Mbwana Samatta uwezo wake wa kawaida Mno, Anabebwa na bahati tu!

kikubwa ni kutumia nafasi anayoipata bila kujali kama ni nafasi nyepesi au ngumu. Kinachotakiwa ni goal tu vingine mbwembwe
 
Kwahiyo sio goli? Lilipofungwa hawakushangilia? halijawekwa kwenye record kwa kukosa mvuto? goli la mvuto kwako hua linakuaje?

Hoja yako ni mfu.
Zaidi ya matokeo, football is entertainment....lazima mfungaji awakune watazamaji kwa kujitahidi kufunga magoli yenye mvuto kadri awezavyo...tunataka magoli bora na si bora magoli...ndio maana mechi na Uganda alikosa goli la wazi kwa sababu ya kukariri kufunga "kiboya"
 
Mleta uzi unamkumbuka van nestroloy au pipo inzahgi drogba Louis saha Emanuel adebayor huiguin list ni kubwa sana
 
Kwa hiyo mchezaji akijikuta anataka kufunga goli ambalo wewe unaona halina mvuto ni bora aupige mpira nje ili isiwe kafunga goli lisilo na mvuto?

Una nipa mashaka kama wewe ni mfuatiliaji wa Football aisee!

Halafu naona unakwepa swali langu! Nimekuuliza swali,goli la mvuto hua likoje? Unataka mtu afunge kwa style ipi ili wewe uone kua goli lina mvuto?

Hivi kama wewe ni shabiki wa team fulani,kama mchezaji wa team unayoisapoti akifunga goli hutoshangilia coz kafunga goli lisilo na mvuto? Hiki ni kichekesho aisee!
 
Mwambie mkeo akukune
 
We mwenye kiwango kikubwa tuonyeshe magoli yako yenye mvuto.........
 
We endelea kumuombea njaa wakati tayari kuna timu "Fulani" ulaya zinawania sahihi yake.
 
Mleta Uzi laiti kama huu wivu ulionao kwa mwanaume mwenzako ungaliuhamishia kwa mkeo...ndo yako changa isingevunjika!
Punguza kihoro mtoto wa kiume, onesha kipaji chako nawe tukujue ebo!
 
tatizo ni umri waafrika wanacheza ulaya mmoja mmoja wanafanya vizuri coz wanacheza na wazungu wenye umri sahihi
 
Ukweli unabaki palepale....jamaa anabebwa na bahati ila mguuni wa kawaida sana!
angalia game ya juzi na uganda goli alilotaka kumfunga kipa wa uganda ndo utajua dogo ana utulivu na kujiamini kwa kias gan mitsubishi wewe.. na by the way umemfatilia huyu dogo wakati anapigana vita ya kiatu cha dhahabu cha champions league ya afrika enzi yupo mazembe?
 
Sometime kwenye mpira tunahitaji bahati zaidii ya uwezo wako waangalie wakina chicharito,schurrel na wengine bahati imewatoa so usimseme mtu kisa anabahati furahia uwezo wake na kazi yake mpaka bahati iishe then uanze kumsema
 


You are right na ninakubaliana nawe kwa asilimia moja.
 
Wakati flani JEMEDARI SAID akiwa TEAM MANAGER pale Azam Fc, kuna match Azam Fc ilichezea kichapo!

Kama kawaida ya akina Kashashas wetu! Kashasha Mmoja akamtumia SMS Kali sana Jemedari Saidi kuwa Azam Fc inafuga wachezaji mizigo, kashasha yule aka cite example kuwa ni HIMID MAO MKAMI ni Mmoja wa wachezaji mizigo!

Jemedari Said hakumjibi Kashasha yule. Kilichofuata ni Himid kuitwa Tanzania National team and thereafter, kawaomba Azam Fc wasimuongeze contract ili aweze kutimiza ndoto ya kucheza Nje! Hatimaye ndoto imetimia!

Naheshimu maoni na mtazamo wa Kashasha mleta mada. Jicho la mleta mada ndio Jicho la watanzania wengi. Watanzania wengi wanapenda soka la MVUTO MACHONI!

Watanzania wanataka SHIW GAME KWANZA kisha matokeo baadae. Hawa hawawezi kumkubali mtu kama Samatta. Hawawezi kumkubali mtu kama himid Ktk team!

Man U walikuwa na mtu anaitwa Ruud Van, jamaa kafunga 85% ya magoli yake ndani ya 18. Hana mbwembwe! Hajui kupiga chenga! Lkn jamaa ana uhusiano mzuri na nyavu!

Humu wengi mnamkumbuka sana Jay Jay Okocha. Bonge la Mchezaji. Lakini ndani ya EPL hana la maana la kujivunia, ukiacha kuwa alichezea BOLTON WONDERERS, hamna kikubwa alichofanya zaidi ya yale matobo, kanzu na vyenga alivowapiga wachezaji wa timu pinzani! Soka halina tuzo za mambo kama hayo!

Mtazame John Bocco. John Bocco wa Azam hana tofauti na John Bocco wa Simba. Edo Kumwembe aliwahi kumsifia John Bocco zamani sana na akasema watanzania wanasubiri Bocco acheze Simba ama Yanga ndio wamuimbe! Leo ndio hicho kinatokea!

Tabia hii ya kupenda vitu visivyo na maana uwanjani ndio imefanya Ngassa mpk leo awe pale alipo! Ngassa alikuwa anapiga chenga afu anaangalia Jukwaani kwa nyodo! Mashabiki wanamshamgilia! Hapo timu ipo nyuma ama haina goli! Ngassa yule angeweza kukupiga kanzu, tobo, kanzu tena afu mpira akarudisha kwa kipa!

Kashashas mtoa mada badili mtazamo wako kuhusu soka la kileo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…