Mch.Rwakatare CCM amedanganya Kamati maadili 1bls Kawe beach!!!

+ KAMATI YA WAKRISTO YA KUITETEA IMANI+
(Wafilipi 1: 27-30, Yuda 1: 3-4, 1Petro 3: 14-16)
P.O. Box 3885 Simu 0755 885095 au 0773 630516
13 March, 2008. Rev Dr. Getrude Rwakatare Mikocheni B Assemblies of God DAR ES SALAAM Mtumishi wa Mungu YAH: MATOLEO YA SH. 40 MILIONI ZA KUGHARAMIA MAKESI YA KI-KATIBA YA KUULINDA UKRISTO NCHINI Tafadhali husika na kichwa cha habari, pamoja na taarifa mbaya zilizomfadhaisha kila Mkristo mwenye mzigo juu ya hatima ya Imani yetu katika nchi hii, za kutupiliwa mbali kesi ya ki-Katiba Nambari 80/2007 iliyokuwa imefunguliwa na ndugu yetu Mchungaji Christopher Mtikila katika Mahakama Kuu kabla ya Bunge la Mwezi October 2007. Baada ya kesi hiyo kuahirishwa mara tatu kutokana na kukosekana wanasheria wa kumsaidia huyu mtumishi wa Mungu, ilipofika tarehe 26 Februari 2008 Mwanasheria Mkuu wa serikali aling'ang'ana kuwa Jopo la Majaji waifute kesi. Kwa mujibu wa Sheria Waheshimiwa Majaji Massati, Makaramba na Nyerere wakatoa uamuzi kwamba wanaifuta kesi kwa sababu ya msingi kwamba Petitioner hakuwa amejitayarisha kwa kesi hiyo, na kushauri kwamba Petitioner atakapokuwa amejitayarisha ndipo aiwasilishe upya Mahakamani. Hadi kufikia hatua hii ya kusikitisha, kesi hii ilitufariji Wakristo wote nchini kwamba ndiyo luku aliyoitumia Mungu wetu kuuzima mkakati uliokuwa umeandaliwa kuupitisha muswada wa kuuingiza Uislamu katika Katiba ya Jamhuri, kwa kutumia kikao cha Bunge cha Mwezi October mwaka jana. Wakristo wote tunajua kwamba kesi hii ni nyeti sana kwa sababu inapinga kuingizwa Uislamu katika Katiba ya Nchi, kwa sababu kufanya hivyo ni kuupa Uislamu nguvu ya Sheria kama dini rasmi ya Taifa, ndipo Jihad iweze kutokomeza kirahisi ukafir (Ukristo) kwa kutumia nguvu hiyo ya ki-Katiba, hatua kwa hatua au kwa upanga moja kwa moja. Lakini pamoja na maombi yote ya Wakristo, sote tunajua kwamba crusade hii inahitaji msaada mkubwa wa kitaaluma huko Mahakamani, ambao una gharama kubwa asiyoiweza mwenzetu, pamoja na uhanga alionao kwa ajili ya Kristo. Pengine kwa kuhofia udini mkali wa Rais Jakaya Kikwete, pamoja na vitisho vya mashehe visivyo na madhara yoyote kwa Mkristo, wanasheria wengi ama walikwepa kuwakilisha au walitaka mamilioni ya fedha ambayo sote tunajua kuwa mwenzetu hanayo, hivyo kwamba yanahitajika matoleo ya Wakristo kwa kadri ya mzigo walio nao kwa ajili ya Mungu wao. Wakristo wote hili wanalijua, na mabilioni ya mapesa yako mikononi mwa Wakristo. Lakini hatari ya kutokuwepo Ukristo wa kweli nchini yaani uhanga kwa ajili ya Bwana wetu Yesu Kristo ndiyo ambayo Roho wa Mungu tuliyemhuzunisha ameidhihirisha kwa kufutwa kwa kesi hii! Shuhuda zinatoka kila kona ya nchi Waislamu wanavyowatambia na kuwazomea makafir, na bilshaka nguvu zinakusanywa na wakuu wa Jihad nchini walioshika dola kutokana na usaliti wetu sisi wenyewe, ili wakamilishe usilimishaji wa Taifa. Tayari wanahimizwa usiku na mchana na vinara wa ugaidi, Iran, Libya, Sudan, Oman, Al-Qaeda na wenzao.
GHARAMA YA KUIREJESHA KESI MAHAKAMANI WIKI HII
Mtumishi wa Mungu, tunaomba uwezeshe kurejeshwa kesi hii Mahakama Kuu wiki hii, shetani asipate nafasi! Ni shilingi 40 milioni za kutupa ushindi. Tunalazimika kugharamia kesi kadhaa za kuvunja nguvu ya Jeshi la Polisi, ambalo Rais Kikwete na Saidi Mwema katika kutekeleza mikakati ya OIC/IAO wanalitumia kuuzima Ukristo kwa kuzuia usihubiriwe, na hasa vikundi vya "Biblia Ni Jibu" ambavyo vinaposikiwa vizuri na Waislamu huwalazimisha kuuacha Uislamu na kuja kwa Yesu. Zaidi ya mikutano 50 ya hadhara ya Wakristo imevunjwa kikatili na askari wenye silaha. Wahubiri wengine kupigwa vibaya na kunyimwa PF 3 na kutupwa ndani. Kwahiyo dawa pekee ni kuwafikisha kizimbani makamanda kadhaa wa Wilaya na/au Mikoa na kuwafanya walipishwe fidia kubwa sana ya kupigwa minada majumba, magari na mashamba waliyojipatia kwa rushwa, pamoja na kuwafungulia mashitaka ya jinai. Matangazo ya kesi hizo katika vyombo habari na kwenye majukwaa yote ya Wakristo nchini itawakomesha kabisa Polisi kuigusa mikutano ya Wakristo, ndipo sisi tutaendelea