Mbunge Sebastian Kapufi Ataka Kasi Iongezeke Ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji Mpanda

Mbunge Sebastian Kapufi Ataka Kasi Iongezeke Ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji Mpanda

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

SEBASTIAN KAPUFI ATAKA KASI IONGEZEKE UJENZI WA SKIMU YA UMWAGILIAJI MPANDA

"Je, Serikali inasema nini kuhusu kasi ndogo ya mradi wa Umwagiliaji Kata ya Mwamkulu Mpanda" - Mhe. Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini

"Mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji iliamza utekelezaji wa mradi wa Umwagiliaji Mwamkulu ambao ulisuasua awali kutokana na kuchelewa kwa malipo ya Awali ya Mkandarasi. Kwasasa Malipo yamekamilika na kazi ya ujenzi inaendelea na utekelezaji wake umefikia 50%" - Naibu Waziri wa Kilimo, David Silinde

"Je, Serikali inayotaarifa kuwa kasi bado ni ndogo na kusuasua kwa awali kumerejea tena? Msimu wa Mvua umeanza na Wananchi wanalitegemea Bonde hilo kupitia Skimu ya Kienyeji. Serikali inawasaidiaje Wakulima wakati mradi haujaanza?" - Mhe. Sebastian Kapufi, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini

"Mkandarasi bado yupo ndani ya muda maana mradi unatarajiwa kukamilika Aprili 2025 na tumeshapeleka fedha. Pia huwa tunawaruhusu Wakulima msimu wa Mvua kutumia Bonde bila kuathiri miundombinu ambayo Mkandarasi anaitengeneza" - David Silinde
hospitali-pc.jpg
 
Miradi ya Umwagiliaji Serikali ya Mama Samia imewekeza vema na tukiisimamia vema naamini ikimalizika yote na kusimamowa vema, tunaweza lisha nchi nyingi za Afrika na Arab countries..!!

Tatizo naloliona mbeleni ni usimamizi madhubuti, maana hapo ndio tatizo kubwa, tumeanza vema sana, serikali iweke macho makali kabisa hii miradi isije kufa huko mbeleni..!!
 
Back
Top Bottom