Mch. Mwasapile vs. Mch. Rwakatale


Wawewza kuniambia kwanini wana waisrael walitakiwa kuimgeukia yule nyoka wa shaba aliyewekwa na musa na sio wageukie upande mwingine. waweza pia kuniambia kwanini wengine waliambiwa wakajichovye marasaba kwenye mto wenye maji machafu wa Yordani na wengine wakaambiwa imani yao imewaponya? Usijemjaribu mungu kwa imani finyu uliyonayo, na wala usije ukadhani ati neema hii itashuka israel au kwa yeyote mwenye ngozi ya rangi nyeupe na wala usijaribu kuwakatisha tamaa wengine wenyematatizo na imani ya kupata neema hii ya babu.

Mungu kamwe hawezi kuwaponya wanafiki na wenye imani haba.
 
Kitu kimoja nimegundua, Miss Judith tayari ana majibu kichwani mwake. Hivyo wote mnaomshauri mnajisumbua bure, tazameni ni post za aina gani alizoweka Thanks. Wa Ndima amemweleza vyema kabisa mbona hakupiga Thanks
 
Samahani sana mkuu yaani "babu" unataka kumfananisha na Yesu????????? Khaaaaa yaani wewe jamaa wa ajabu sana unamfananisha Messi na Ngasa?! Yesu ni world ICON huwezi kumfananisha na mtu wa kawaida mkuu..............

Kaka unaweza kumfananisha Messi na Ngassa nawala si Yesu na Babu, so hata wewe umejaribu kuweka vitu kwenye mzani visivyo pimika
 
Ikumbukwe dawa ya mti anaoutumia babu ni mti unaotumiwa na wamasai kutengenezea sumu ipakwayo kwenye mikuki na mishale ya kuwindia wanyama na kulindia mifugo yao.

Kisha naona tatizo lingine linalokupa tabu ni Ndoto anayoisema babu labda tukudadavulie NDOTO kwa maana ya kiroho na kiimani ni kama UFUNUO, kumbuka YUSUFU alifunuliwa kuwa atakuja kuwa kiongozi juu ya kaka zake na ile ilikuwa ndoto. Mungu humjia binadamu kwa namna tofauti, Mfano

Mariam mama wa Yesu - malaika
YUSUFU - Ndoto
Musa - Sauti ya Mungu
Mtume Paulo-?
Isaya-?
Samweli-?
 
Kitu kimoja nimegundua, Miss Judith tayari ana majibu kichwani mwake. Hivyo wote mnaomshauri mnajisumbua bure, tazameni ni post za aina gani alizoweka Thanks. Wa Ndima amemweleza vyema kabisa mbona hakupiga Thanks
umemsoma Miss Judith ukamwelewa? yeye hajaomba ashauriwe kama aende kwa babu au lah, ila anawatahadharisha watu wanaoenda huko kuzingatia mambo kadha wa kadha.
 

mwisho wa dunia utakuja kwako mwenewe, biblia huijui bora ukaekimya au uombe kuelimishwa.
 

Mimi sioni sababu ya kuogopa.Tumeamriwa tukemee uovu.Babu anachofanya ni uovu na Mungu wa Mbinguni hapenzwi na uovu huo hata kidogo.Shetani anamdanganya.Ingekuwa heri kwake kama angecha mara moja.
 
Wazungu na Waarabu walileta dini Afrika ili waweze kututawala vizuri nafikiri lengo lao limefanikiwa sana ... tunapoteza muda mwingi sana kwenye mambo ya dini na kubaki nyuma huku wao waliozileta hizo dini wakipiga hatua kila siku na sisi kubakia karne ya 18 ..hatuwezi hata kutengeneza toothpick wakati miti imejaa kila mahali.
 

The new testament asks us to question the spirits in operation. All miracles performed after redemption were through the name of Jesus which is the power above all in heavens and on earth. Its important to note that during Jesus time so was during prophets and priests before He came used media to perform miracles because the holly spirit was not yet released into the world. Alikuwa anavuvia watu au vitu na hivyo kusababisha miracle kutokea; lakini sasa yupo available in whoever believeth in the above all name Jesus. Hahitaji tena hizo media for our bodies are His temple and he uses our body organs to perform miracles. Bali katika yote bado nguvu na uweza una yeye Mungu wetu; kama la toka kwa Ibilisi halitadumu na itaonekana wazi lakini kama ni la Mungu basi If God say yes who can be against?
 

thanks my dear. ubarikiwe sana.

