ambaye ni mjumbe wa Kamati ya Elimu ya Juu, ametoa maoni yake Bungeni kuhusu hali ya mikopo ya elimu nchini. Maoni hayo yalikuja baada ya Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu (HESLB) kudai kushindwa kupata marejesho kutoka kwa waliokopa mikopo ya elimu na kutangaza kuandaa oparesheni ya kuwakamata wadaiwa wote. Kishimba alisisitiza kuwa Bodi ya Mikopo inapaswa kuwajibikaji zaidi katika kutoa mikopo kwa wanafunzi. "Bodi ya Elimu imempa mtu wa chuo hizo pesa, mtu wa chuo akampa Elimu mwanafunzi, elimu ambayo haiajiriki. Sasa anayetakiwa kushitakiwa ni nani? Ni mwanafunzi au ni Chuo?" alihoji Kishimba.

Pia, Soma: Bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu HESLB imetimiza miaka 20, je imekuwa msaada ipavyo kwa wanafunzi wasiokuwa na uwezo kufikia elimu ya juu?

Mbunge huyo aliongeza kuwa, kwa sasa, dunia inabadilika na kwamba hatuwezi kuendelea kutumia kauli za kale kama "Elimu ni Ufunguo wa Maisha," wakati wanafunzi wanapewa bidhaa ambayo hawana uwezo wa kuiuza. Aliiomba Bodi ya Mikopo kuongeza masharti kwa vyuo ili kuhimiza utoaji wa elimu inayohakikisha ajira kwa wahitimu. "Kama Bodi ya Mikopo inazitupa tu hela kwa mtu halafu anaenda kumfundisha GPA isiyoajirika, taasisi hii si itafilisika," alisisitiza.

Aidha, Kishimba alitoa wito kwa taasisi za elimu (Vyuo) kutafuta mitaala inayolenga kuwapa wanafunzi ujuzi unaohitajika kwenye soko la ajira, ili waweze kurejesha mikopo yao kwa ufanisi.
 
Mbunge Jumanne Kishimba, ambaye ni mjumbe wa Kamati ya Elimu ya Juu, ametoa maoni yake Bungeni kuhusu hali ya mikopo ya elimu nchini. Maoni hayo yalikuja baada ya Bodi ya Mikopo kudai kushindwa kupata marejesho kutoka kwa waliokopa mikopo ya elimu na kutangaza kuandaa oparesheni ya kuwakamata wadaiwa wote. Kishimba alisisitiza kuwa Bodi ya Mikopo inapaswa kuwajibikaji zaidi katika kutoa mikopo kwa wanafunzi. "Bodi ya Elimu imempa mtu wa chuo hizo pesa, mtu wa chuo akampa Elimu mwanafunzi, elimu ambayo haiajiriki. Sasa anayetakiwa kushitakiwa ni nani? Ni mwanafunzi au ni Chuo?" alihoji Kishimba.

Mbunge huyo aliongeza kuwa, kwa sasa, dunia inabadilika na kwamba hatuwezi kuendelea kutumia kauli za kale kama "Elimu ni Ufunguo wa Maisha," wakati wanafunzi wanapewa bidhaa ambayo hawana uwezo wa kuitumia. Aliiomba Bodi ya Mikopo kuongeza masharti kwa vyuo ili kuhimiza utoaji wa elimu inayohakikisha ajira kwa wahitimu. "Kama Bodi ya Mikopo inazitupa tu hela kwa mtu halafu anaenda kumfundisha GPA isiyoajirika, taasisi hii si itafilisika," alisisitiza.

Aidha, Kishimba alitoa wito kwa taasisi za elimu (Vyuo) kutafuta mitaala inayolenga kuwapa wanafunzi ujuzi unaohitajika kwenye soko la ajira, ili waweze kurejesha mikopo yao kwa ufanisi.
Sasa kama kuna elimu isio ajirika si ufutwe tabaki na hiyo inao ajirika kwa mjibu wake.
 
Ukweli ni kwamba vyuo vimejaa kozi za hovyo ambazo haziajiriki. Nenda SUA kuna kozi vichefuchefu watu wànasoma hazina application popote mtaani. Watu wànasoma sababu hela ni za mkopo na hakuna mtu hàta mmoja anayesoma hizo kozi kwa hela yake hata ukimwambia achangie 1ⁿ%
 
Tatizo mfumo wa elimu wa Tanzania hauendani na Dunia inavyotaka Mfano ukimchukua mwanafunzi aliyesoma Uganda na Tanzania Kwa elimu sawa halafu ikapatikana nafasi ya kazi Kwa kampuni ya marekani au ya kichina,mganda atapata haraka kuliko mtanzania.Hii nimejionea pale ccecc(kampuni ya kichina ya ujenzi)mtanzania anapata kazi ya saidia fundi lakini siyo zile za maana.Ndiyo maana kurudisha mikopo HESLB inakuwa ngumu
 
uM
Ukweli ni kwamba vyuo vimejaa kozi za hovyo ambazo haziajiriki. Nenda SUA kuna kozi vichefuchefu watu wànasoma hazina application popote mtaani. Watu wànasoma sababu hela ni za mkopo na hakuna mtu hàta mmoja anayesoma hizo kozi kwa hela yake hata ukimwambia achangie 1ⁿ%
Unaionea SUA bure kabisa, waliosoma kozi za vyuo vingine wanaajirika? Ulitaka vyuo vyote vifundishe kozi za nursing na medicine ambazo zimepata ajira hivi karibuni? Hujawa fair katika hoja hii.
 
