Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 2,833
- 1,301
MBUNGE NDAISABA RUHORO AZUNGUMZA NA MAKUNDI MBALIMBALI KATA YA MABAWE, NGARA
MHE. NDAISABA GEORGE RUHORO Mbunge wa Jimbo la Ngara amehudhuria Mkutano wa hadhara Kata ya Mabawe ulioandaliwa na UMOJA WA VIJANA WA CCM PAMOJA UMOJA WA VIJANA WA BODA BODA Kata ya Mabawe.
Mhe. Ndaisaba Ruhoro amepokea kero za wananchi na kuzitatua, ameshafanya mikutano zaidi ya kumi ndani ya Kata ya Mabawe na kuimarisha mahusiano ya Chama Cha Mapinduzi na Serikali kwa wananchi wa Kata ya Mabawe
Aidha, Mhe. Ndaisaba Ruhoro amewasihi wananchi waendelee kumwamini Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DKT. SAMIA SULUHU HASSAN Mbunge, Pamoja na Madiwani kwani wamesukuma miradi mingi kwenye Kata zote za Jimbo la Ngara.
Wananchi wakiwakirisha makundi tofauti wametoa pongezi nyingi kwa Mhe. Ndaisaba Ruhoro kupitia hadhara ya mkutano huo na kumtuza zawadi kwa uongozi bora unaotatua kero za wananchi.
Katibu Mkuu wa CCM Taifa Dkt. Emmanuel Nchimbi alisema " Mwana CCM yeyote hahitaji kibali kuyaongelea na kuyapongeza mazuri ya CCM na Viongozi wa CCM" wananchi wa Mabawe wamedhihirisha Kauli hiyo Kwa vitendo kwa MAMA SAMIA SULUHU HASSAN, Mhe. Ndaisaba Ruhoro na Mhe. Safari Diwani wa Kata ya Mabawe
Attachments
-
WhatsApp Image 2024-11-15 at 09.41.28.jpeg164.2 KB · Views: 2 -
WhatsApp Image 2024-11-15 at 09.41.28 (1).jpeg141.8 KB · Views: 2 -
WhatsApp Image 2024-11-15 at 09.41.29.jpeg118.5 KB · Views: 2 -
WhatsApp Image 2024-11-15 at 09.41.30.jpeg192.3 KB · Views: 3 -
WhatsApp Image 2024-11-15 at 09.43.00.jpeg112.1 KB · Views: 6