Uzalendo wa Kitanzania
JF-Expert Member
- Mar 8, 2020
- 3,585
- 8,106
Wadau hamjamboni nyote?
Jisomeeni wenyewe hapo chini kwa kiswahili:
Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mrisho Mashaka Gambo amemuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kusaidia kufanikisha upatikanaji wa Shilingi milioni 200 zilizotapeliwa na waliokuwa Viongozi wa Umoja wa Waendesha Bodaboda Jiji la Arusha, miaka minne iliyopita.
Wakati wa Mkutano mkuu wa Waendesha Bodaboda Jiji la Arusha uliofanyika Ijumaa Disemba 27, 2024, mbele ya mgeni rasmi ambaye ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM Taifa, Mohammed Kawaida, Gambo amedai kuwa watu hao wanafahamika, akiahidi kutoa milioni moja kwa kila atakayefanikisha kutiwa mbaroni kwa wahusika wa wizi na utapeli huo wa fedha za wavuja jasho.
Jisomeeni wenyewe hapo chini kwa kiswahili:
Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mrisho Mashaka Gambo amemuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kusaidia kufanikisha upatikanaji wa Shilingi milioni 200 zilizotapeliwa na waliokuwa Viongozi wa Umoja wa Waendesha Bodaboda Jiji la Arusha, miaka minne iliyopita.
Wakati wa Mkutano mkuu wa Waendesha Bodaboda Jiji la Arusha uliofanyika Ijumaa Disemba 27, 2024, mbele ya mgeni rasmi ambaye ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM Taifa, Mohammed Kawaida, Gambo amedai kuwa watu hao wanafahamika, akiahidi kutoa milioni moja kwa kila atakayefanikisha kutiwa mbaroni kwa wahusika wa wizi na utapeli huo wa fedha za wavuja jasho.