Mbunge Sylvia Sigula: Watanzania Wanatamani Kutumia Gesi Kwenye Magari Kwasababu Gesi ni Gharama Nafuu

Mbunge Sylvia Sigula: Watanzania Wanatamani Kutumia Gesi Kwenye Magari Kwasababu Gesi ni Gharama Nafuu

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301
Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Sylvia Francis Sigula ameihoji Serikali ni magari mangapi ya Serikali yamefungwa mfumo wa gesi baada ya kuanza kwa kuhamasisha matumizi ya mfumo huo.​

Sigula amehoji hilo Bungeni Jijini Dodoma wakati akichangia Makadiro ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa mwaka wa Fedha 2024/25.

“Tumeona kwenye hotuba zaidi ya magari 3000 yamebadilishwa kwenye mfumo wa gesi lakini tunasema Watanzania wanatamani kuendelea kutumia gesi kwenye magari yao kwasababu ni gharama nafuu na tumeona mna mpango wa kuongeza vituo japo ni vichache lakini vifaa vya kubadilishia mifumo ni gharama sana ukitaka kubadili sio chini ya milioni mbili lakini sijaona Serikali ambayo ndio inasimamia jambo hili hamasa ipi inatupa Serikali wao kama Serikali ni magari mangapi yamefunga gesi?

WhatsApp Image 2024-04-26 at 18.58.48.jpeg
WhatsApp Image 2024-04-26 at 18.58.48(1).jpeg
WhatsApp Image 2024-04-26 at 18.58.48(2).jpeg
WhatsApp Image 2024-04-26 at 18.58.49.jpeg
WhatsApp Image 2024-04-26 at 18.58.49(1).jpeg
 
Kufungiwa gesi ni usumbufu tu.bora tuendelee na mafuta.kufungia mtungi wa kilo 11 milioni 2.6-3 baada ya kufungiwa unatakiwa Kila baada ya miezi mitatu uwapelekee waliokufungia waikague kama huo mfumo Bado uko salama na unawalipa Tena pesa nyingi tu.
 
Back
Top Bottom