Pre GE2025 Mbunge wa Viti Maalumu CCM Jesca Kishoa: Kuna kiongozi alinishauri nisisaidie wananchi, alitaka nihonge wajumbe ili nishinde Uchaguzi

Pre GE2025 Mbunge wa Viti Maalumu CCM Jesca Kishoa: Kuna kiongozi alinishauri nisisaidie wananchi, alitaka nihonge wajumbe ili nishinde Uchaguzi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu.

Wabunge wa CCM washaanza kutoa siri za kambi

Mbunge wa viti maalum Jesca Kishoa hivi karibuni akiwa nanaongea na wananchi amefichua kuwa aliwahi kushauriwa na kiongozi mmoja wa kisiasa kwamba abadili mbinu zake za kisiasa na kwamba badala ya kuwahudumia wananchi, aweke akiba ya fedha kwa ajili ya kutoa hongo wakati wa uchaguzi.

kizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Nkalakala, Wilaya ya Mkalama, Mkoani Singida, tarehe 16 Februari, 2025 Kishoa amesema:

"Aliniambia, ‘Jesca, tunza fedha zako, cheza na wajumbe. Unatumia njia ndefu mno. Kipyenga kikipulizwa, zitumie kuwahonga wajumbe ikiwa utagombea kupitia CCM au chama chochote.’

Katika ziara hiyo, Mhe. Jesca Kishoa alizungumza na wananchi na pia alitoa mchango wa zaidi ya shilingi milioni 6 kwa ajili ya kukamilisha miradi ya maendeleo. Aligawa mitungi 40 ya gesi kwa mama ntilie, seti 12 za jezi kwa timu mbalimbali, na shilingi laki tano kwa mama mwenye mtoto mwenye ulemavu.

 
Wakuu.

Wabunge wa CCM washaanza kutoa siri za kambi

Mbunge wa viti maalum Jesca Kishoa hivi karibuni akiwa nanaongea na wananchi amefichua kuwa aliwahi kushauriwa na kiongozi mmoja wa kisiasa kwamba abadili mbinu zake za kisiasa na kwamba badala ya kuwahudumia wananchi, aweke akiba ya fedha kwa ajili ya kutoa hongo wakati wa uchaguzi.

kizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Nkalakala, Wilaya ya Mkalama, Mkoani Singida, tarehe 16 Februari, 2025 Kishoa amesema:

"Aliniambia, ‘Jesca, tunza fedha zako, cheza na wajumbe. Unatumia njia ndefu mno. Kipyenga kikipulizwa, zitumie kuwahonga wajumbe ikiwa utagombea kupitia CCM au chama chochote.’

Katika ziara hiyo, Mhe. Jesca Kishoa alizungumza na wananchi na pia alitoa mchango wa zaidi ya shilingi milioni 6 kwa ajili ya kukamilisha miradi ya maendeleo. Aligawa mitungi 40 ya gesi kwa mama ntilie, seti 12 za jezi kwa timu mbalimbali, na shilingi laki tano kwa mama mwenye mtoto mwenye ulemavu.

Kwa hiyo amewasaidia nini wananchi, na nini mchango wake Bungeni
 
Kadada kajinga haka?

Sasa si obvious game kwenye siasa?

Wananchi hawafanyi maamuzi nani apeperushe bendera ya chama gani...

Hawa watu hawatakiwi kwenye siasa zetu
 
watanzania ni wajinga sana, iko siku tutapigwa miti uwanja wa taifa
 
Hapo anaona ameongea bonge la point na kufichua siri nzitoooo, naona kawa mzunguuuu
 
Wakuu.

Wabunge wa CCM washaanza kutoa siri za kambi

Mbunge wa viti maalum Jesca Kishoa hivi karibuni akiwa nanaongea na wananchi amefichua kuwa aliwahi kushauriwa na kiongozi mmoja wa kisiasa kwamba abadili mbinu zake za kisiasa na kwamba badala ya kuwahudumia wananchi, aweke akiba ya fedha kwa ajili ya kutoa hongo wakati wa uchaguzi.

kizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Nkalakala, Wilaya ya Mkalama, Mkoani Singida, tarehe 16 Februari, 2025 Kishoa amesema:

"Aliniambia, ‘Jesca, tunza fedha zako, cheza na wajumbe. Unatumia njia ndefu mno. Kipyenga kikipulizwa, zitumie kuwahonga wajumbe ikiwa utagombea kupitia CCM au chama chochote.’

Katika ziara hiyo, Mhe. Jesca Kishoa alizungumza na wananchi na pia alitoa mchango wa zaidi ya shilingi milioni 6 kwa ajili ya kukamilisha miradi ya maendeleo. Aligawa mitungi 40 ya gesi kwa mama ntilie, seti 12 za jezi kwa timu mbalimbali, na shilingi laki tano kwa mama mwenye mtoto mwenye ulemavu.

Chukuwachakomapema mapema ni hatarii kwa maisha Yako!
 
Back
Top Bottom