Ukweli ni kwamba vyuo vimejaa kozi za hovyo ambazo haziajiriki. Nenda SUA kuna kozi vichefuchefu watu wànasoma hazina application popote mtaani. Watu wànasoma sababu hela ni za mkopo na hakuna mtu hàta mmoja anayesoma hizo kozi kwa hela yake hata ukimwambia achangie 1ⁿ%
Tatizo ni uchumi wetu kushindwa kutengeneza ajira za kutosha. Hayo mengine ni kubebesha vyuo mzigo wa lawama bila sababu.
 
Tatizo mfumo wa elimu wa Tanzania hauendani na Dunia inavyotaka Mfano ukimchukua mwanafunzi aliyesoma Uganda na Tanzania Kwa elimu sawa halafu ikapatikana nafasi ya kazi Kwa kampuni ya marekani au ya kichina,mganda atapata haraka kuliko mtanzania.Hii nimejionea pale ccecc(kampuni ya kichina ya ujenzi)mtanzania anapata kazi ya saidia fundi lakini siyo zile za maana
Hata sie watanzania wenyewe akili zetu haziko imara kabisa tunawaza kuiba kula rushwa na kupiga pesa kwa namna yoyote, hatujui kujenga personality au career.
 
Ye si katoa mfano tu, SUA imechukuliwa kama case study, ila hana maana ni SUA peke yake. Asilimia kubwa sana ya vyuo vina program za ajabu
 
Dunia inaend kasi sana, ila watu wengi akili ziko nyuma,
Unasomesha mtoto tena kwa kuuza mashamba alafu anarudi na vyeti tu kuomba mtaji tena 😮‍💨
 
Mbona hata madaktari hawaajiriwi, shida ni serikali haina mipango ya kutoa ajira kwa wahitimu
 
Mnalaumu vyuo.

Lakini mnajua kwamba hizo kozi siyo mkuu wa chuo na wahadhiri wanazitunga?

Hua zinatengenezwa kwa ushirikiano na wizara ya elimu. Changamoto ninayoihisi ni kwamba unakuta kozi ya chuo hiki na chuo kile zina modules zinafanana na in practice zinaendana ila wa chuo hiki ataajiriwa kwa hiyo kozi na mwingine ataambiwa kozi haitambuliki.

Mfano kuna kozi inaitwa Political Science and Public Administration kisha kuna kozi inaitwa Politics and Management of Social Development. Hizi kozi ni nearly identical ila utakuta wa hiyo ya kwanza anaajiriwa huyu wa pili anaambiwa kozi haijulikani.

Here is where it will get weird. Inservice atayesoma kozi yoyote kati ya hizo serikali itamtambua na itampa promotion, heslb itampa mkopo yoyote kati ya atayesoma kozi yoyote hapo.

Njoo kwenye kuajiriwa 😅😅😅

Now kwanini kozi za mtindo huo wasizivunje? Wakaamua tu kwamba kuanzia mwaka fulani kozi hii itaitwa hivi au vile n.k.
 
Mjumbe wa kamati ya elimu ya juu aliyeishia la saba
 
Mnalaumu vyuo.

Lakini mnajua kwamba hizo kozi siyo mkuu wa chuo na wahadhiri wanazitunga?

Hua zinatengenezwa kwa ushirikiano na wizara ya elimu. Changamoto ninayoihisi ni kwamba unakuta kozi ya chuo hiki na chuo kile zina modules zinafanana na in practice zinaendana ila wa chuo hiki ataajiriwa kwa hiyo kozi na mwingine ataambiwa kozi haitambuliki.

Mfano kuna kozi inaitwa Political Science and Public Administration kisha kuna kozi inaitwa Politics and Management of Social Development. Hizi kozi ni nearly identical ila utakuta wa hiyo ya kwanza anaajiriwa huyu wa pili anaambiwa kozi haijulikani.

Here is where it will get weird. Inservice atayesoma kozi yoyote kati ya hizo serikali itamtambua na itampa promotion, heslb itampa mkopo yoyote kati ya atayesoma kozi yoyote hapo.

Njoo kwenye kuajiriwa 😅😅😅

Now kwanini kozi za mtindo huo wasizivunje? Wakaamua tu kwamba kuanzia mwaka fulani kozi hii itaitwa hivi au vile n.k.
Ilishawahi kunikuta kwenye sahili mbili tofauti nikaambiwa kozi yangu haijulikani, wakapiga simu sehemu kisha wakaniruhusu niingie chumba cha usahili, Namshukuru Mungu kozi hiyo hiyo ndio ikaniptia ajira serikalini
 
Back
Top Bottom