Mbunge Sichalwe Afanya Mkutano na Wakulima Kijiji cha Nkala, Wilaya ya Momba

Mbunge Sichalwe Afanya Mkutano na Wakulima Kijiji cha Nkala, Wilaya ya Momba

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

MHE. CONDESTER SICHALWE AFANYA MKUTANO NA WAKULIMA WA KIJIJI CHA NKALA, MOMBA

Mbunge wa Jimbo la Momba Mkoa wa Songwe, Mhe. Condester Mundy Michael Sichalwe na Afisa Kilimo wamekutana na wakulima wa Kijiji cha Nkala na kuwasisitiza kuhudhuria mafunzo ya Kilimo yanayotolewa na Maafisa Kilimo.

Katika Mkutano huo wa hadhara, Mhe. Condester Sichalwe aliambatana na Maafisa Kilimo wa Kijiji cha Nkala ambao walizungumza na wananchi kuhusu Kilimo chenye tija, Mbegu bora za kutumia na jiografia ya eneo inayoendana na aina ya Kilimo cha Mpunga

Wananchi wa Kijiji cha Nkala wametoa maoni yao kuhusu mwenendo wa Sekta ya Kilimo huku wakidai kukutana na changamoto za Kukosa mikopo, kupewa mbegu ambazo hazifai, kukosa mbolea na wananchi wa chini Kukosa mikopo wanapoomba, wazee wa TASAF kutopata stahiki zao na kutokuwa na benki Nkala ili fedha wazichukulie hapo hapo Kijijini

Mhe. Condester Sichalwe amesema kuwa wananchi wanapaswa kuunda vikundi vya ushirika ili waaminike kupewa mikopo kwani wananchi wengine dhamana yao ni vikundi vya pamoja.

Mhe. Condester Sichalwe amesema ili ulime na upate faida nzuri ni lazima kuzingatia ubora wa udongo, ubora wa mbegu, jiografia ya eneo na kuomba Wataalam wa TASAF kukutana na wahusika ili kushauriana na wazee kwanini TASAF zao zinachelewa sana.
 

Attachments

Back
Top Bottom