Mbunge wa Viti Maalum (CHADEMA), Felista Njau aeleza namna alivyotumia pesa kupata Ubunge na kwenda kuapa Dodoma kwa siri

Watanzania hasa wanaopiga kelele kwenye club house, space, vyama vya siasa na wanahatakati huru wanaojiita '" eti ni makamanda wanatukomboa"' ni wachumia tumbo watafuta chochote hakuna Cha kututetea Wala ukombozi. Mfano mdogo hili tukio la Gekul, alikuwa na yeye anajiita kamanda mkomboaji, akapata fursa serikalini ona kilichotokea. Pata uongozi au fedha tujie tabia yako. Wote wasaka tonge kupitia mgongo wa wananchi
 
Kuna hitaji kubwa la kikatiba kuongeza sifa na vigezo vya mtu kuwa Mbunge. Alichoongea Felista ni uharo mtupu na kadhihirisha alivyo mtupu kichwani. CHADEMA nao wajisahihishe. Rushwa ndani ya chama chao imekithiri hasa nyakati za uchaguzi. Au watataka kusema CCM ndo imesababisha wao kuwa na wajumbe wapenda rushwa kwenye chaguzi zao za ndani?
 
"Mungu anakupa kitu ukiwa unafanya" huyu ni Mungu wa namna gani anayesupport rushwa kwa wajumbe?
"Nyumbani kwetu mimi ndiyo tajiri" kumbe wanagombea ubunge ili kwenda kutajirika
 
Chadema ilishasema vita maalum vifutwe na kuonyesha seriousness ndio chama pekee kilichoweka wagombea wengi wanawake katika historia ya Tanzania zaidi ya 75 waligombea majimboni.

So Chadema inaheshimu wanawake ila inataka wapewe equal footing kwenye kupambana sio dezo dezo za viti maalum.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…