mi hoja yangu ni kuwataka wote tuwe na kawaida ya kutafakari na kujaribu (ku-test) kila kinachoitwa revelation. kupokea tu ndoto au ufunuo eti kwa kuwa imekuja "kupitia mchungaji" ni kukubali bila sababu yoyote kuwa we are not resposible Christians. hao wanaonishambulia eti nampinga au namhoji Roho Mtakatifu na kunukuu mafungu tele tele ya biblia, wamerukia tu kuhitimisha kuwa "......hiyo ni kazi ya Roho Mtakatifu" bila kui-test! na hii ni hatari kwani siku moja hata shetani ataleta ndoto (na amekwishaleta nyingi sana) na watu watajazana kwake na hatimaye kuangamia pamoja naye kwa kukosa maarifa.

kumbukeni kuwa imani ya kikristo ni tofauti na imani nyingine. hii inaanzia kwenye (brain) rationality na kukua kuelekea spirituality na si kinyume chake. wote wanaokimbilia kusema kuwa "masuala ya imani magumu kueleweka" au "Roho Mtakatifu ana namna nyingi za kutenda kazi na ni ngumu kuzielewa kwa akili zetu" nk wanakimbia wajibu wao. wanajaribu kutuaminisha kuwa imani ya kikristo huanzia kwenye spirituality kushuka chini kwenye brain (rationality), na hivyo haiwezekani kuzielewa basis za imani!. ni uongo mkubwa sana huu na ni silaha ya ibilisi ili watu waangamie kwa kukataa kwa makusudi kutafuta maarifa.

ufunuo wowote unaokuja nje ya neno la Mungu haupaswi kupita bila kuhojiwa. Roho Mtakatifu si lazima adhihirishwe kwa miujiza. Mungu hujishughulisha na kuponya roho na si kuponya Mwili. hata pale mwili unapopona ni kwa sababiu roho imepona na hivyo uponyaji wa rohoni umepelekea uponyaji wa mwili. uponyaji wowote uanziao kwenye mwili bila kuzingatia uponyaji wa roho, ni wa kuhojiwa.

neno la Mungu ni kamili na halihitaji miujiza ili liwe kamili au lipate nguvu. kama maelfu ya watu wamiminikao loliondo leo wamekuwa wakisikia injili kila siku wasiamini, ila leo wakasema wanaamini kwa sababu wameona ishara ya dawa ya ajabu, basi hilo haliwezi kupita bila kuhojiwa na wenye kuamini neno la kweli. pia haijathibitika kuwa wote wanywao ule mti humrudia Mungu kwa toba bali inajulikana kuwa kila anywaye hujiondokea zake na habari kuishia hapo. Mungu ninayemfahamu hana tabia hiyo.

neno la Mungu liiko wazi, alikuja kuokoa na kutafuta kilichopotea, na ndio maana hata wakati wa Yesu ama Elisha (kama wengi walivyotoa mifano ya Naamani mshamu aliyeponywa ukoma na wengine walioponywa) si kila aliyekuwa na ukoma laiponywa! tafakarini sana hapo ndugu zangu.

Yesu mwenyewe alituonya mara nyingi sana tusiwe vipofu na kutahadharisha kuwa kipofu akimongoza kipofu mwenzie, wote watatumbukia shimoni. kwa msingi huuu, ni wajibu wa mkristo kuzijaribu kila roho ili kuona kuwa zimetokana na Mungu.

mwenye kuweza kutafakari na atafakari. mimi nimetimiza wajibu wangu

Glory to God
 

Mkuu nakubaliana na wewe.....

Huyu babu angekuwa Mzungu, na anatoa tiba hii huko Yerusalem hakuna ambaye angeingiwa na mashaka........hata Judy mtoa mada.

Tatizo hapa babu Mnyakyusa, Huduma anaitolea Loliondo......Mashaka kibao!

Hivi alishawahi tokea mwafrika akaitwa nabii, mtume, mtakatifu na majina yoyote mazuri?...Waafrika tumemkosea nini Mungu? Hivi ni kwanini hata picha za shetani wanazochora wasanii huwa zinakuwa na rangi nyeusi na zile za malaika na watakatifu huwa nyeupe?......Waafrika tumelaaniwa au tunajishusha wenyewe?

Agrrrrrrrrrrrrr!!
 
Naaman, yule ambaye alikuwa na ukoma aliwaambiwa akajichovi mara saba kwenye mto Yordan atapona ukoma wake, akaenda akajichovva mara saba........ngozi yake ikatakasika kama ngozi ya mtoto mchanga..................
 