kuwavuna Waislamu WOTE na kuifuta dini hii kutoka Alexandria mpaka Cape of Good Hope. Tuna mzigo pia juu ya ufunguzi wa kesi maalum ya Katiba ya kuyarudishia Makanisa shule, vyuo na mahospitali ambavyo vilitaifishwa, pamoja na fidia na gharama za matengenezo. Tumeamua pia kuwasilisha katika Mahakama Kuu kesi ya Katiba ya kukirejesha Chuo Kikuu cha TANESCO walichopewa Waislamu kinyume cha Katiba kikawa "Islamic Univerysity". Tunahitaji msaada pia kwa ajili ya azma yetu ya kudai mapesa yote ambayo serikali imeyatumia kwa ajili ya Hija ya Waislamu, kama zile Bilioni 2.5 alizowachotea Rais Kikwete safari hii walipokwama Uwanja wa Ndege. Wakristo wanayo hija katika Nchi Takatifu, yenye maana kuliko hiyo ya Waislamu ya kwenda kutazama jiwe Arabuni wakati tunayo mawe mengi sana hapa hapa kama Mwanza. Tunataka kiasi kile kilichotumiwa kwa ajili ya Waislamu kitolewe pia kwa Wakristo, halafu serikali ikomeshwe kabisa kugharamia ibada ya dini zote. Kamati inaomba ushirikiano wako sana katika kuulinda Ukristo nchini, kwa kuimarisha secularism, na Basic Human Right to Freedom of Worship, ambayo mhimili wake duniani kote ni religious tolerance, ambapo kila mtu analazimika kuvumulia imani za wengine pale zinapokuwa makufuru au matusi kwake, kama ambavyo watu wote wanalazimika kuivumilia ya kwake yeye. Yaani kama Mahakama ya Rufaa ilivyohukumu katika kesi ya Hassan Dibagula kwamba hakukosea alipoutukana Ukristo (ukafir) kwamba Yesu si Mungu wala si mwana wa Mungu kwa vile Mungu hakuoa wala hukuzaa, kwa sababu ndiyo imani yake inavyosema katika vitabu vya dini yake na uhuru wa kuamini hivyo anao chini ya Ibara ya 19 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Uhuru wa Kuabudu, hivyo kwamba kosa wanakuwa wametenda Wakristo kama hawawavumilii Waislamu imani na mafundisho yao yanapokuwa makufuru na matusi dhidi ya Ukristo, vivyo hivyo Waislamu wanatenda makosa makubwa kisheria wasipowavumilia Wakristo wanapowahubiria kwamba Uislamu ni ugaidi na ushetani, tena kwa uthibitisho hata wa maandiko ya Uislamu wenyewe yanayosisitiza hivyo. Maono ya kuirejesha nchi hii Takatifu kwa Bwana yatafanikiwa kwa kuwaacha wajahidina wautukane Ukristo kama walivyofanya siku zote (kwa kuzingatia kwa dhati haki ya uhuru wa kuabudu), kusudi na sisi tujithibitishie haki ya kujibu hoja zao na kuumaliza kabisa Uislamu nchini. Mkakati huu uendeshwe sambamba na Uamsho wa nguvu utaopokea hayo mavuno na kuyajenga katika Neno la Uzima na maisha mapya hata ya kimwili. Waislamu wanajivunia mafanikio ya mkakati wa OIC/IAO ulioanza mwaka 1986, wa Islam kukamata uchumi wa nchi ili makafir (Wkristo) wabaki katika utwana, kwamba umefanikiwa kwa kuweka asilimia zaidi ya 80 ya utajiri mikononi mwao, na sasa wanakazana kukamata ardhi yote nchini. Kamati imo katika kubuni mikakati ya ukombozi wa kiuchumi wa Wakristo nchini, na tumefunuliwa kuanzishwa Benki maalum kwa lengo hili. Lakini mtumishi wa Mungu tunaomba kwanza msaada wako kwa ajili ya dharura hii ili tuvuke hili jaribu la hatari kwa kuirejesha kesi Mahakamani wiki hii. Mungu akubariki. Askofu Isack Kalenge MWENYEKITI NB: Matoleo yako ukiandika cheque unaombwa kui-address kwa Life Ministry (Kamati maalum ya Wakristo), waliojitolea Kamati itumie account yao kwa dharura hii.
 
Yaelekea mama huyu ni mbwa mwitu katika mavazi ya kondoo kwani tuhuma zinazojifunua zinazidi kuthibitisha hilo. Ama kweli Yesu alisema; "Mtawatambua kwa matendo yao". Huyu mama anapenda pesa, umaarufu, kujikweza na yuko tayari kufaanya lolote ili kufikia malengo yake hayo! Pole zao wanaoendelea kumwamini.
 
Kiulizwe chama kilichompa ubunge, ama kweli ndege wanaofanana huruka pamoja
 
kama dini inalipa, na sisi tuingie tufaidi

Bujibuji dini siku hizi inalipa kwani juzi nimeshangaa jamaa mmoja tumekua nae magomeni Mikumi enzi hizo nae siku hizi ana kanisa lake, na mkewe amekuwa mfanyabiashsra mkubwa nchini; chakushangaza ni kuwa familia ya jama huyu siku nyingi wanajishuhulisha na biashara ya madawa ya kulevya hivyo mimi nahisi hili kanisa ni gelesha tu ya biashsra yao!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…