Mbunge wa Jimbo la Itilima, Mkoani Simiyu, Njalu Silanga amesema kuwa serikali imefanya kazi kubwa ya kuboresha sekta ya kilimo, ambapo Wilaya hiyo imepokea matrekta 35 kwa ajili ya kulima mashamba ya wakulima wa pamba kwa bei nafuu.
Mbunge huyo aliongeza kuwa dhamira yake ni kuona kila mkulima wa pamba katika jimbo lake anazalisha kilo 1,500 kwa hekari moja kabla ya kuacha ubunge.
"Natamani kupokea simu moja nikitangaza kuacha ubunge, nikijua wakulima wote wanazalisha kilo 1,500 kwa hekari moja ili waweze kunufaika na kilimo cha zao hili.