Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 2,833
- 1,301
📌 AHOJI UTEKELEZWAJI WA AAGIZO LA WAZIRI MKUU
📌 ATAKA KUJUA HALI YA KIUTENDAJI KWENYE HALMASHAURI ILIVYO
MBUNGE wa Viti maalum Mkoani Iringa Mhe. Rose Tweve ametaka kujua kiundani juu ya utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa aliliolitowa mapema tarehe 22 Mei 2024 akiziagiza Halmashauri kuu zote Nchini kutenga Bajeti juu ya ununuzi Dawa za kupambana na Mbu huko Kibaha.
Mhe. Rose Tweve akizungumza mbele ya Naibu spika wa Bunge amesema "Mhe. Naibu Spika bado sijiridhishwa na majibu ya Serikali, Swali langu lilikuwa wazi kuwa ni Halmashauri ngapi hapa Nchini zimetekeleza agizo la waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizitaka Halmashauri Kuu Nchini kutenga Bajeti juu ya ununuzi wa Dawa Kibaha na kusambaza kwenye Halmashauri zote Nchini katika kuhakikisha wananyunyuzia mazalia ya mbu ili kuokoa maisha ya Watanzania wakiwemo akina mama na watoto".
Aidha, Mhe. Rose Tweve ameisisitiza Serikali kuchukua hatua za haraka katika kutekeleza agizo hilo la Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa
#Alamaonline #Pamojatuongee
📌 ATAKA KUJUA HALI YA KIUTENDAJI KWENYE HALMASHAURI ILIVYO
MBUNGE wa Viti maalum Mkoani Iringa Mhe. Rose Tweve ametaka kujua kiundani juu ya utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa aliliolitowa mapema tarehe 22 Mei 2024 akiziagiza Halmashauri kuu zote Nchini kutenga Bajeti juu ya ununuzi Dawa za kupambana na Mbu huko Kibaha.
Mhe. Rose Tweve akizungumza mbele ya Naibu spika wa Bunge amesema "Mhe. Naibu Spika bado sijiridhishwa na majibu ya Serikali, Swali langu lilikuwa wazi kuwa ni Halmashauri ngapi hapa Nchini zimetekeleza agizo la waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizitaka Halmashauri Kuu Nchini kutenga Bajeti juu ya ununuzi wa Dawa Kibaha na kusambaza kwenye Halmashauri zote Nchini katika kuhakikisha wananyunyuzia mazalia ya mbu ili kuokoa maisha ya Watanzania wakiwemo akina mama na watoto".
Aidha, Mhe. Rose Tweve ameisisitiza Serikali kuchukua hatua za haraka katika kutekeleza agizo hilo la Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa
#Alamaonline #Pamojatuongee