MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,018
- 16,802
Mbunge wa Kawe Askofu Josephat Mathias Gwajima hujawahi na wala humpendi mpaka hukupenda Rais Samia kuwa Kiongozi hivi leo isipokuwa unachokifanya sasa ni kumpaka tu Mafuta Mama wa Watu kwa Mgongo wa Chupa na bahati nzuri hata Yeye ameshakushtukia na anasubiri ujae vizuri amalize Shughuli ndani ya Kamati ya Maadili na CC ya CCM.
Gwajima wadanganye wale Wapuuzi wako kadhaa uliowateka Akili zao mbovu na wanakuamini ila kamwe siyo kwa Sisi wengine ambao tunayajua yako angalau kwa 75% tu na yanatutosha na leo tunaanza Kufunguka taratibu juu ya tabia zako za Unafiki, Dharau, Sanifu na Ubaguzi wa Kidini.
Askofu Gwajima hivi siyo Wewe wakati Hayati Rais Dkt. Magufuli ( Poti wako na aliyekuweka hapo Kawe kuwa Mbunge ) ulikuwa ukienda Kuzungumza nae Mambo yenu ulikuwa ukimsihi asimshirikishe Makamu wake ( Samia Suluhu Hassan Kipindi hicho ) na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwa Uislamu wao?
Mimi Mightier ni Mkristo tena Mkatoliki kabisa ila kama kuna Kiongozi wa Dini ( hasa wa haya Madhehebu ya Kiroho na Kilokole ) ambaye kupitia Watu wake wa karibu nimeambiwa ni Mbaguzi na hawapendi Waislamu ni Wewe Askofu Jossphat Mathias Gwajima.
Na Ushahidi wa hili upo kupitia ile Kauli yako ambayo Watu wa CHADEMA walikuwa wakiirudia mno katika Kampeni za mwaka jana. Na Kauli ile ilikumaliza sana tu isipokuwa kwakuwa Ndugu yako ( Poti Hayati) alishaamua uwe Mbunge iwe Jua au Mvua ukawa kwa Mabavu ya NEC na si ya wana Kawe.
Maelezo yako yote uliyoyatoa leo pamoja na Sifa dhidi ya President Samia's Royal Tour yake yamejaa Unafiki mtupu na kwa Wabobezi wa Saikolojia kama Mightier leo Body Language yako ilikuwa haiendani na uliyokuwa ukiyasema.
Wenye Akili Kubwa kukuzidi Askofu Jossphat Mathias Gwajima ( japo huwa unajitapa una Akili sana ) tumejua kuwa leo umemsifia mno Mama ( Rais Samia Suluhu Hassan ) kwakuwa unajua kuna Hukumu yako ndani ya Chama Tawala ( CCM ) dhidi yako inakusubiri na Yeye kama Mwenyekiti wako ndiyo mpiga Rungu Mkuu wa Adhabu Kali inayokustahili.
Rais Samia Suluhu Hassan nawe namalizia kwa Kukuambia kuwa kama kuna Mtu ambaye hakupendi na hajapenda Urais wako na hata akiwa na Marafiki zake Wanafiki na Magaidi ndani ya Chama Tawala ( CCM ) basi Mwandamizi ( Kiongozi ) wao nj huyu Mbunge wa Kawe Askofu Jossphat Gwajima.
Tena nakusihi kuwa nae makini kuliko unavyodhania ni Nyoka mwenye Sumu Kali ambaye alilelewa vyema na Mtangulizi wako ( sasa Hayati ) ili aje Kuwangata vibaya Watanzania ila kwa sasa anataka kuanza Kukungata Wewe Kwanza ila bado anakitafuta Kisigino chako hajabahatika kukipata kwakuwa nawe hutulii sehemu moja mara Unguja mara Dar es Salaam na mara Dodoma.
Askofu Gwajima ANGUKO LAKO laja.
Gwajima wadanganye wale Wapuuzi wako kadhaa uliowateka Akili zao mbovu na wanakuamini ila kamwe siyo kwa Sisi wengine ambao tunayajua yako angalau kwa 75% tu na yanatutosha na leo tunaanza Kufunguka taratibu juu ya tabia zako za Unafiki, Dharau, Sanifu na Ubaguzi wa Kidini.
Askofu Gwajima hivi siyo Wewe wakati Hayati Rais Dkt. Magufuli ( Poti wako na aliyekuweka hapo Kawe kuwa Mbunge ) ulikuwa ukienda Kuzungumza nae Mambo yenu ulikuwa ukimsihi asimshirikishe Makamu wake ( Samia Suluhu Hassan Kipindi hicho ) na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwa Uislamu wao?
Mimi Mightier ni Mkristo tena Mkatoliki kabisa ila kama kuna Kiongozi wa Dini ( hasa wa haya Madhehebu ya Kiroho na Kilokole ) ambaye kupitia Watu wake wa karibu nimeambiwa ni Mbaguzi na hawapendi Waislamu ni Wewe Askofu Jossphat Mathias Gwajima.
Na Ushahidi wa hili upo kupitia ile Kauli yako ambayo Watu wa CHADEMA walikuwa wakiirudia mno katika Kampeni za mwaka jana. Na Kauli ile ilikumaliza sana tu isipokuwa kwakuwa Ndugu yako ( Poti Hayati) alishaamua uwe Mbunge iwe Jua au Mvua ukawa kwa Mabavu ya NEC na si ya wana Kawe.
Maelezo yako yote uliyoyatoa leo pamoja na Sifa dhidi ya President Samia's Royal Tour yake yamejaa Unafiki mtupu na kwa Wabobezi wa Saikolojia kama Mightier leo Body Language yako ilikuwa haiendani na uliyokuwa ukiyasema.
Wenye Akili Kubwa kukuzidi Askofu Jossphat Mathias Gwajima ( japo huwa unajitapa una Akili sana ) tumejua kuwa leo umemsifia mno Mama ( Rais Samia Suluhu Hassan ) kwakuwa unajua kuna Hukumu yako ndani ya Chama Tawala ( CCM ) dhidi yako inakusubiri na Yeye kama Mwenyekiti wako ndiyo mpiga Rungu Mkuu wa Adhabu Kali inayokustahili.
Rais Samia Suluhu Hassan nawe namalizia kwa Kukuambia kuwa kama kuna Mtu ambaye hakupendi na hajapenda Urais wako na hata akiwa na Marafiki zake Wanafiki na Magaidi ndani ya Chama Tawala ( CCM ) basi Mwandamizi ( Kiongozi ) wao nj huyu Mbunge wa Kawe Askofu Jossphat Gwajima.
Tena nakusihi kuwa nae makini kuliko unavyodhania ni Nyoka mwenye Sumu Kali ambaye alilelewa vyema na Mtangulizi wako ( sasa Hayati ) ili aje Kuwangata vibaya Watanzania ila kwa sasa anataka kuanza Kukungata Wewe Kwanza ila bado anakitafuta Kisigino chako hajabahatika kukipata kwakuwa nawe hutulii sehemu moja mara Unguja mara Dar es Salaam na mara Dodoma.
Askofu Gwajima ANGUKO LAKO laja.