Chachu Ombara
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 6,067
- 10,938
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ndugu Nape Nnauye, akizungumzia mafanikio ya safari ya ujumbe wa Rais Samia nchini Korea Kusini amesema kuwa...
Wenzetu wamepiga hatua kubwa kwenye miundombinu ya mawasiliano, hapa kwetu tunaendelea na uwekezaji, uwekezaji huo ni gharama, kingine wenzetu wanazalisha smart device kwa maana ya simu janja n.k, sisi kwetu tuna changamoto ya kusambaa kwa vifaa hivyo kwasababu ni ghali, moja ya eneo ambalo tumezungumza kwa kina ni kuona namna ambavyo tunaweza kushirikiana nao tukazalisha hapa kwetu kwa maana ya kuviunganisha vifaa ambavyo vitakuwa kwa bei nafuu ili Watanzania waweze kuvimudu
Najua swali kubwa hapa ni kwamba miundombinu vijijini ikoje, mtakumbuka bajeti yetu iliyopita tumetangaza mchakato wa kuwa na satelaiti yetu kama Nchi, mchakato huo unaendelea vizuri, zipo Timu zimeenda Duniani, Katibu Mkuu na Timu yake walikuwa China, wengine wataenda Marekani na kwingine , baada ya pale pamoja na miundombinu mingine ambayo tunaendelea lakini hili la kuwa na satelaiti yetu kama Nchi linaendelea vizuri na changamoto hizi zitapungua
Lazima tujenge utamaduni aa kufanya kazi huu utamaduni wa Watu wanashinda mtandaoni masaa 24 halafu baada ya pale mfukoni hamna kitu huu utamaduni lazima tuupige vita vinginevyo hatuwezi kutoka, na ni kupitia kazi, Watu wasifikiri kuna Mjomba atakuja mahali akuletee maendeleo ya maisha yako
Wenzetu wamepiga hatua kubwa kwenye miundombinu ya mawasiliano, hapa kwetu tunaendelea na uwekezaji, uwekezaji huo ni gharama, kingine wenzetu wanazalisha smart device kwa maana ya simu janja n.k, sisi kwetu tuna changamoto ya kusambaa kwa vifaa hivyo kwasababu ni ghali, moja ya eneo ambalo tumezungumza kwa kina ni kuona namna ambavyo tunaweza kushirikiana nao tukazalisha hapa kwetu kwa maana ya kuviunganisha vifaa ambavyo vitakuwa kwa bei nafuu ili Watanzania waweze kuvimudu
Najua swali kubwa hapa ni kwamba miundombinu vijijini ikoje, mtakumbuka bajeti yetu iliyopita tumetangaza mchakato wa kuwa na satelaiti yetu kama Nchi, mchakato huo unaendelea vizuri, zipo Timu zimeenda Duniani, Katibu Mkuu na Timu yake walikuwa China, wengine wataenda Marekani na kwingine , baada ya pale pamoja na miundombinu mingine ambayo tunaendelea lakini hili la kuwa na satelaiti yetu kama Nchi linaendelea vizuri na changamoto hizi zitapungua
Lazima tujenge utamaduni aa kufanya kazi huu utamaduni wa Watu wanashinda mtandaoni masaa 24 halafu baada ya pale mfukoni hamna kitu huu utamaduni lazima tuupige vita vinginevyo hatuwezi kutoka, na ni kupitia kazi, Watu wasifikiri kuna Mjomba atakuja mahali akuletee maendeleo ya maisha yako