Pre GE2025 Mbunge Saashisha Mafuwe Akabidhi Mashine ya X-Ray ya Milioni 196 na Magari Mawili, Hospitali ya Wilaya ya Hai

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

Mbunge Saashisha Mafuwe akabidhi mashine ya X-ray yenye thamani ya Tsh. milioni 196 na magari mawili
Your browser is not able to display this video.

Mbunge wa Jimbo la Hai, Mkoani Kilimanjaro, Saashisha Mafuwe tarehe 10 Agosti, 2024 amefanya ziara katika Hospitali ya Wilaya ya Hai na kukabidhi Ultrasound na X Ray Machine za kisasa zenye thamani ya zaidi ya Milioni 196 pamoja na Magari Mawili ya Hospitali ya Wilaya.

Saashisha Mafuwe ametembelea na kuona vifaa na majengo mapya ikiwemo; Jengo la wodi ya wazazi, Jengo la Maabara, Jengo la Famasi, Jengo la Private ward, Njia za kuunganisha majengo yaani walk way, Jengo la incinerator yaani machine ya kuchoma taka, Jengo la ICU.

Zaidi ya Wananchi 350 ambao hufika kupata matibabu katika hospitali ya Wilaya ya Hai kila siku wanatarajia kunufaika na huduma bora za kiafya zitolewazo hospitalini hapo baada ya Serikali kuendelea kuboresha huduma hizo ikiwemo ununuzi wa vifaa tiba mbalimbali.

Soma Pia:
Akikabidhi mashine hiyo, Mbunge Saashisha Mafuwe amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jinsi ambavyo ameendelea kutoa fedha za miradi mbalimbali katika wilaya ya Hai ambapo imepelekea wananchi wa wilaya ya Hai kuondokana na adha mbalimbali walizokuwa wakikumbana nazo hapo awali.

"Leo hii tuna X -ray Mashine mpya, ICU yenye vifaa vyote vya kisasa, maabara pamoja na wataalam wa kutosha, hakika hii ni dhamira nzuri ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kutuhudumia wananchi wa Hai" - Saashisha Mafuwe.



 

Attachments

  • WhatsApp Video 2024-08-10 at 12.02.32.mp4
    7.3 MB
  • WhatsApp Image 2024-08-10 at 12.02.47.jpeg
    34.8 KB · Views: 3
Vyote vina thamani sawa na mshahara wake wa miaka mitatu kwa pamoja/jumla.

Tumesikia kuwa siku hizi wanalipwa tsh 18,000,000 baada ya Samia kuongeza tsh 5,000,000 kwenye vitita vyao.

Chanzo cha mapato yake yote ni kipi?
 
Vyote vina thamani sawa na mshahara wake wa miaka mitatu kwa pamoja/jumla.

Tumesikia kuwa siku hizi wanalipwa tsh 18,000,000 baada ya Samia kuongeza tsh 5,000,000 kwenye vitita vyao.

Chanzo cha mapato yake yote ni kipi?
Sarakasi hizo machishe kapewana CCM baada ya kuona ana hali mbaya jimboni kama Samia ataamuru uchaguzi uwe huruma na haki wabunge wengi wa CCM hawatarudi tena bungeni.
 
Tumpongeze Mbunge au Mhe Raisi?

Yeye angetuambia Hadi Leo Serikali imeshamlipa zaidi ya Shs Milioni 600. Karudisha shukrani gani kwa Wana - Hai?
 
Alikwina?
 
Vyote vina thamani sawa na mshahara wake wa miaka mitatu kwa pamoja/jumla.

Tumesikia kuwa siku hizi wanalipwa tsh 18,000,000 baada ya Samia kuongeza tsh 5,000,000 kwenye vitita vyao.

Chanzo cha mapato yake yote ni kipi?
Hivyo vifaa hajanunua yeye. Vimenunuliwa na serikali - ie, ni kodi zetu watanzania.
 
196m x- Ray do Mbuge atupie na risiti
 
Magari mbona yana number plate za serikali?
 
Hawa mbuzi hawana aibu, wanapiga kampeni kwa kutumia pesa zetu halafu eti mbunge sijui mama katoa, wanafikiri hatuna akili
 
Mbowe alishindwa kukabidhi mashine ya x ray kwa miaka 20 ya ubunge wake, shame on him
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…