Mbunge wa Mpwapwa angalia wenzio wanachanja mbuga wewe unasali tu

Mbunge wa Mpwapwa angalia wenzio wanachanja mbuga wewe unasali tu

ebaeban

JF-Expert Member
Joined
Jan 15, 2012
Posts
2,205
Reaction score
2,697
IMG_2828.jpg

Mbunge wa Jimbo wa Jimbo la Mlimba, Godwin Kunambi amemaliza changamoto ya Umeme, Maji na Choo katika Soko la Chita jimboni humo baada ya kutoa Sh Milioni 1.5.

Mbunge wetu wa Mpwapwa unaona wabunge wenzako wanavyosonga mbele serikali itawafuata nyuma wewe umebaki kuitisha misa tu badala ya kupambana.

Changamoto za jimbo la Mpwapwa zinajulikana mtu anaweza hata kuziimba kama ndege, unangoja nini? Utazitatua huko kanisani unakoshinda unasali?

Labda nikusaidie:

1. Barabara ya lami toka mbuyuni Kongwa hadi Mwanakiyanga Mpwapwa- Hii ni changamoto kubwa hata miaka miwili ikiwa bado tutakuelewa lakini inabidi uanze mahali.

2. Maji, maji ya baridi huu eti ni mradi wa watu kujipatia kipato . si unaona mikokoteni na baiskeli na madumu barabarani? Hii ya uuzaji maji inabidi uiondoe. kwani maji yako chini kidogo tu tukichimba tutayakuta, mradi wa kuuza maji inabidi uumalize

3. Jokofu la mochwale hospitali ya wilaya siyo zuri sana maiti zinaharibika haraka liangalie.

4. Bima za afya walioisha kata fuatilia wapate huduma

5. Buni vyanzo vipya vya mapato, makusanyo ya mapato ya halmashauri ni hafifu, ni vigumu kufikisha malengo kwa vyanzo vilivyopo inabidi ulivalie njuga pamoja na madiwani ukizubaa ulete siasa unajua kitakachotokea serikali awamu hii haina mchezo mchezo

6. Elimu. Elimu shule za secondali ziboreshwe hizi hizi zilizopo, Maabara za masomo ya sayansi ziboreshwe na anzisha vyumba vya kompyuta. TEHEMA kipindi hiki ndo habari ya mjini, boresha zilizopo siyo lazima kuanzisha zingine, toka kanisani tembelea mashuleni, shule za msingi na secondari zungumza na walimu upate vilio vyo uvifikishe serikalini kupitia vikao vya bunge.

7. Vifo vya akina mama wajawazito,fuatilia watumishi afya kwenye zahanati n VITUO VYA AFYA. sikiliza vilio vyao ili uwapandishe morale wa kazi pia ukaangalie akina mama ngojea pale hospitali ya wilaya ujilizishe na mazingila wanayoishi.

8. Anza mchakato inatakiwa vijiji vya Bumila, Chibwechangula na Lupeta wapate zahanati na iwe Chibwechangula ili iwe rahisi kuhudumia vijiji hivyo vyote masuala ya chanjo kwa watoto na akina mama wajawazito pia na masuala mengine ya afya, hili yule uliyemrithi alinasibiwa kwamba aliuliza masuali mengi kuliko mbunge yoyote , maswali 103 hilo la zahati eti hakuuliza, sijui sasa alikuwa anauliza nini.

9. VETA , kuwepo kwa mafunzo ya VETA kunahitajika sana Mpwapwa kuliko hata Chato, VETA Mpwapwa inalipa sana ikiwepo, hiyo ni changamoto anza nayo ili Mpwapwa iwe kama sehemu zingine

10. Umeme. umeme Mpwapwa umekuwa wa kubahatisha hasa kipindi hiki chako mbunge. Umeme ni maisha unakatika kila siku saa ingine masaa 24, fuatilia kuna nini? Umeme mheshimiwa mbunge usipofuatilia ujue tatizo ni nini unatosha kabisa kukung`oa.

Toka huko kanisani unakosali, ingia mtaani, angalia wenzio wanavyochachalika. Mlungu ntaza hanze nolumanko.

Rais anapeleka maendeleo Chato, na wewe Mbunge yalete jimbo la Mpwapwa


Aksante Mh .Mbunge nakutakia kazi njema sikulaumu chochote bado ndio umeanza ila nakusaidia tu uanzeje.
 
Umeleta litania ya matatizo kama kawaida yetu. Ila nafikiri Mh.Mbunge amekusikia
 
Bora nyie wa Mp town japo umeme wanakata kila siku.

Sisi wa huku kiboriyani shida tupu! Barabara hazipitiki, network hakuna,maji hakuna,tukikata mkaa police wanatubambika kesi za kulima bangi.
 
Umenena yalio mema kwani mpwapwa ni kati ya Wilaya kongwe kabisa ila kimaendeleo ni zero. Asiye sikia la Mkuu huvunjika guu 2025 sio mbali sana, atahukumiwa na wajumbe.
 
Hivi mbunge wa sasa wa Mpwapwa ni nani mkuu....
Nimetoka Mpwapwa miaka kadhaa iliyopita.
Nimeguswa sana na hili suala la ''maji ya kwenye mikokoteni''. Kumbe hadi sasa hali hii inaendelea ?
Nakumbuka walikua wanatoa maeneo ya Kikombo kule, hii si sawa kwa makao makuu ya wilaya kupitia kadhia za namna hii, nyakati hizi.
 
Hivi mbunge wa sasa wa Mpwapwa ni nani mkuu....
Nimetoka Mpwapwa miaka kadhaa iliyopita.
Nimeguswa sana na hili suala la ''maji ya kwenye mikokoteni''. Kumbe hadi sasa hali hii inaendelea ?
Nakumbuka walikua wanatoa maeneo ya Kikombo kule, hii si sawa kwa makao makuu ya wilaya kupitia kadhia za namna hii, nyakati hizi.
Anaitwa Nataniel Malima yeye saa zote anaitisha misa tu baada ya kuingia chaka
 
Kusali ni muhimu, maana wachawi wamepamba moto.....msije mkamsombesha mbunge tofali usiku wa manane. Unafikiri yeye ni mjinga hawajui!
 
Back
Top Bottom