OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 53,868
- 121,001
BAADA ya Simba kukabidhiwa kombe la ubingwa wa FA bila zawadi ya pesa, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limesema itakabidhiwa fedha wakati wowote.
Simba imetwaa ubingwa wa kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) baada ya kuichapa Yanga bao 1-0 kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma, juzi.
Baada ya ushindi huo, Simba ilikabidhiwa zawadi ya kombe bila pesa taslimu Sh50 milioni ambazo hutolewa kwa bingwa.
Jana, Rais wa TFF, Wallace Karia alisema suala la zawadi ya mshindi lipo chini ya mkurugenzi wa Mashindano, Salum Madadi au katibu mkuu wa TFF, Wilfred Kidao.
“Lini bingwa wa FA atakabidhiwa zawadi ya pesa hilo linashughulikiwa na mkurugenzi wa mashindano na katibu wao ndiyo wana ratiba ya jambo hilo,” alisema Karia.
Madadi alipoulizwa alisema mchakato wa kukabidhi zawadi kwa bingwa utafanyika wakati wowote na Simba itakabidhiwa pesa zao.
My Take:
Mbona Azam Tv walikuwa na mabango mengi sana. Yaani 50m kweli? Au hii ni hela ya TFF tu, kuna donge la Azam?
Simba imetwaa ubingwa wa kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) baada ya kuichapa Yanga bao 1-0 kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma, juzi.
Baada ya ushindi huo, Simba ilikabidhiwa zawadi ya kombe bila pesa taslimu Sh50 milioni ambazo hutolewa kwa bingwa.
Jana, Rais wa TFF, Wallace Karia alisema suala la zawadi ya mshindi lipo chini ya mkurugenzi wa Mashindano, Salum Madadi au katibu mkuu wa TFF, Wilfred Kidao.
“Lini bingwa wa FA atakabidhiwa zawadi ya pesa hilo linashughulikiwa na mkurugenzi wa mashindano na katibu wao ndiyo wana ratiba ya jambo hilo,” alisema Karia.
Madadi alipoulizwa alisema mchakato wa kukabidhi zawadi kwa bingwa utafanyika wakati wowote na Simba itakabidhiwa pesa zao.
My Take:
Mbona Azam Tv walikuwa na mabango mengi sana. Yaani 50m kweli? Au hii ni hela ya TFF tu, kuna donge la Azam?