Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 2,833
- 1,301
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Singida, Mhe. Martha Nehemia Gwau ameshiriki Mahafali ya kidato cha sita Shule ya sekondari ya wasichana Tumaini iliyopo Kinampanda Wilaya ya Iramba akiwa mgeni rasmi wa mahafali hayo.
Katika mahafali hayo, Mhe. Martha Nehemia Gwau aliambatana na wageni mbalimbali akiwemo Afisa elimu taaluma wilaya pamoja na wageni wengine waalikwa waliofanikiwa kufika katika hafla hiyo.
Aidha, Mhe. Martha Nehemia Gwau aliwasihi wanafunzi katika hotuba yake kusoma kwa bidii na kuishi kwenye zao Ili kufikia malengo yao kabla ya maisha ya ndoa pia amewaahidi walimu kuzibeba changamoto walizompa na kwenda kuzifanyia kazi haraka Ili wanafunzi waendelee kupata elimu bora.
Vilevile, Katika mahafali hiyo, Mhe. Martha Nehemia Gwau amepata nafasi ya kuonyeshwa namna ya kutengeneza Pipi yenye maziwa na kahawa.
Imetolewa na
Ofisi ya Mbunge Viti Maalum Mkoa wa Singida.
#MarthaGwauKazini
#KaziIendelee✅✅
Katika mahafali hayo, Mhe. Martha Nehemia Gwau aliambatana na wageni mbalimbali akiwemo Afisa elimu taaluma wilaya pamoja na wageni wengine waalikwa waliofanikiwa kufika katika hafla hiyo.
Aidha, Mhe. Martha Nehemia Gwau aliwasihi wanafunzi katika hotuba yake kusoma kwa bidii na kuishi kwenye zao Ili kufikia malengo yao kabla ya maisha ya ndoa pia amewaahidi walimu kuzibeba changamoto walizompa na kwenda kuzifanyia kazi haraka Ili wanafunzi waendelee kupata elimu bora.
Vilevile, Katika mahafali hiyo, Mhe. Martha Nehemia Gwau amepata nafasi ya kuonyeshwa namna ya kutengeneza Pipi yenye maziwa na kahawa.
Imetolewa na
Ofisi ya Mbunge Viti Maalum Mkoa wa Singida.
#MarthaGwauKazini
#KaziIendelee✅✅