Nakuunga mkonao: Waafirka hatulalaniwa na Mungu, ila wazungu walileta neno la Mungu likiwa limevaa utamaduni wa Kizungu ili kumpumbza Mwafrika ajione duni atawaliwe kirahisi. Utakumbuka vitu vya asili vyote walii ushenzi na ushetani .....hata kucheza ngoma za asili, dini za asili, uongozi wa kiukoo....... watu wakafundishwa elimu ya kizungu yenye ubaguzi kuandaa vibaraka...................Tangu waafrika walilogwa na wazungu kwa nama hiyo. Halafu kibaya zaidi, wazungu wakabaki na umoja wao, waafrika wakaendelea kutengana kinoma......Angalia United State of America...... sasa hebu linganisha na Jumuiya ya Afrika Mashriki ambaye ni URAFIKI WA MASHAKA, HAKUNA ANAYEMWAMNI MWENZAKE......
 

Dada Judith,
Mambo ya MUNGU hayapimwi kwa theolojia hata kidogo bali kwa ROHO MTAKATIFU. Tunahitaji kukaa sana katika uwepo wa MUNGU maishani mwetu ili ROHO MTAKATIFU atufunulie ni kipi cha kweli na kipi si cha kweli vinginevyo twaweza kujikuta tukataa huduma ya MUNGU au kukubali huduma isiyotokana na MUNGU. Kuhusu suala la vitambaa yaweza ikawa si MUNGU kama mtumishi mwenyewe hayuko na MUNGU na inaweza ikawa ni MUNGU kama mtumishi mhusika yuko na MUNGU vizuri maana tunaona hata enzi za mtumishi wa MUNGU Paulo watu waliponywa kwa vitambaa.


Acts 19 (Amplified Bible)


11And God did unusual and extraordinary miracles by the hands of Paul,

12So that handkerchiefs or towels or aprons which had touched his skin were carried away and put upon the sick, and their diseases left them and the evil spirits came out of them
 

Hapo kwenye blue ndo msisitizo the power was in Paul na siyo handkerchiefs...Hata kunasehemu kivuli chake kilipomgusa mtu alipata uponyaji...Nasisitiza roho matakatifu yupo ndani yetu sasa hivi kama alivyokuwa kwa Yesu so its not about media its about the power that worketh in us...ndiyo maana nashindwa kum qualify mchungaji/babu au kum disqualify maana anasema dawa lazima akupe kwa mkono wake which means the power is inside him...Lakini pia a devil can do miracles in the same maner ndiyo maana lazima tuipe muda ili kweli ijidhirishe huku tukiendelea kuomba..Kitu kingine ni kuwa ili uwe muujiza wakimungu lazima uthibitishwe na vitu vitatu so far Babu peke yake ndiyo mwenye revelation why? Hii ni kanuni ya Mungu kwamba ushuhuda wa watu watatu ndiyo kamili...Time will tell.
 

Mkuu hapa mwenye kuponya ni MUNGU na si Paulo. Nguvu iliyokuwa ndani ya Paulo ni nguvu ya MUNGU inayoweza kuwa ndani ya mtumishi mwingine yeyote leo akijitoa kumtumikia kisawasawa. Nguvu hiyo yaweza kuwekwa kwenye vitambaa kwa kuombewa na kupelekwa kwa wagonjwa na wakapokea uponyaji.
 
Jamani wale wote mnaotilia mashaka juu ya uponyaji wa babu kule loliondo, IMANI jamani kila mtu ana imani yake, kama babu anawaambia watu kuwa ukinywa dawa unapona na watu wakanywa dawa wakaponywa tatizo liko wapi? MUNGU ni wa ajabu sana na anaweza kumtumia mtu yeyote yule kufikisha ujumbe wake au anaweza kumtumia malaika pia. kama ameamua kumtumia babu kwa sasa unapaswa kufurahia uponya wa mungu otherwise unapenda watu waendelee kuteseka na magonjwa yao. sijui kama unaweza kuwa na moyo wa namna hiyo, wa kufurahia watu wanapoteseka na mara wanapopata mponyanji unaanza kuhoji kwa nini anaweka masharti katika uponyaji wake.
Ni mawazo yangu tu jamani.
 

.
Naunga mkono hoja.
Ila katika kitabu cha biblia tunachokiamini kuna aya inawataka wanawake wenye kuukiri uchaji wafunikwe kwa mavazi ya kusitiri (dicent).
Avatar yako inaunga mkono ushauri huo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…